Kuepuka yale ya Ruge, Kusaga na Makonda, sheria zetu za mikataba ya biashara zinaruhusu kipengele hiki?

Keynez

JF-Expert Member
Feb 12, 2007
2,397
3,884
Mengi yanasemwa kuhusiana na Clouds Media na uanzishwaji wa Wasafi Media. Mada yangu haitajikita huko, nimeutoa huo kama mfano tu, tuchukulie tu ule kama mfano wa jambo ambalo lipo sana tu katika mifumo yetu ya biashara.

Mada yangu inaongelea pale watu wawili au zaidi wanapoingia makubaliano ya kuanzisha biashara ya pamoja, partnership au limited company, lakini baada ya muda, kwa sababu moja ama nyingine, mmoja au baadhi wanawazunguka wenzao na kwenda kuanzisha biashara ya aina hiyo hiyo au inayofanana na hiyo bila kuwashirikisha (m)wenzao.

Katika nchi zilizoendelea, huwa partners au shareholders wanawekeana kitu kinachoitwa exclusive agreement. Yaani partner kwenye huo mkataba, haruhusiwi kwenda kuanzisha au kujiunga kama partner katika biashara yoyote ya aina hiyo au yoyote ile inayoleta ushindani wa moja kwa moja na biashara wanayoanzisha. Nadhani hata pale partner/shareholder anapojiondoa katika makubaliano hayo, bado anakuwa anafungwa na vifungu hivyo kwa miaka fulani.

Kipengele hiki kinaondoa udanganyifu na uwezekano wa partners kuzungukana.

Je, kwa sheria zetu za mikataba, kipengele kama hiki kinawezekana na kinatambulika?
 
Hizo sheria zipo, nadhani ziko kwenye Conflict of Interests.

Ila wanaweza kuanzisha kupitia ndugu au jamaa wa karibu.

Sidhani kama sheria inawazuia, labda kama nao wako kwenye payroll.

Hata Wasafi FM iko kwa mfumo huo.
 
Don Clericuzio,
Kuanzisha kupitia ndugu inawezekana ila inaleta complications nyingi. Kwa muda gani muhusika ataweza kujificha bila kuonekana ndiye mmiliki rasmi? Ni jambo ambalo kinadharia linawezekana ila kivitendo ni kama haliwezekani.

Unajua sheria zinaweka muda gani baada ya partner/shareholder kuondoka/kujitenga au inategemea na makubaliano yenu wenyewe?
 
Keynez hilo haliwezekani kwa África ni sawa na kusema mtu akijivua gamba asijiunge CDM hiyo never


Sent using IPhone X

Ni jambo gumu kuweza kulisimamia ila biashara inapokuwa ni kubwa na yenye maslahi makubwa, kinakuwa na umuhimu wa pekee. Cha muhimu ni kujua kwanza kama sheria zetu za mikataba zinatambua kipengele kama hicho.
 
Ni jambo gumu kuweza kulisimamia ila biashara inapokuwa ni kubwa na yenye maslahi makubwa, kinakuwa na umuhimu wa pekee. Cha muhimu ni kujua kwanza kama sheria zetu za mikataba zinatambua kipengele kama hicho.

Ukiondoa madawa ya kulevya siasa za África ni biashara kubwa sana mkuu believe me


Sent using IPhone X
 
Back
Top Bottom