Kuhamia DP World au Kubaki TPA: Ushauri kwa wafanyakazi wa TPA

koryo1952

JF-Expert Member
Mar 7, 2023
390
776
Majuzi kumetokea tangazo kwa wafanyakazi wa TPA kuchagua kubaki TPA au kuhamia DP World. Hili ni jambo zuri lakini binafsi nina ushauri kwa wafanyakazi wa TPA. Kwanza uamuzi wa jambo hili lifanyike kwa umaakini mkubwa na ninashauri kama ifuatavyo:

(1) Kampuni yeyote inapofanya kazi nia kubwa ni kupata fada. Hilo halina mjadala na hivyo nia kubwa ya DP World ni kupata faida. Pindi DP World atakapoanza kazi atafanya maboresho makubwa katika shughuli zake kwa maana ya mashine za kisasa ili kurahisisha kazi na kazi iliyokuwa inafanyika mfano kwa watu 100 inaweza sasakufanyika na watu 10 na hivyo kupunguza watu 90. DP World watawaita wale watu 90 na kuwapunguza kazi. Nia yao ni faida kubwa.

(2) Wale watakaohamia DP World watawekewa sheria zisizo rafiki, sheria ambazo hawakuzizoea walipokuwa TPA na hivyo kuwafanya kujiondoa wenyewe.

(3) Kufanya kazi DP World hakutakuwa usalama wa kazi (Security) kama ilivyokuwa TPA hivyo wakati wowote mfanyakazi anaweza kufukuzwa bila kufuata utaratibu.

Pamoja na maelezo niliyoyatoa hapo juu pia nitatoa faida ya kuendelea kufanya kazi TPA.

(1) Kufanya kazi TPA kuna usalama mkubwa wa kazi. Una uhakika na mshahara wako japo unaweza kuwa ndogo lakini utaendelea nao mpaka utakapostaafu kazi.

(2) Pia kufanya TPA una uhakika wa malipo ya uzeeni yaani pensheni pindi utakapofika umri wa kustaafu.

(3) Inawezekana kuhamishwa mikoani kwenye bandari mbalimbali mfano Musoma, Mwanza, Kyela, Ukerewe, Bukoba, Mtwara, Tanga n.k. Hiyo isikutishe. Mikoani kuna fursa nyingi.

Kwa hitimisho nawashauri MSIHAMIE DP World na baadaye msije mkajuta ila kama DP World atamhitaji mtumishi mmoja mmoja basi mkae nao meza moja na kujadiliana nao kwa kufuata vipengele vyote vya kazi na baadaye mnaweza kukubaliana.
 
Kama mfanyakazi alikuwa ni mfanyakazi mwaminifu muadilifu na mchapakazi hana sababu ya kuiogopa DPW !
Ila kama ni kinyume chake ni lazima awe makini katika kufanya uchaguzi .

Maana huko Dipiwedi naamini itakuwa hakuna kubebana kwa kujuana.
 
Kwenda DP World ni kutake risk hilo inabidi wafanyakazi hao wafahamu.
Pili kinachotangulia ni kuchsgua kwenda Dp Workd au kubakia TPA hili ni kama kuuziwa mbuzi kwenye gunia. Ilipaswa kwanza kabla ya kuchagua pa kwenda kwanza wauone na kuusoma mkataba wa kazi wa DP World ili mtu aweze kupima kama anaweza terms zake ndipo sasa achague.

Utakapokuwa umechagua DP Workd kisha baadae ukipewa mkataba hata kana masharti yake sio rafiki utalazimika kusaini tu kwa sababu umeishatoka TPA .

Inaweza kuwa pia kuna probation period kwa atakayeenda huko.

MIkataba ya kazi itakuwa ya vipindi maalum na unaweza usiruhusiwe ku renew pale mkataba unapolazimika.

Mambo ya ruhusa ruhusa eti unaenda kuzika mara mama/mtoto anaumwa, kuchelewa kazini hiyo haipo huko.

DP world inawafaa wale wasio na ajira sio wafanyakazi wa serikali.
 
Taasisi za umma mazoea yamezidi hiyo job security inawapa kiburi nimefurahi sana sana kwa hili la dpw , waende sasa wakafanye kazi wamezoea kubebana mtoto wa mjomba na washangazi, nilitaka kulipia kodi ya gari kuna kijana kakaa na karatasi yangu pale tra fast mwezi mzima kutoa barua tu ya mimi kulipa kodi alikuwa anajizungusha kama mungu mtu, na hata ukienda kwa senior wake ni yale yale tu, taasisi za umma kidogo magufuli aliweza kuweka uwajibikaji sasahivi ni shamba la bibi
Na nashukuru kwamba serikali imeona kwamba tuongeze ufanisi tumpe mtu aendeshe ili watu wawajibike na serikali ipate mapato yake fullstop unayepinga hili unapinga kwa faida ya nani kama sio wizi na mazoea
Likewise mwendo kasi apewe muwekezaji aendeshe hakutakuwa tena na ujinga kama huu wa sasa
 
Hapa wapiga dili na waliokuwa wanabebwa watajulikana dpw hawezi kukaa na mzoga na kama taasisi zetu zingejengwa kwa misingi hii tungekuwa mbali sana , kwa hili la dpw naiunga mkono serikali 100% watu waache mazoea wafanye kazi
Naona unatema chuki. Watunishi wa umma sio walioosababisha ukose ajira. Huna ajira kwa sababu sio competent.

Subiri DP Wirkd watatangaza kazi mbalimbali apply uende ukachape kazi.
 
Kwenda DP World ni kutake risk hilo inabidi wafanyakazi hao wafahamu.
Pili kinachotangulia ni kuchsgua kwenda Dp Workd au kubakia TPA hili ni kama kuuziwa mbuzi kwenye gunia. Ilipaswa kwanza kabla ya kuchagua pa kwenda kwanza wauone na kuusoma mkataba wa kazi wa DP World ili mtu aweze kupima kama anaweza terms zake ndipo sasa achague.

Utakapokuwa umechagua DP Workd kisha baadae ukipewa mkataba hata kana masharti yake sio rafiki utalazimika kusaini tu kwa sababu umeishatoka TPA .

Inaweza kuwa pia kuna probation period kwa atakayeenda huko.

MIkataba ya kazi itakuwa ya vipindi maalum na unaweza usiruhusiwe ku renew pale mkataba unapolazimika.

Mambo ya ruhusa ruhusa eti unaenda kuzika mara mama/mtoto anaumwa, kuchelewa kazini hiyo haipo huko.

DP world inawafaa wale wasio na ajira sio wafanyakazi wa serikali.
Kufanya kazi kwa mazoea yale ya kishikaji hiyo itakuwa bye bye !
 
Naona unatema chuki. Watunishi wa umma sio walioosababisha ukose ajira. Huna ajira kwa sababu sio competent.

Subiri DP Wirkd watatangaza kazi mbalimbali apply uende ukachape kazi.
My friend usidhanie watu wote tunawaza ajira kama wewe tulishafanya kazi at senior levels na sasa tupo nje ya nchi tunafanya biashara zetu u have poverty mentality ndio maana unaona kila mtu anayekosoa anawaza ajira yako , ndio tatizo la elimu ya tanzania inadumaza watu , wote wanawaza wasome ili waajiriwe mwisho wa siku hicho kiajira kikikutoka siku mbili unaumwa unakufa get out of that comfort zonevili ukuwe
 
Ukiona MTU anaongelea security ya kazi ujue ni muoga WA maisha. Kuwa private hakuna maana kwamba huko waliopo ni mbumbumbu wasiojua wala kufuata sheria za kazi. Kuna baadhi ya taasisi za private wanajali wafanyakazi kuliko huko serikalini. Serikalini pia huwa wanapunguza wafanyakazi kutokana na sababu mbalimbali kwahiyo siyo DPW Tu ndo wanaweza punguza watu kazi. Kubaki TPA kuna risk ya kuhamishiwa mtambaswala ambapo pengine hukuwa na plan napo. DPW Kwa kuwa ni kampuni mpya hapa bongo watakao hamia watakuwa na fursa nyingi za kukuwa na kujifunza.
 
Taasisi za umma mazoea yamezidi hiyo job security inawapa kiburi nimefurahi sana sana kwa hili la dpw , waende sasa wakafanye kazi wamezoea kubebana mtoto wa mjomba na washangazi, nilitaka kulipia kodi ya gari kuna kijana kakaa na karatasi yangu pale tra fast mwezi mzima kutoa barua tu ya mimi kulipa kodi alikuwa anajizungusha kama mungu mtu, na hata ukienda kwa senior wake ni yale yale tu, taasisi za umma kidogo magufuli aliweza kuweka uwajibikaji sasahivi ni shamba la bibi
Na nashukuru kwamba serikali imeona kwamba tuongeze ufanisi tumpe mtu aendeshe ili watu wawajibike na serikali ipate mapato yake fullstop unayepinga hili unapinga kwa faida ya nani kama sio wizi na mazoea
Likewise mwendo kasi apewe muwekezaji aendeshe hakutakuwa tena na ujinga kama huu wa sasa
Na Tanesco wapewe watu binafsi naamini tutakuwa vizuri
 
Majuzi kumetokea tangazo kwa wafanyakazi wa TPA kuchagua kubaki TPA au kuhamia DP World. Hili ni jambo zuri lakini binafsi nina ushauri kwa wafanyakazi wa TPA. Kwanza uamuzi wa jambo hili lifanyike kwa umaakini mkubwa na ninashauri kama ifuatavyo:-
(1) Kampuni yeyote inapofanya kazi nia kubwa ni kupata fada. Hilo halina mjadala na hivyo nia kubwa ya DP World ni kupata faida. Pindi DP World atakapoanza kazi atafanya maboresho makubwa katika shughuli zake kwa maana ya mashine za kisasa ili kurahisisha kazi na kazi iliyokuwa inafanyika mfano kwa watu 100 inaweza sasakufanyika na watu 10 na hivyo kupunguza watu 90. DP World watawaita wale watu 90 na kuwapunguza kazi. Nia yao ni faida kubwa.
(2) Wale watakaohamia DP World watawekewa sheria zisizo rafiki, sheria ambazo hawakuzizoea walipokuwa TPA na hivyo kuwafanya kujiondoa wenyewe.
(3) Kufanya kazi DP World hakutakuwa usalama wa kazi (Security) kama ilivyokuwa TPA hivyo wakati wowote mfanyakazi anaweza kufukuzwa bila kufuata utaratibu.
Pamoja na maelezo niliyoyatoa hapo juu pia nitatoa faida ya kuendelea kufanya kazi TPA.
(1) Kufanya kazi TPA kuna usalama mkubwa wa kazi. Una uhakika na mshahara wako japo unaweza kuwa ndogo lakini utaendelea nao mpaka utakapostaafu kazi.
(2) Pia kufanya TPA una uhakika wa malipo ya uzeeni yaani pensheni pindi utakapofika umri wa kustaafu.
(3) Inawezekana kuhamishwa mikoani kwenye bandari mbalimbali mfano Musoma, Mwanza, Kyela, Ukerewe, Bukoba, Mtwara, Tanga n.k. Hiyo isikutishe. Mikoani kuna fursa nyingi.
Kwa hitimisho nawashauri MSIHAMIE DP World na baadaye msije mkajuta ila kama DP World atamhitaji mtumishi mmoja mmoja basi mkae nao meza moja na kujadiliana nao kwa kufuata vipengele vyote vya kazi na baadaye mnaweza kukubaliana.
Naona waongelea haki za wafanyakazi kulindwa na vingine muhimu kwa wafanyakazi.

Mimi nilipokuwa nikifanya kazi huko ughaibuni kabla sijarejea bongo, nimepitiwa sana na hili wanolifanya DP World.

Huu waitwa TUPE transfer yaani Transfer of Undertakings ya biashara au kampuni na yale yote yaliyomo kuzingatia sheria za kazi yaani Protection of Employment.

Sasa sheria ya kazi na ajira ya Tanzania yasemaje kwenye mambo kama hili la TUPE yaani employment regulation act? Hilo ndilo la kuliangalia.

Lakini kwa kifupi mwajiri mpya huja na masharti mapya ya kazi, hubadili utendaji wa kazi na hulipa mishahara kutokana na ufanisi wa kazi na hufuata kitu chaitwa KPI .KPI mbovu huweza kusababisha kupoteza kazi.

Tukumbuke DP World ni kampuni ya kimataifa hivyo ni kweli wafanyakazi wasome uzuri yaliyomo kwenye mikataba lakini pia wajiandae na utaratibu mpya kabisa ambao hawajauzoea au wajiondoe kutafuta kazi nyingine, huo ndo ukweli.
 
Wabaki tu kama mtu hajiamini au alikuwa anakula kwa urefu wa kamba basi abaki tu hapo
Huko watakuta camera kila kona na masharti kibao hata kama ulikuwa sio mwizi bali umezoea ilifika saa 5 tu unaenda zako kutafuta mlo masaa manne ukirudi unaenda home
Huko unakutana na clock card utakula ulichopanda au unaweza hata kufukuzwa
Kubadili tabia ni ngumu kwa wengi kwa hiyo kuna hatari ya kufukukwa kwa uzembe au wizi
 
Back
Top Bottom