Kuhusu maandamano ya kumpinga rais wa Tanzania Washington DC

Yona F. Maro

R I P
Nov 2, 2006
4,202
218
"No nation has the right to make decisions for another nation; no people for another people. "Julius Kambarage Nyerere, from his A
Peaceful New Year speech given in Tanzania on 1 January 1968. Nimesoma kwa masikitiko makubwa sana juhudi za Kundi la Wanaojiita watanzania wa nchini Marekani kufanya maandamano ya Amani kupinga Ziara ya Raisi wa Tanzania Nchini humo.

Nimejaribu kusoma Kundi hilo jina lake ni nini ? Sijapata , Kiongozi wake ni nani ? Sijaona popote badala yake nimeona watu wakijitambulisha kwa majina bandia ambayo sio yao kwa uhakika na matumizi ya Barua pepe wanazotengeneza Kila mara . Kwa kawaida watu wanavyoitisha maandamano kwanza wanakuwa na Agenda zao baada ya kujipanga na kufanya majadiliano kadhaa pia wanakuwa wameomba ruhusa za maandamano hayo ili kuweza kupata ulinzi na miongozo mengine kwa ajili ya maandamano hayo na mwisho wa siku wanakuwa na viongozi wao .

Kutokuwa na viongozi pamoja na agenda na masuala mengine muhimu kwenye maandamano madhara yake yanakuwa kama nchi ya Misri inavyozidi kuangamia sasa hivi kwa kukosa viongozi baada ya maandamano ya kuondoa utawala Fulani madarakani sasa hivi nchini humo kila mtu hamwamini mwenzake na hata maandambano hayajulikani viongozi wake haswa ili waweze kuweka jamii na nchi yao sawa . Utashangaa na kuona aibu ni maandamano gani yasiyokuwa na viongozi tena yanayofanyika katika nchi za watu na watu ambao hawajafika Tanzania kwa kipindi cha miaka 10 iliyopita na hawajui shida zozote zinazoikabili nchi kwa sasa hivi kwa vitendo zaidi ya kusoma kwenye mitandao bila kuchukuwa hatua yoyote .

Hawa ni watu waliosomeshwa kwa kodi zetu wenyewe wakaamua kuasi na kubaki huko na sasa wanaanza kutumiwa na nchi hizo kama vibaraka kwa kificha nyuso zao , majina yao na hata kujitenga na jamii nyingine za watanzania zilizoko Ulaya na Marekani kwa sababu hata vyama na jamii hizo hazitambui wito wa maandamano hayo wala wale walioyaandaa . Tunawataka watu hao warudi nchini , waje kujenga nchi na sasa hivi kuna fursa nyingi sana kwa sababu ya jumuiya ya afrika mashariki , Comesa , Sadc na nyingine nyingi ambazo nchi yetu imejiunga nazo .

Hizi ni Fursa ambazo waandamanaji hawajawahi kuzihoji wala kuzitumia badala yake ni kupanga maandamano ya kumdhalilisha kiongozi wa nchi pamoja na kuziba fursa nyingine kwa wale wanaotaka kujua zaidi kuhusu Tanzania haswa wageni na wawekezaji . Ni matumaini yangu watu hao wanaojiita watanzania watabadilisha mawazo na muelekeo wao na kuacha kutumia jina la watanzania waishio marekani kwa malengo ya kuharibu jina la nchi na viongozi wake bila kujali itikadi ya vyama vyao , makabila wala dini zao .

Wengine tunaopata fursa za kutoa maoni yetu kwenye mijadala kama mimi hapa , tutumie fursa hizi vizuri na kwa uhuru katika kuelimisha watu bila kuchoka na bila kuogopa vitisho vyovyote toka kwenye makundi ya watu wowote . "...intellectuals have a special contribution to make to the development of our nation, and to Africa. And I am askin understanding that they should possess, should be used for the benefit of the
society of which we are all members."Julius Kambarage Nyerere, from his book Uhuru na Maendeleo (Freedom and Development), 1973.
 
mkuu, mi nadhani kama kweli azma yao itatimia, bas watakuwa wamefuata taratibu zote zinazotakiwa na mamlaka za huko wanakoishi, kwa hiyo kama mamalaka za huko zitawataka wataje viongozi wao na matakwa mengine naamini watafanya hivyo na kinyume chake hawataruhusiwa.

kuhusu kumdhalilisha mheshimiwa rais, mi sioni kama ni ishu hapo kwani kuandamana ni kutoa mawazo tu ili wasikike maoni yao, ni mbinu ambayo watu wanyonge hutumia kuwashauri wakubwa hasa wale wasiofikika kirahisi. mfano hatuwezi kusikia mawaziri wakiandamana na mabango barabarani kwa sababu wao wana utaratibu wa kumshauri rais mara kwa mara kadiri inavyohitajika, lakini mfano mimi kama sijaridhishwa na mambo yanavyoenda, huyo raisi nitamshauri saa ngapi? na hii nchi ya kidemokrasia?

kuhusu utanzania wa wanaotarajiwa kushiriki, sina hakika kama una utata au la, ila kama ni watanzania, nafikiri tusiwaelewe vibaya. naamini kwa kuishi kwao nje ya nchi wameona tofauti ya maendeleo na namna yanavyopatikana hivyo kama raia wenye wajibu hawawezi kukosa namna ya kushauri na/au kushinikiza mabadiliko wanayodhani yanapaswa kufanyika, na ndivyo wanavyofanya hivyo sioni ubaya.

pia ni vizuri nyinyi mlio karibu na mheshimiwa rais mkamshauri kuwa sasa ni wakati muafaka ajifanyie tathmini mwenyewe juu ya safari zake za mara kwa mara na gharama za safari hizo huku nchi yake ikiwa hoi kuichumi na shida za wanachi zinaongezeka kila kukicha, na namna umma unavyoutazama uwajibikaji wake hasa wakati kama huu wa vizungumkuti kibao ndani ya nchi kama umeme, mafuta, sukari, rushwa nk badala ya kuwatazama kwa jicho baya kila wanaotaka kumuona akiwajibika zaidi. sisemi kuwa hawajibiki, bali nasema wengi wanataka kumuona akiwajibika ZAIDI.

mwisho nashauri tujitahidi kuona nguvu hizi za mabadiliko na kuzipa mtazamo chanya kwani haziwezi kuendelea kusitirika kama ilivyokuwa zamani. mabadiliko hayana budi kuja, jinsi maandamano yanavyoshika kasi nchini ndivyo na watz walio nje ya nchi wanavyozidi kuamka na kujiunga katika maandamano ili waweze kushiriki kwa vitendo michakato ya maendeleo ya taifa lao hata wawapo huko nje

natunaini nimeeleweka vyema,
ni mtazamo wangu tu na naweza kusahihishwa

asante
 
Shy yupo karibu na Rais gani, zaidi ya uopportunist tu? Huyu leo utamkuta anamuunga mkono Dr. Slaa mara kesho yupo kwa Magamba. Huwa haeleweki kabisa jamaa. Yeye anaishi kwa kuangalia ni wapi upepo unaelekea. Sasa hivi ameona ajipendekeze kwa CCM kwa style hii ya kujifanya anapinga maandamano. Keep on bro, pengine watakufikiria kwenye ukuu wa wilaya, si unajua bado hajateua?
 
Hakuna kurudi nyuma lazima tuandamane..Watanzania wenzetu wakiandamana wanapigwa na risasi zamoto wakidai haki yao..sasa tuone na nani atakayetupiga na risasi za moto..
Nidhamu ya woga ilikwisha habari yake..
 


Relax dude ... jazba na kashfa zote za nini.. jibu hoja kwa hoja.. kama huna hoja .. kaa kimya

Soma hoja iliyotolewa, kuanzia na crap na inakomalizia sentensi ndo jibu la hoja. Maandamano ni haki ya kidemokrasia na wananchi waliompa dhamana rais ili aongoze nchi ni haki yao kuandamana kama mambo hayaendi kama alivyoahidi.
 
Soma hoja iliyotolewa, kuanzia na crap na inakomalizia sentensi ndo jibu la hoja. Maandamano ni haki ya kidemokrasia na wananchi waliompa dhamana rais ili aongoze nchi ni haki yao kuandamana kama mambo hayaendi kama alivyoahidi.

sasa hayo maneno niliyoweka bold ndiyo majibu !!! sio pale juu uliweka jazba mbele ....
 


Relax dude ... jazba na kashfa zote za nini.. jibu hoja kwa hoja.. kama huna hoja .. kaa kimya

Kwa taarifa yako wengu humu si wanachama wa Chama cho chote cha siasa ila ni wapenda demokrasia ya kweli na maendeleo ya taifa letu. Mfano hapa chini nakuletea hotuba ya Makinda aliyotoa Bungeni juzi au jana, nimependezwa na mtazamo huo alio nao sasa Makinda na ndiyo tunayotaka lakini kushabikia bila akili wakati mtumbwi unazidi kuzama ni sawa na vuvuzela linalotoa tu sauti mradi limepulizwa na hewa yako au na upepo mkali ulioingia ndanimo.

Hii hapa ni hotuba ya makinda ambayo nampa big up na kama atatekeleza hivyo ndio kufanikiwa kuongoza vema bunge letu.

[h=2]Spika Makinda atoa kauli nzito kwa mawaziri[/h]
Spika wa Bunge, Anne Makinda, jana aliwashukia mawaziri baada ya kuwataka kufanya kazi waliyopewa kwani itafika kipindi watageukwa na ukumbi mzima wa Bunge. Aliyasema hayo jana mchana, muda mfupi kabla ya kuahirisha shughuli za Bunge.

"Hivyo nyie waheshimiwa mawaziri inawabidi mfanye kazi mliyopewa, itafika mahali mtageukwa na ukumbi mzima." Alisema wabunge, ambao wanawaunga mkono wapo, lakini ni vizuri na wao (mawaziri) wakafanya kazi zao kwa uhakika. Aliwataka mawaziri kufanya kazi zao kwa kujiamini kwa sababu wamepewa vitendea kazi.

Alisema wiki iliyopita alikuwa katika mkutano wa maspika wanaotoka katika nchi, ambazo ni wajumbe wa Jumuiya ya Madola.
Spika Makinda alisema mkutano huo, ambao hufanyika kila baada ya miaka miwili katika moja ya nchi wanachama, ulifanyika nchini Malawi.
Alisema katika mkutano huo wamekuwa wakijadiliana kuhusiana na mambo yanayohusu nchi zao na maspika wanashirikiana kupeana uzoefu kuhusiana na mambo wanayokubaliana.

Alisema miongoni mwa mambo waliyokwenda kuzungumza katika mkutano huo ni nafasi ya vyama vya upinzani katika Bunge kuweza kuimarisha demokrasia na kufanya maendeleo ya nchi kuonekana. "Kitu, ambacho napenda kuwashukuru, hamuwezi kuwa wabunge wa Tanzania halafu mkawa wabunge wa CCM, wabunge wa Chadema, wabunge wa NCCR, kwa maslahi ya wananchi hatufanyi sawa. Hivi sasa mlivyoanza mkikubaliana jambo kwamba hili ni la National Interest (manufaa ya taifa), mnasimama kama wabunge wa Tanzania, kitu ambacho ni kizuri," alisema.

"Lakini tuwe na hoja ya msingi ya kuwasaidia wananchi wetu wale wanaotusikiliza. Kwa hiyo, mimi nasema hili lazima tutofautishe. Kwa mfano mnapitisha bills (miswada) za sheria ya nchi haiwezi kuwa sheria ya CCM ama ya Chadema, lazima iwe sheria ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Ubaya wake uzungumzwe, uzuri wake uzungumzwe, manufaa kwa wananchi yazungumzwe bila hata kukopesha, tusifanye mchezo usiokuwa na akili nzuri."

Alisema "Utatungaje sheria ya Chadema, utatungaje sheria ya CCM, hakuna kitu kama hicho mimi naomba kama ile ninayosema networking (mtandao), ni muhimu, ila tuwe genuine (halisi), tuwe wakweli hii ni maslahi ya wananchi ama maslahi ya siasa tu? Haya mambo ya siasa tuna muda mwingi sana wa kufanya huko nje, wapi lakini hapa tutunge sheria zitakazowalinda Watanzania wa leo, wa kesho na wengine na historia itatukumbuka."
Aliwataka wabunge kutofautisha na kwamba wanapofikia katika suala la kitaifa ni lazima kutoa maoni kama wanataka kuwasaidia Watanzania.

Katu sitakuwa mtumwa wa Chama fulani cha siasa
ila fikra sahihi zenye kuleta tija na maendeleo ya kwali kwa taifa letu
 
Mimi nina swali wakuu. Je kuandamana Marekani kuhusu matatizo ya Tanzania kutasaidia kitu? Nauliza hivi kwa sababu nia na madhumuni ya maandamano ni kushinikiza. Sasa kama maandamano hayo hayata pewa air time ya kutosha kwenye vyombo vya habari vya Marekani na Tanzania tutakuwa tumepata faidia gani?

Nauliza haya kwa sababu si mara ya kwanza kusikia Watanzania waliopo Marekani wanataka kuandamana. Mwaka wa jana baada ya uchaguzi walisema wataandamana. Sasa sijui kama waliandamana na kama waliandamana basi hayo maandamano haya kutimiza lengo kwa sababu hamna mwananchi wa kawaida Tanzania aliye yasikia wala kuyaona.

We have limited resources. Let us direct them towards plan that actually work. Kama maandamano yanayo fanyika Tanzania na Chadema naona faida zake kwani zina shinikiza serikali kujiangalia. Sasa haya ya Marekani sioni any positive effect from them.
 
nimejihisi kutapika kwa ujinga ulio uandika hapa,
1. Wale ni watanzania ambao ni ndugu zetu na wanaumia kuona sisi ndugu zao tunaumia na kupata shida bila sababu ya msingi.

2. Hata wao wanaatthirika kiuchumi wao binafsi kwani lazima watumie sehem ya kipato chao kwa kuwatumia ndugu zao ambao wapo Tanzania kwaajili ya kugaramia elimu na matibabu,huduma ambayo wangepaswa kupewa bure na serikali.

3. Wanakila sababu ya kufanya hivyo kwani kwetu hapa Tanzania tumekosa fursa huru ya maandamano na kama kwa maandamano ya kumpinga meya tu wa arusha mjini(sio mbunge sio waziri) watu 3 waliuawa na makumi kujeruhiwa, je tukiandamana kumpinga rais watuua wangapi? (si maanishi hakuna cku halitatokea hili, ila waambie hao walio kutuma kuwa wanatengeneza taifa la watu wasio na cha kupoteza!)

We mwakilishi wa walanchi umepotosha kila jambo ulilojaribu kulijengea hoja, Hiv unadhan watanzania wote tuna weza kuwa wajinga kiasi hicho, Hiv unadhan hatujui sheria ya maandamano marekani inasemaje! Mbona unakurupuka kumpa mkeo vidonge vya majira wakati ni mjamzito? Bob alisema ''the time will tell'' . . . . . .

WanaJF tuachane na huyu mwenye fikra finyu na mawazo mgando na tuwaunge mkono hawa wakombozi wetu, hata kama hawaishi tanzania kwa sasa! Mbona aliyefanya mapinduzi ya Zanzibar hakuwa MZanzibari? Mbona che guevara hakuwa mcuba lakini alishiriki kufanya mapinduzi cuba na nchi nyingine nyingi duniani? Mi niwaombe mnao weza kwenda Marekani kuwaunga mkono wakombozi wetu hawa mfanye hivyo!
 
Kwasasa naona hali imefika pabaya zaidi kwani watu mumewekeza hata kufikiri, mumebinafsisha hata kufikiri hivi nani aliyesema kuandamana ni kosa, naye Jk kutalii amezidi mno sasa wamundamanie huko huko mpaka kieleweke, Wa Us fanya juu chini hilo jamaa la Magogoni lijue kuwa halikubaliki ndani na nje ya nchi,
 
Shy;2355852Ni matumaini yangu watu hao wanaojiita watanzania watabadilisha mawazo na muelekeo wao na kuacha kutumia jina la watanzania waishio marekani kwa malengo ya kuharibu jina la nchi na viongozi wake bila kujali itikadi ya vyama vyao said:
intellectuals have a special contribution to make to the development of our nation, and to Africa. And I am askin understanding that they should possess, should be used for the benefit of the society of which we are all members."[/B]Julius Kambarage Nyerere, from his book Uhuru na Maendeleo (Freedom and Development), 1973.

Mkuu, I like your point of view! However, you need to recollect your memories better than this if you are old enough to understand the politics of Tanzania.
  1. You should know that most of the learned tanzanian working abroad had been forced to do so by the TANU/CCM policies of non tolerance to alternative ideology.
  2. Some of them because you could not appreciate their contribution to the nation when they were here. Now they've left and made it there you pretend that they are Tanzanians! You took part in frustrating them by opting for incompetent individuals who were "mwenzetu". You denied them opportunity to promotion because of not being CCM members and NOT because they were opposing your policies!
  3. Up until now the CCM government is bent on oppressing intellectuals who patriotically chose to ignore your oppresion and remained here to work. You do not tolerate constructive criticsm from them! An example is still ringing in our ears when in April or May this year the government threatened University lecturers who "teach politics in the classrooms". YOU REALLY 'VE GOT SOME NERVES TO HAVE TO WRITE THIS THREAD! Shame on you. You forgot that users of this forum are not ignorant farmers you bribe every five years and they forget instantly.
  4. In 2009, the government decided to revoke powers of University Councils to employ Professors on contract and gave them to Utumishi which is directly under the President's Office. The famous Baregus and Mlambitis were axed from State Universities!!!! More are in the waiting list for the same action. Oooo dear, oo dear, ........ and a lot more ......
My friend, I also do not like demonstrations, and specifically if the country may stand to loose, however, if there is anyone to be ashamed here, it is the system that brought a docile people to the brink of starvation. I think JK rightly deserve it. He's been flying all over the world while his people suffers (Cf. David Cameron had to cut short his family holiday to attend to his people).

Again, Shame on you and the likes of you

Cheers
 


sasa hayo maneno niliyoweka bold ndiyo majibu !!! sio pale juu uliweka jazba mbele ....

Jaribu kusomelea elimu ya mahusiano na tabia ili ujue tofauti za watu na tabia zao. Kuna wale sanguiniki, flegmatiki, melankoliki nk, kwa maana hiyo binadamu hawafanani kitabia na katu hatutafanana kwa mantiki ya kuwasilisha ujume, we kwa akili na tabia yako soma kilichoandikwa na ujumbe unaotakiwa thats all, vinginevyo humu kila mtu ana namna yake ya kuwasilisha ujumbe na kama unaonja hivyo utapata ugonjwa wa moyo bure yakhe.

Na kumbuka kuna watu kwa akili zao na uzoefu pamoja na mbinu zao wa kiuandishi au kikazi wanaandika kwa kukusudia ili watu kama wewe tujue unavyopata kakasi.

:coffee:Take it easy man, you choose to be a member in JF to find all kind of people in this world.
:coffee:​
 
Mimi nina swali wakuu. Je kuandamana Marekani kuhusu matatizo ya Tanzania kutasaidia kitu? Nauliza hivi kwa sababu nia na madhumuni ya maandamano ni kushinikiza. Sasa kama maandamano hayo hayata pewa air time ya kutosha kwenye vyombo vya habari vya Marekani na Tanzania tutakuwa tumepata faidia gani?

Nauliza haya kwa sababu si mara ya kwanza kusikia Watanzania waliopo Marekani wanataka kuandamana. Mwaka wa jana baada ya uchaguzi walisema wataandamana. Sasa sijui kama waliandamana na kama waliandamana basi hayo maandamano haya kutimiza lengo kwa sababu hamna mwananchi wa kawaida Tanzania aliye yasikia wala kuyaona.

We have limited resources. Let us direct them towards plan that actually work. Kama maandamano yanayo fanyika Tanzania na Chadema naona faida zake kwani zina shinikiza serikali kujiangalia. Sasa haya ya Marekani sioni any positive effect from them.
bila shaka hufahamu umuhimu wa kuandamana hujui tofauti kati ya kutembea na kuandamana ndio maana unashangaa maandamano kufanyika US,suala hapa ni ujumbe umfikie hatujali wapi utamfikia,ajue watu hatumtaki na wala hatumpendi miaka minne iliyobaki kwa kweli ni JEHANAM ametutengenezea.
 
Mimi nina swali wakuu. Je kuandamana Marekani kuhusu matatizo ya Tanzania kutasaidia kitu? Nauliza hivi kwa sababu nia na madhumuni ya maandamano ni kushinikiza. Sasa kama maandamano hayo hayata pewa air time ya kutosha kwenye vyombo vya habari vya Marekani na Tanzania tutakuwa tumepata faidia gani?

Nauliza haya kwa sababu si mara ya kwanza kusikia Watanzania waliopo Marekani wanataka kuandamana. Mwaka wa jana baada ya uchaguzi walisema wataandamana. Sasa sijui kama waliandamana na kama waliandamana basi hayo maandamano haya kutimiza lengo kwa sababu hamna mwananchi wa kawaida Tanzania aliye yasikia wala kuyaona.

We have limited resources. Let us direct them towards plan that actually work. Kama maandamano yanayo fanyika Tanzania na Chadema naona faida zake kwani zina shinikiza serikali kujiangalia. Sasa haya ya Marekani sioni any positive effect from them.

Heshima mbele Mkuu

Hao ni Watanzania (JK anawahusu) wanaoishi Marekani, wana nduguzao, marafiki, jamaa nk hapo Tanzania, Hali halisi ya Siasa za Tanzania na mambo yanavyoenda wanazielewa na wanazifatilia kwa karibu kama wako nyumbani tu,
nachelea kusema Kwa Walio Tanzania wanaona hali ni kama ya kawaida , Kukosa Umeme, Maji, Mafuta, Ufisadi< rushwa nk kuwa ni sawa (Hakuna action ya maana iliyofanyika kupeleka msg mpaka sasa).

Lakini kwa mtu anayeishi kwenye nchi zenye kufuata sheria, usawa na haki za binadamu hali ya Tanzania sio ya kuvumilika hata kidogo, Hao Watanzania wana haki ya Kumwonyesha Rais ujumbe wao. Hayo maandamano sio kwa ajili ya CNN ni kwa ajili ya kupeleka ujumbe kwa Raisi kuwa nchi inayumba, nchi haiwezi kuendelea wala kuwa na Amani na umoja madhubuti kama kila mtu anafanya lake.
 
Heshima mbele Mkuu

Hao ni Watanzania (JK anawahusu) wanaoishi Marekani, wana nduguzao, marafiki, jamaa nk hapo Tanzania, Hali halisi ya Siasa za Tanzania na mambo yanavyoenda wanazielewa na wanazifatilia kwa karibu kama wako nyumbani tu,
nachelea kusema Kwa Walio Tanzania wanaona hali ni kama ya kawaida , Kukosa Umeme, Maji, Mafuta, Ufisadi< rushwa nk kuwa ni sawa (Hakuna action ya maana iliyofanyika kupeleka msg mpaka sasa),
Lakini kwa mtu anayeishi kwenye nchi zenye kufuata sheria, usawa na haki za binadamu hali ya Tanzania sio ya kuvumilika hata kidogo, Hao Watanzania wana haki ya Kumwonyesha Rais ujumbe wao,Hayo maandamano sio kwa ajili ya CNN ni kwa ajili ya kupeleka ujumbe kwa Raisi kuwa nchi inayumba, nchi haiwezi kuendelea wala kuwa na Amani na umoja madhubuti kama kila mtu anafanya lwake

Asante kwa jibu lako la staha na heshima mkuu

Mkuu mimi sipingani na hayo maandamano. Lakini nia na madhumini ya maandamano siyo tu ujumbe umfikie mhusika bali afeel pressure ya kubadilisha mwenendo wake. Ndiyo maana nikasema maandamano ya Chadema nyumbani naona mantiki yake kwa sababu tunaona matokeo yake. Hata hayo ya Marekani kama yataleta kweli shinikizo kwa serikali yetu naona ni jambo jema. Ila I doubt that will happen. Ndiyo maana nikapoint out yale maandamano yaliyo kuwa yafanyike Marekani kupinga matokeo ya uchaguzi. No body ever heard of them again.
 
bila shaka hufahamu umuhimu wa kuandamana hujui tofauti kati ya kutembea na kuandamana ndio maana unashangaa maandamano kufanyika US,suala hapa ni ujumbe umfikie hatujali wapi utamfikia,ajue watu hatumtaki na wala hatumpendi miaka minne iliyobaki kwa kweli ni JEHANAM ametutengenezea.

Mkuu unajibu kwa hisia siyo hoja kwa hiyo nitaenda na wewe taratibu. Punguza tu jazba kwanza.

Kwanza mimi nimesema maandamano. Huko kutembea umesema wewe na sijui hata imetoka wapi. Kwa hiyo tuachane na hilo kwanza.
Pili, ndiyo nia ya maandamano ni kufikisha ujumbe kwa mhusika lakini je ujumbe umefika? Kumbuka Marekani baada ya uchaguzi kulikua na maandamano ya kupinga matokeo ila nina uhakika hata wewe huwezi kunijibu hayo maandamano yalikwendaje. hata nikikuomba picha hutakua nazo because they went by simply unnoticed.

Maandamano siyo lazima yafanyike nchi husika. Kuna maandamano yamefanyike nje kupinga maswala ya nchi husika. Ila maandamano hayo kufanikiwa ni lazima yapate exposure ndiyo kutakuwa na pressure ya mhusika kubadilika. Laa sivyo kufanya hivyo kutakua kupiga gitaa kwa mbuzi. Na ndio maana nikatoa mifano ya maandamano ya Chadema ambayo ukiangalia unaona kabisa yana impact na yana lazimisha serikali kuact.

Sasa ni yapi usiyo taka kuelewa mkuu?
 
Back
Top Bottom