Tindo
JF-Expert Member
- Sep 28, 2011
- 59,045
- 103,460
Big up mkuu umeongea kwa hisia kuu.
Watu wanachezea sana nchi hii.
CCM waliichezea kwa sababu ya Ukongwe na wakati huo.
Pia CCM imewachezea watanzania lwa sababu ya nguvu ya Dola inayoliongoza.
Sasa kuruhusu tena nchi hii kuwa na chama Kingine mbadala kibovu kuliko CCM ni jambo lisilokubalika potote.
Mbowe sio tuu anapaswa kupingwa Bali kupigwa vita vya aina zote na kufurushwa nje ya ukumbi kwa kuzomewa na kukataliwa kabisa.
Kama Wajumbe wote wa mkutano mkuu Chadema wataruhusu dikteta kuongoza Chama basi ni dhahiri kuwa wamebariki Nchi yetu kuachana na Demokrasia.
Mwaka 2015 Chadema Chini ya Mbowe imetutoa kwenye agenda ya Ifisada kibabe na kwa ubabe wa Mbowe asiyeshaurika.
Sasa Mwaka huu tena ubabe wa Mbowe na genge lake wanataka kututoa kwenye agenda ya kupigania Demokrasia kibabe tena. Mbowe akirudi tena kama Mwenyekiti wa Chama tutawaambia nini Watanzania kuhusu kupigania Demokrasia na kupinga Udikteta .
Patakua na umuhimu gani wa kufanya Chaguzi za Kidemokrasia na kuweka ukomo wa Uongozi?
Kumbe basi ukomo utakua hauna maana kama anayetawala au kuongoza atakua ni kiboko wa jambo fulani. Yani tusema JPM ni kiboko wa Mafisadi na kiboko ya wapinzani wa CCM basi atawale mpaka atakapoamua kuondoka mwenyewe.
Demokrasia itakua haina maana kama kiongozi anaamua mwenyewe muda wa kukaa madarakani kupitia mgongo wa Demokrasia inayosimamiwa na wale aliowateua.
Hivi Mbowe haoni kuwa hana tofauti na Rais aliyeko madarakani anayeteua tume ya uchaguzi halafu anagombea bila ukomo?
Mbowe hajui kuwa Tanzania kama Rais asingekua na ukomo asingekuja kushindwa kwenye uchaguzi.
Busara ya Ukomo kwenye Uongozi iliwekwa na Baba wa Taifa baada ya kuona madhara yake katika kupigania Demokrasia. Hii ni ndani na nje ya Chama na Vyama vyote.
Mbowe mwenye anajua kabisa kuwa Kwa sheria na katiba ya nchi yetu Chama kinachotawala kina nguvu kubwa sana kuliko viongozi wa Serikali.
Sasa Mbowe asipoheshimu Demokrasia ya Chama tujue wazi kabisa kuwa endapo Chadema itashinda tutakua na mihimili Minne ya nchi inayoongozwa na wakuu wake wananne. Yani Bunge, Chama , Serikali na mahakama. Chama kisichokua na Demokrasia hakitakua na maelekezo ya kidemokrsia kwa serikali yake hasa kutokana na kuwa na Mwenyekiti ambaye ni tofauti na Rais. Matokeo yake ataliingiza Taifa katika mgogoro mkubwa baina vya Mwenyekiti wa Chama Dikteta na Amiri Jeshi Mkuu mwenye Demokrasia.
Kama Chadema watashupaza Shingo zao na kuona kuwa wanamkomoa JPM na kumchagua Mbowe basi tujue tunatengeneza siasa za kitoto kabisa ndani ya Chadema.
Ingekua Mwenyekiti anapokaa muda mrefu kwenye Uongozi wa chama ndio kukua na kukijenga Chama basi UDP na Cheyo kingekua ndicho chama Tawala.
Wangalau leo umeongea jambo linalokubalika na hoja zisizo na propaganda za kijinga. Naunga mkono hoja yako kwa 100%.