Kuhusu Manji: Shikamoo Tanzania

Kuhusu Manji: Shikamoo Tanzania

Tumeonesha unafki wa kiwango cha lami... Mungu hatatusamehe hasa kizazi cha kuanzia miaka ya 70 mpaka leo.
Kuanzia Mafisadi Papa yupo..(wote tulipaza sauti)
Kagoda (yupo wote tulipaza sauti)
PSPF & NSSF (yupo wote tulipaza sauti)
TANESCO (yupo wote tulipaza sauti)
COCO BEACH (Yupo na wote tulipaza sauti).

Watafuna nchi kumi (yupo wote tulipaza sauti)
Leo mungu kasikia dua zenu, mumebadilika completely kila mtu kaonewa mara chuki.

Tuacheni unafki Mungu anatuona mjue?....
NB: I have enough resources to respond to whoever comes with logical questions.
Wewe ndiwe mnafiki wa hali ya Jun. Maana unaandika vitu usivyovijua and kwa tamaa ya madaraka au Kwa kujifanya mwehu wakati una akili timamu.
Hatupingi juhudi yenye nia njema bali tunapinga usanii unaoendelea sasa hivi ama kwa chuki au kwa nia ya kukomoa watu wasio upande wenu.
Dhamira ya Makonda kwa Manji ni chuki binafsi au katumwa na Ridhiwani
 
Mods naomba ID yangu iheshimiwe na kulindwa. Manji na Gwajima mtakumbuka walifika kituoni siku moja na kulala wote chumba kimoja (SHIMONI), baada ya kwenda kwa mkemia ,kuu wa serikali Gwajima alliruhusiwa na kurudi kwenye makazi yake. Watu hawajiulizi kwanini Manji mpaka leo anashikiliwa na jeshi la polisi ila tu kutoa lawama kwamba anaonewa.
Issue ni kwamba Baada ya kwenda kwa mkemia Manji alionekana na kiwango kikubwa cha madawa ya kulevya na hivyo kulazimika kubaki na kusaidia upande wa jamuhuri ni wapi anapopata na hapo ndipo presha ilipoanzia.
oVa
Manji ndio engine ya mafanikio ya Yanga kwa miaka 5 mfululizo sasa, je, hakuna chembechembe za wa mchangani hapa? hakuna ajuae.
 
Tatizo mi nadhani si watu kulalamikia Manji kuonewa bali kinacholeta hii mitazamo ni ukiukwaji wa taratibu za nchi katika kukabiliana na uharifu huu.Kama sikosei kama Taifa ni wiki jana ndiyo tumegunda kwamba tunazo taratibu za kisheria za kupambana na uharifu japo zilikuwepo.Katika Mazingira kama hayo huwezi kulaumu mwananchi ambaye ana hisia kwa mbali kwamba taratibu za nchi hazijafuatwa katika kulishughulikia tatizo.
Wahalifu hawatumii taratibu za kisheria kufanya uhalifu, vivyo hivyo sometimes it's fair kutumia mbinu za kihalifu kulazimisha watu kufuata sheria
 
Manji ndio engine ya mafanikio ya Yanga kwa miaka 5 mfululizo sasa, je, hakuna chembechembe za wa mchangani hapa? hakuna ajuae.
hahahah we nae sijui umetoka wapi na akili zako za mgando, nani anayeweza kumweka Manji ndani kisa mpira ok fanya kawekwa ndani kwasababu ya mpira inamaana hataweza tena kusaidia timu? fuatilia Mois Katumbi wa TP MAZEMBE yuko wapi na timu yake ipo vipi kiuchumi.

comrade
 
One is proved guilty by the court of law and no one else
Let's wait for the interrogations & investigations comes to an end.. Why are you guys worried, mahabusu haijatengenezwa kwa ajili ya mbuzi au kuku
 
Waliobadilika ni Watanzania wachache ambao wameanza kampeni za Urais 2020. Kwao kila kinachofanywa na serikali ya JPM lazima kipingwe kwa nguvu zote
Sikushangai kwa kuwa unalinda kibarua pia ni mnufaika wa dhambi hii
 
Kutaja na kuwepo kwa ulichotaja ni vitu viwili tofauti kabisa, people are complaining the approach which is unconstitutional, mara madawa ya kulevya hamjampata, mnakimbilia uhamiaji na kusema na kulazimisha kuwa mwajiri kitu ambacho siyo kweli. Manji ni mtanzania mwekezaji to much police force, with lot of pampus, hii si sawa kinachoonekana hapa ni utekelezaji wa story za vijiweni 'kwamba huyu jamaa ni fisadi sana' no proof, keshokutwa kwako
Nani kakupa matokeo ya uchunguzi suala la Madawa?
 
Twambie tu uhusiano wako na Manji tuujue!
Manji ni mdhamini mkuu wa Yanga, ole wenu yanga ishindwe kulibeba kombe mtachukiwa hata na watoto wadogo. Watu watashindwa kutofautisha kati ya makosa ya Manji na chuki ya Simba dhidi ya Yanga kuongoza ligi
 
Kumbe nyakati zote tulipaza sauti? Kwanini hakukamatwa basi?

Tunachopaza sauti sasa kupinga uonevu huu ni aina ya tuhuma anazotuhumiwa nazo.

Madawa ya kulevya hana hatia,na hili sakata la uhamiaji kwa sasa hana hatia pia.

Tunachotaka ni atuhumiwe kwa haki,sio kuzunguka mbuyu.
Period
Ni kweli Nifah, tumemuhumu huyu mtu kwa mambo mengi ambayo kweli kama yangefuatiliwa yangekuwa na tija lakini kwa vile yaligusa kwenye mfupa hayakufanyiwa Kazi. Mnamtafuta kwa kuhakikisha issue haiwagusi watu wenu na wakati mtu huyo ana issue zinazogusa watu wenu na zina maslahi ya taifa mmeziacha halafu mnataka tuwaunge mkono.!! Tuiteni wanafiki, wazushi na mengine mtakayoona yanatufaa lkn hatuwezi kuficha udhalimu wenu wa kufichiana maovu na kutafuta mbuzi wa kafala.
 
Back
Top Bottom