Kuendesha nyumba kwa remote control

Wanachit-chat nawasalimu.
kuna hili jambo huwa linanitokea sana.
Utakuta nimesafiri, sipo nyumbani kwa siku, wiki, miezi kadhaa, lakini huwa nina tabia ya kuendesha maisha ya nyumbani kana kwamba sijaacha mtu. kila siku lazima nipige simu kuulizia/kutoa maelekezo (mmepika nini?, watoto wamekula?, jioni mtawapa nini?, kesho toa net uzifue......). sasa najiuliza hii ina maana gani? ni mimi tu au hata wamama wenzangu mnafanya hivi?
wababa wanalipokeaje? wanashukuru kuwa tunawasaidia kuendesha nyumba hata kama hatupo nyumbani au wanaona hatuwaamini?
Fixed Point, yaani bila kufanya hivyo kwa wiki tu ni balaa haswa kama unakaa mbali, especialy ukiwa na watoto, yaani lazma kupiga simu ikifika jioni, dada watoto wamevaa masweta?, chakula cha baba kwenye ma-hotpot haraka, mtoto mkubwa apewe dawa za jioni! chumba cha twins kipulizwe dawa, hapohapo utanisikia dada kesho nje kulimiwe watoto wakilala mchana nikirudi nisikute majani, na mabuibui yatolewe! yaani ofisini kwetu huwa wanacheka nikisafiri nao! hata kama ni wapi! mwenzio nishawahi kuwa mkoa kwa wiki 3, na bado nyumba iliwekwa tiles nikiwa hukohuko, yaani naongea na muuza tiles dukani apeleke hm, malipo kwa m-pesa! naongea na fundi akaweke hizo tiles, malipo kwa m-pesa, na dada naye awafungie watoto rum kwangu ili wasipate vumbi la cement! mpaka nyumba iliisha! so my dear you are not alone hata kidogo! am one of them!
 
Last edited by a moderator:
yap...napendaga apige sana tu...naona anajali...ILA sio kuwa awe fixed...aamini kuwa aliowaacha pia wanaweza kuwa na uamuzi mzuri wakati mwingine...mathalani ishu ya chakula!
 
Dena Amsi kumbe haya mambo yapo kila nyumba! mara nyingi watoto afya zina-shake sana mama akisafiri, wadada wengi hawajali milo ya watoto, na ukizingatia watoto wetu wa siku hizi kula mpaka umuimbie, nani atafanya kazi hiyo mara 5 kwa siku!
Fixed Point mi namshukuru MUNGU mdada aliyenilelea twins wangu alikuja wana miezi mi5, mpaka leo miaka 4 na nusu yupo na hana mpango wa kuondoka leo wala kesho, ila nampa 80 thou kwa mwezi nadhani mshahara nao unahamasisha anakaa, yaani kila nikiongezewa mshahara january, na ye namboost kwa elf kumi, labda na kitenge na kanga ya ahsante umenilelea wanangu vizuri. sasa twins wangu toka kipindi hichoooooooo utaimba nyimbo zote hafungui mdomo, wadada walikuwa wasepaje?? alivyokuja huyu nikapata wazo la kuwalisha kwenye maji, yaani najaza maji yale ma pool ya plastic pale moroco nawadumbukiza kwenye maji na michezo ya kila aina mpaka vinguo vyao vya kufua, so within tn minutes huwa kama ni uji umekwisha, kama ni ndizi nazo zimekwisha, yaani hawatupi taabu kwenye kula vitu vya liquids, ila ugali, wali na vingine vigumu tunakula nao mezani kama kawaida!
 
Last edited by a moderator:
Fixed Point, yaani bila kufanya hivyo kwa wiki tu ni balaa haswa kama unakaa mbali, especialy ukiwa na watoto, yaani lazma kupiga simu ikifika jioni, dada watoto wamevaa masweta?, chakula cha baba kwenye ma-hotpot haraka, mtoto mkubwa apewe dawa za jioni! chumba cha twins kipulizwe dawa, hapohapo utanisikia dada kesho nje kulimiwe watoto wakilala mchana nikirudi nisikute majani, na mabuibui yatolewe! yaani ofisini kwetu huwa wanacheka nikisafiri nao! hata kama ni wapi! mwenzio nishawahi kuwa mkoa kwa wiki 3, na bado nyumba iliwekwa tiles nikiwa hukohuko, yaani naongea na muuza tiles dukani apeleke hm, malipo kwa m-pesa! naongea na fundi akaweke hizo tiles, malipo kwa m-pesa, na dada naye awafungie watoto rum kwangu ili wasipate vumbi la cement! mpaka nyumba iliisha! so my dear you are not alone hata kidogo! am one of them!
Ni kweli kabisa cacico. sasa hao wadada wenyewe wafanye basi yale tunayoagiza kwa simu. kuna siku sikusema ntarudi lini tuka safari, na Mr naye nikamwambia asiwaambie. kila siku wanamwuliza baba mama atarudi lini anawaambia bado, na mimi kila siku kama kawaida simu haziishi. simu ya mwisho ya maelekezo niliipiga nusu saa kabla sijafika home. kuingia nyumbani, yooooooooooote niliyoyaagiza juzi, jana, leo, hakuna lililofanywa. kumaliziana hela ya simu tu!
 
Last edited by a moderator:
yap...napendaga apige sana tu...naona anajali...ILA sio kuwa awe fixed...aamini kuwa aliowaacha pia wanaweza kuwa na uamuzi mzuri wakati mwingine...mathalani ishu ya chakula!
sawa BAGAH, ndo nyie nyumbani mama akiondoka kila siku kunakaangwa chipsi kuku............ hakuna cha makande wala wali maharage
 
Last edited by a moderator:
  • Thanks
Reactions: BAK
Fixed Point mi namshukuru MUNGU mdada aliyenilelea twins wangu alikuja wana miezi mi5, mpaka leo miaka 4 na nusu yupo na hana mpango wa kuondoka leo wala kesho, ila nampa 80 thou kwa mwezi nadhani mshahara nao unahamasisha anakaa, yaani kila nikiongezewa mshahara january, na ye namboost kwa elf kumi, labda na kitenge na kanga ya ahsante umenilelea wanangu vizuri. sasa twins wangu toka kipindi hichoooooooo utaimba nyimbo zote hafungui mdomo, wadada walikuwa wasepaje?? alivyokuja huyu nikapata wazo la kuwalisha kwenye maji, yaani najaza maji yale ma pool ya plastic pale moroco nawadumbukiza kwenye maji na michezo ya kila aina mpaka vinguo vyao vya kufua, so within tn minutes huwa kama ni uji umekwisha, kama ni ndizi nazo zimekwisha, yaani hawatupi taabu kwenye kula vitu vya liquids, ila ugali, wali na vingine vigumu tunakula nao mezani kama kawaida!
huyo dada shikamana naye. katika vitu nasisitiza nyumbani kwani ni kuhakikisha watoto wamekula vizuri, lakini ndo jambo linaenda vibaya kuliko yote, maana nina ma-miss nyumbani kwangu hawapendi kula, kupikia watoto pia hawataki
 
Ni kweli kabisa cacico. sasa hao wadada wenyewe wafanye basi yale tunayoagiza kwa simu. kuna siku sikusema ntarudi lini tuka safari, na Mr naye nikamwambia asiwaambie. kila siku wanamwuliza baba mama atarudi lini anawaambia bado, na mimi kila siku kama kawaida simu haziishi. simu ya mwisho ya maelekezo niliipiga nusu saa kabla sijafika home. kuingia nyumbani, yooooooooooote niliyoyaagiza juzi, jana, leo, hakuna lililofanywa. kumaliziana hela ya simu tu!
Fixed Point uwiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii wanakeraje ikifika hapo?? kuwa unaagiza kitu halafu hakitekelezwi?? huwa napata kichaa wallah! nways huwa sina utani when it comes to my husband na watoto, kwamfano tu, labda nguo za baba hazitakati kola, tutagombana sana wanajua hilo! huwa always nina wadada wawili, wa watoto tu, na wa kazi nyingine za nyumbani. au vitu vya watoto haviendi kama nilivyopanga, ratiba ya kula ifuatwe, kufanya homework wanafanya na dad wao, siku zote coz anarudi mapema kuliko mimi, so wanatakiwa waoge na kula kabla dad hajarudi so that wafanye h/w ikitokea tu ratiba imebadilika dada wa watoto atawajibika, yaani huwa tunacheka, ila nikikasirika pia wanajua kabisa kuwa hapa kimenuka!
 
Fixed Point uwiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii wanakeraje ikifika hapo?? kuwa unaagiza kitu halafu hakitekelezwi?? huwa napata kichaa wallah! nways huwa sina utani when it comes to my husband na watoto, kwamfano tu, labda nguo za baba hazitakati kola, tutagombana sana wanajua hilo! huwa always nina wadada wawili, wa watoto tu, na wa kazi nyingine za nyumbani. au vitu vya watoto haviendi kama nilivyopanga, ratiba ya kula ifuatwe, kufanya homework wanafanya na dad wao, siku zote coz anarudi mapema kuliko mimi, so wanatakiwa waoge na kula kabla dad hajarudi so that wafanye h/w ikitokea tu ratiba imebadilika dada wa watoto atawajibika, yaani huwa tunacheka, ila nikikasirika pia wanajua kabisa kuwa hapa kimenuka!
ndo maana wadada wanafurahi mama akisafiri maana wanajua wanakuwa free sana. sasa mimi nina tabia ya kushtukiza kurudi home mchana, hii huwa nafanya randomly, yaani unakuta asubuhi yooooote hakuna kazi iliyofanyika, ni mwendo wa kushinda kwenye TV. kazi zinaaza kufanywa jioni mnapokaribia kurudi, muda huo wadada wanakuwa busy sana mpaka utamhurumia.
 
Hapana ni kutambua na kujitambua..kutambua wajibu, na kuutekeleza kwa mapenzi bila kuona kuwa ni mzigo.
asante sana kwa complement. pale kwangu huwa mtu ananishukuru sana akikuta kitu kimefanywa halafu aambiwe "mama alituambie tufanye" sikujua kama anaona kuwa natambua wajibu wangu na kuutekeleza kwa mapenzi
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom