Kuendelea kutegemea wakulima wadogo wenye jembe la mkono, mfumuko wa bei ya vyakula hautashuka kamwe CCM imeshindwa kubadili kilimo chetu kwa miaka 61

Sir robby

JF-Expert Member
Jun 22, 2022
2,400
4,074
Tanzania chini ya CCM imeshindwa kabisa kukibadilisha kilimo cha wananchi wake. Nakiri kusema toka imepata uhuru wake mwaka 1961 imekuwa na wakulima wadogo wadogo wanaolima kwa kutumia jembe la mkono na mbolea ya kubahatisha miaka yote mpaka leo 2023.

Kilimo hicho ni kigumu sana kwani kinategemea mvua ambazo hazina uhakika. Mavuno ya kilimo hicho ni duni sana kiasi ambacho nguvu kubwa inatumika lakini mavuno hafifu na ndio maana watu wengi wanakimbia kilimo.

Tanzania kama tunataka tuondokane na bei ya vyakula kupanda ni lazima tubadili kilimo chetu tunatakiwa tufanye uwekezaji mkubwa kwenye kilimo. Kilimo kiwe cha kibiashara na cha zana za kisasa kama vile matrekta n.K. Badala ya majembe ya mikono.

Bila kufanya hivyo tutakuwa tunadanganyana tunaimba wimbo na kwa sasa kilimo chetu siyo tena uti wa mgongo tena.
 
Tanzania chini ya CCM imeshindwa kabisa kukibadilisha kilimo cha wananchi wake. Nakiri kusema toka imepata uhuru wake mwaka 1961 imekuwa na wakulima wadogo wadogo wanaolima kwa kutumia jembe la mkono na mbolea ya kubahatisha miaka yote mpaka leo 2023.

Kilimo hicho ni kigumu sana kwani kinategemea mvua ambazo hazina uhakika. Mavuno ya kilimo hicho ni duni sana kiasi ambacho nguvu kubwa inatumika lakini mavuno hafifu na ndio maana watu wengi wanakimbia kilimo.

Tanzania kama tunataka tuondokane na bei ya vyakula kupanda ni lazima tubadili kilimo chetu tunatakiwa tufanye uwekezaji mkubwa kwenye kilimo. Kilimo kiwe cha kibiashara na cha zana za kisasa kama vile matrekta n.K. Badala ya majembe ya mikono.

Bila kufanya hivyo tutakuwa tunadanganyana tunaimba wimbo na kwa sasa kilimo chetu siyo tena uti wa mgongo tena.
Sitaki kupingana nawe, kwa sababu hujaeleza kifasaha jambo unalolizungumzia.

Ninakubalina nawe juu ya zana za kilimo zinazotumika sasa hivi, na pia kutokuwepo na pembejeo stahiki kwa mkulima, na hiyo ya utegemezi wa mvua...., yote hayo ninakubaliana kabisa na wewe.

Sasa mahali ambapo pengine tutapishana ni hapo tu pa "wakulima wadogo", maana hujafafanua maana yake ni ipi hasa!


Kama maana yako ni kuwa wakulima wadogo hawafai/ waondoke kupisha wakulima wenye mashamba makubwa pekee, hilo sikubaliani nawe hata kidogo.

Unaweza kuzalisha kwa ufanisi hata katika hayo mashamba madogo madogo. Najua utakuja na hoja za 'advantage of scale", lakini hoja hiyo ni hoja mfu, kwani ukiwaunganisha wakulima wadogo 50, 'scale' iko pale pale.

Utawapeleka wapi wakulima wetu wadogowadogo.
 
Sitaki kupingana nawe, kwa sababu hujaeleza kifasaha jambo unalolizungumzia.

Ninakubalina nawe juu ya zana za kilimo zinazotumika sasa hivi, na pia kutokuwepo na pembejeo stahiki kwa mkulima, na hiyo ya utegemezi wa mvua...., yote hayo ninakubaliana kabisa na wewe.

Sasa mahali ambapo pengine tutapishana ni hapo tu pa "wakulima wadogo", maana hujafafanua maana yake ni ipi hasa!


Kama maana yako ni kuwa wakulima wadogo hawafai/ waondoke kupisha wakulima wenye mashamba makubwa pekee, hilo sikubaliani nawe hata kidogo.

Unaweza kuzalisha kwa ufanisi hata katika hayo mashamba madogo madogo. Najua utakuja na hoja za 'advantage of scale", lakini hoja hiyo ni hoja mfu, kwani ukiwaunganisha wakulima wadogo 50, 'scale' iko pale pale.

Utawapeleka wapi wakulima wetu wadogowadogo.
Wakulima wadogo ni mkulima anayetumia jembe la mkono tena Mzee maana Vijana wote wapo Mijini
 
Muhtasari toka tovuti ya wizara ya kilimo

"Nchini Tanzania, Sekta ya Kilimo ni muhimili wa maendeleo ya uchumi. Sekta hii inachangia kiasi cha nusu ya pato la Taifa, robo tatu ya bidhaa zinazouzwa nje ya nchi na chanzo cha chakula pamoja na utoaji wa fursa za ajira zaidi ya 75% ya Watanzania. "
 
Muhtasari toka tovuti ya wizara ya kilimo

"Nchini Tanzania, Sekta ya Kilimo ni muhimili wa maendeleo ya uchumi. Sekta hii inachangia kiasi cha nusu ya pato la Taifa, robo tatu ya bidhaa zinazouzwa nje ya nchi na chanzo cha chakula pamoja na utoaji wa fursa za ajira zaidi ya 75% ya Watanzania. "
Kaangalie huo muhtsari uliandikwa lini! Na jinsi serikali inavyodelay kuupdate taarifa mh!
 
Kwani takwimu kama hizi zinakua valid kwa muda gani kwanza?
Huo Ni muhstasari yamkini uliandikwa tangu kilimo Ni uti wa mgongo, siasa Ni kilimo mpaka kilimo kwanza na pawatila za Mizengo Pinda. Wanachokifanya Ni kucopy na kupaste kwani wanajua watanzania sio wafuatiliaji wazuri wa takwimu!
Na kwa kulisiliba Hilo wakaja na ile Sheria ya takwimu kwamba NBS Pekee ndio anatoa takwimu hata ukifanya utafiti wako mwenyewe bado Ni invalid.

Kwahiyo kuhusu muda wa kudumu kwa takwimu hizo hata milele inawezekana.

Ni juzi tu tumefanya sensa ya watu na makazi na taarifa hazijawekwa waaazi Sana isipokua lisherehe kikubwa la kuzindua idadi ya watu hatujui uwiano wa idadi ya watu na shughuli za kiuchumi!

Awamu ya tano haikuajiri kwa takribani miaka sita mfululizo, vijana hao ambao wanacompose the largest proportion of the population hatuoni wakiingia kwenye kilimo ispokua motivesheni spikaz, Boda Boda biashara mtandao na uchawa ili kuvizia uteuzi!

Vijana wengi mjini na vijijini wamejikimbiza kwenye kazi rahisi na sio kilimo, kwaninkilimo hakijawa enhanced kwa maana ya kuwa na zana Bora za kilimo pamoja na Sera nzuri za umiliki wa ardhi pamoja na kuihusianisha secta ya kilimo, viwanda na biashara.

Ukitaka kuthibitisha hili hebu fuatilia kwenye habari picha kuhusu ugawaji wa mbolea ya Ruzuku wanaopanga foleni Ni wazee na akina mama na sio vijana!
Adios
 
Wakulima wadogo ni mkulima anayetumia jembe la mkono tena Mzee maana Vijana wote wapo Mijini
Kwa maana yako hiyo: mkulima anayelima kwa kutumia plau inayokokotwa na ng'ombe, akilima eka zake tano, huyo humhesabu kuwa ni mkulima mdogo?

Maana yako ya "mkulima mdogo" ni finyu sana.
 
Simple tu! Sectorial linkage and political will!
Dah!

Mkuu, hii 'jargon' umeiokota hivi karibuni?

Naona bado inakuchemsha damu kwelikweli!

Naomba niulize tu mkuu, kwa nia njema kabisa. Unao uhusiano wowote na Mheshimiwa sana, mchumi namba moja Mwigulu Nchemba?
Usione ajabu kwangu kuuliza hili swali, kwa sababu naelewa tabia za watu huanzia kwenye mfanano wa 'genes'. Zenu, yaani Mwigulu na zako zinashabihiana kwa karibu sana, kutokana na haya uliyobandika hapo juu kama jibu lako kwa swali nililouliza.
 
Dah!

Mkuu, hii 'jargon' umeiokota hivi karibuni?

Naona bado inakuchemsha damu kwelikweli!

Naomba niulize tu mkuu, kwa nia njema kabisa. Unao uhusiano wowote na Mheshimiwa sana, mchumi namba moja Mwigulu Nchemba?
Usione ajabu kwangu kuuliza hili swali, kwa sababu naelewa tabia za watu huanzia kwenye mfanano wa 'genes'. Zenu, yaani Mwigulu na zako zinashabihiana kwa karibu sana, kutokana na haya uliyobandika hapo juu kama jibu lako kwa swali nililouliza.
Mkuu naomba unitake radhi kabisa Tena kabisa Sina uhusiano nae kwa namna yoyote iwe kisiasa, kikabila au hata kidini hakuna kitu tunashare in common.

Hiyo kitu nikiyoandika sio jargon Ni lugha rahisi tu!

Yes nimemjibu muuliza swali kwamba Ni rahisi na Mambo yanawezekana ikiwa tu kutakua na

Muunganiko wa kisecta kwenye Mambo ambayo Ni commonu mathalani
Sekta ya kilimo-viwanda-biashara.

Lakini katika hayo waliopewa dhamana wawe na utashinwa kisiasa (political will) ya kuyasimamia na kuyatekeleza hayo!
Kitu ambacho viongozi wetu hawana kwa Sasa ikiwemo Huyo Trab na Trat ambae ameshauri wabubunge kujadili Mambo ya waganga wa kienyeji na sio maswalia ya uchumi!

Umenielewa?
 
Mkuu naomba unitake radhi kabisa Tena kabisa Sina uhusiano nae kwa namna yoyote iwe kisiasa, kikabila au hata kidini hakuna kitu tunashare in common.

Hiyo kitu nikiyoandika sio jargon Ni lugha rahisi tu!

Yes nimemjibu muuliza swali kwamba Ni rahisi na Mambo yanawezekana ikiwa tu kutakua na

Muunganiko wa kisecta kwenye Mambo ambayo Ni commonu mathalani
Sekta ya kilimo-viwanda-biashara.

Lakini katika hayo waliopewa dhamana wawe na utashinwa kisiasa (political will) ya kuyasimamia na kuyatekeleza hayo!
Kitu ambacho viongozi wetu hawana kwa Sasa ikiwemo Huyo Trab na Trat ambae ameshauri wabubunge kujadili Mambo ya waganga wa kienyeji na sio maswalia ya uchumi!

Umenielewa?
Uliyemjibu swali ni mimi, usisahau hilo.

Hiyo niliyoiita 'jargon' ni kwa maksudi tu kama 'derogatory', wala usidhani sikujuwa ulichomaanisha.

Hata hivyo, naona maana iliyokusudiwa katika jibu langu hukuipata sawia, lakini hilo si neno.

Nashukuru kwamba wewe na Mwigulu hamna uhusiano kama ulivyoelezea hapo; lakini naona mko kwenye fani moja.

Kwa hiyo pengine mfanano huu mnauokota huko huko darasani kwenu mnakopitia.
 
Back
Top Bottom