Kuhusu Morogoro a.k.a mji kasoro bahari

Kuhusu Morogoro a.k.a mji kasoro bahari

Moro nilikaa Kiwanja Cha Ndege maji ilikuwa ni Shida,nikahamia Mazimbu Kule mbele ya Neema Dispensary,yaani maji ilikuwa full kujiachia kila siku yanatoka kuanzia saa tisa mpaka saa moja asubuhi.Maisha ni poa tu.Ila Sehemu.nyingine maji ni Shida lkn huwezi linganisha na Dar.Ni junction nzuri sana Moro.Ila sio mji mkubwa ni mji mdogo lakini unakua kwa kasi.Halafu pale kati mjini,na kule manzese yale maeneo yangeendelezwa kwa kujengwa majumba makubwa.
 
Ukweli kuhusu moro pia, ni mji ambao watu wabara wengi huamia kwa kasi kwa sababu kuna fulsa nyingi za kimaendeleo. Wengi wao wapo maeneo ya kihonda,,,,,,mnakaribishwa jamani mje Moro mji mzuri, una matunda mengi mno...na pia mzunguko wa pesa ni mkubwa ila kasoro kubwa jamani ni upatikanaji wa maji tu...na maji yapo mengi ila utendaji mbaya wa viongozi.

Vipi Abood hajachimba visima kihonda? Ila Moro utakuja kuwa mji mkubwa tu watu wa mipango miji wajitahidi,kule kihonda mizani ndani ndani kule,halafu kwendea Mzumbe kasanga kule kukiendelezwa nauona mji mwingine Tanzania,Dar ni chumbani na Sebuleni ni Morogoro
 
Vipi Abood hajachimba visima kihonda? Ila Moro utakuja kuwa mji mkubwa tu watu wa mipango miji wajitahidi,kule kihonda mizani ndani ndani kule,halafu kwendea Mzumbe kasanga kule kukiendelezwa nauona mji mwingine Tanzania,Dar ni chumbani na Sebuleni ni Morogoro
Abood alichimba sijui idadi ya visima...ila havikidhi mahitaji, mji umepanuka sana kwa sasa. Kwahyo mamlaka husika inabidi zibadilishe miundo mbinu ili iendani na idadi ya watu. Mfano, barabara kutoka msamvu kuenda town ni nyembamba...na pia waboreshe masuala ya maji. Mji huu unakuwa kwa kasi mno....
 
Haya mchambuzi wa kimataifa na mtu wenye akili kupita wote humu ndani

Na Kweli Hujakosea Nina Uwezo Wa Kufikiri Kushinda Wewe Kwani Kwa Kunijibu Kwako Tu Hivi Umeshadhihirisha Kuwa Wewe Ni POPOMA, Shikamoo.
 
pale msamvu stend kubwa-moro
maendeleo ni ya miaka ya juz tu.. zamani palikuwa na vumbi sn.

kdg wameboresha..
 
Abood alichimba sijui idadi ya visima...ila havikidhi mahitaji, mji umepanuka sana kwa sasa. Kwahyo mamlaka husika inabidi zibadilishe miundo mbinu ili iendani na idadi ya watu. Mfano, barabara kutoka msamvu kuenda town ni nyembamba...na pia waboreshe masuala ya maji. Mji huu unakuwa kwa kasi mno....

Hiyo barabara ya msamvu kwenda mjini ni uzembe mkubwa wa manispaa na mkandarasi, yaani wameeweka barabara ya waenda kwa miguu kubwa kiasi kile....
 
msamehee...

ajatembelea profile yako...!?

Imebidi niitembelee kwa mshawasha aise labda ukijibu kwenye thread nyingine kama ulivoahidi ndo ntajua uspesheli wa hii profile,lkn otherwise mpaka sasa naitreat kama profile ya kawaida sana humu ndani ya JF
 
Wadau,

Nimekuwepo hapa Moro town kwa zaidi ya miaka 4 lakini hapo awali nimekua nikiishi nakusoma hadi high school huko mikoani. Nikiwa huko mikoani nidhahiri watu wamekua wakiisifu moro kua ni mahali pazuri sana, pana karibia kuwepo na kila aina ya starehe,majengo mazuri na vingine vingi.

Nikweli Moro mfano kwa wasafiri wakifika round about ya msamvu panamandhari nzuri nayakuvutia kwani inadaiwa msamvu ndio round about nzuri na kubwa kwa hapa Tz, pia Moro kwa tafiti ndogo nilizozifanya watu wa mikoa mingine hupaona Morogoro mahali fulani pako vizuri sana.

Kwa mimi nilichokiona moro nipakawaida tu nisawa tu au hata kuzidiwa na manispaa zingine, miundo mbinu na sehemu za vitega uchumi kiukweli bado sana yaani nitofauti sana Moro inavyotafsiriwa na watu ambao huwa wanapita tu bila Msamvu.

Tulitegemea Moro pengine kwa kua iko karibu na Dar mkoa wenye makao makuu ya shughuli nyingi zenye tija pia ianunganisha barabara kubwa za kuelekea kusini,kaskazini na Magharibi basi pangekua na vitega uchumi vikubwa na vyenye tija lakini bado mambo yanayofanyika ya kawaida sana.

Sijui wewe mdau unauzungumziaje mkoa huu mji kasoro bahari?

Nawasilisha.

Military base.
 
Morogoro, mlima uluguru mapambazuko asubuhi ya 22/03/2015 picture taken 15 km fara away from mount uluguru
 

Attachments

  • 1427028380493.jpg
    1427028380493.jpg
    156.8 KB · Views: 105

Similar Discussions

Back
Top Bottom