Hawa ndio Viongozi waliowaokoa Kubenea na Komu ndani ya CHADEMA. Walikabiliana na kundi la Mbowe lililotaka wafukuzwe

Daimler

JF-Expert Member
Sep 11, 2018
556
973
IMG_9601.JPG


Viongozi wa Kamati Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), wiki iliyopita walifanikiwa kuruka kiunzi na mtego mkali kwa ustawi wa Chama chao baada ya kuwabakiza Wabunge wake wawili walioonekana watukutu - Saed Kubenea na Anthony Komu. Hata hivyo, si kabla hawajaonyeshana ubabe wakati ambao kundi la Mbowe lilitaka wafukuzwe lakini kundi lililoongozwa na Edward Lowassa lilifanikiwa kutuliza hali na kuwabakiza Wabunge hao.

Viongozi wa Kamati Kuu waliotaka Kubenea na Komu wafukuzwe ndani ya Chama ni:
  • Freeman Mbowe - Mwenyekiti.
  • Mch. Peter Msigwa.
  • Godbless Lema.
  • Halima Mdee.
  • Ester Bulaya.
  • Boniface Jacob.
Viongozi wa Kamati Kuu waliowatetea Kubenea na Komu ni:
  • Dk. Vincent Mashinji - Katibu Mkuu.
  • Edward Lowassa.
  • Frederick Sumaye.
  • Joseph Mbilinyi.
  • Prof. Mwesiga Baregu.
  • Prof. Abdallah Safari.
  • Arcardo Ntagazwa.
  • Cecil Mwambe.
Inadaiwa kuwa, kundi la Mbowe lilifanya kampeni kubwa kabla ya Kikao hicho ili kuhakikisha Wabunge hao wanafukuzwa ndani ya Chama, sema tu kuwa kura hazikutosha.

Je, haya makundi yako hivyo accidentally ama ni organized. Time will tell but bila shaka uamuzi huu utakuwa umeongeza kambi ndani ya CHADEMA kuelekea katika Chaguzi za Chama.

IMG_9597.JPG

Wabunge Anthony Komu na Saed Kubenea.

IMG_9596.JPG
 
Ni kama umeandika kishabiki. Kwenye vikao kama hivyo kuwepo kwa kutofautiana maoni juu ya jambo lolote ni kitu cha kawaida, na ndio demokrasia yenyewe. Cha msingi ni hatimaye kwenda na maamuzi ya wengi.
Kwa mfumo wa Chadema uliokuwepo, nakuhakikishia hiki ni kitu kigeni kabisa kwa M/Kiti kupata upinzani hivi. Huu ni mwanzo wa mgawanyiko na makundi ndani ya Chadema. Kirusi kile kile kilichoitafunaga CCM kimeanza kuitafuna Chadema. Time will tell
 
Hiyo ndiyo demokrasia, maamuzi ni kwa njia ya vikao, siyo yale ukitoa maoni yako wanakutishia kumpiga shangazi yako na kukufukuza ubunge.
CCM ina demokrasia zaidi ya CDM mkuu!! Waulize wakina Zitto watakueleza yaliyowakuta ila kwa sasa ndani ya CDM kuna CCM ndiyo maana Mbowe na kundi lake wameshindwa kuwafukuza Komu na Kubenea.
 
Ama kweli mwaka huu Lumumba mtawashwawashwa kweli. Endeleeni tu tutaja Chadema kila siku.
 
View attachment 906840

Viongozi wa Kamati Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), wiki iliyopita walifanikiwa kuruka kiunzi na mtego mkali kwa ustawi wa Chama chao baada ya kuwabakiza Wabunge wake wawili walioonekana watukutu - Saed Kubenea na Anthony Komu. Hata hivyo, si kabla hawajaonyeshana ubabe wakati ambao kundi la Mbowe lilitaka wafukuzwe lakini kundi lililoongozwa na Edward Lowassa.

Viongozi wa Kamati Kuu waliotaka Kubenea na Komu wafukuzwe ndani ya Chama ni:
  • Freeman Mbowe - Mwenyekiti.
  • Mch. Peter Msigwa.
  • Godbless Lema.
  • Halima Mdee.
  • Ester Bulaya.
  • Boniface Jacob.
Viongozi wa Kamati Kuu waliowatetea Kubenea na Komu ni:
  • Dk. Vincent Mashinji - Katibu Mkuu.
  • Edward Lowassa.
  • Frederick Sumaye.
  • Joseph Mbilinyi.
  • Prof. Mwesiga Baregu.
  • Prof. Abdallah Safari.
  • Arcardo Ntagazwa.
  • Cecil Mwambe.
Inadaiwa kuwa, kundi la Mbowe lilifanya kampeni kubwa kabla ya Kikao hicho ili kuhakikisha Wabunge hao wanafukuzwa ndani ya Chama, sema tu kuwa kura hazikutosha.

Je, haya makundi yako hivyo accidentally ama ni organized. Time will tell but bila shaka uamuzi huu utakuwa umeongeza kambi ndani ya CHADEMA kuelekea katika Chaguzi za Chama.

View attachment 906839
Wabunge Anthony Komu na Saed Kubenea.

View attachment 906849
Ebu achana na chadema katika kikao chochote kuna kutofautiana mawazo lkn the end lenu linakuwa moja. Labda nikuulize nini maana ya kamati kuu??? Kwanini walikaa lazima mawazo yawe tofauti mwishoni mnaelewana. Na ndio maana kuna CCM na Opposition kwasababu mawazo ni tofauti. Lowassa alisema na anaendelea kusema ELIMU! ELIMU! ELIMU! Tanzania nakulilia wengi hawajielewi.
Gazeti la CCM unategemea ingeandika nn. Walifurahi wakijua akna Kubenea watafukuzwa lkn imekuwa tofauti. Wanaanza kugeuza maneno. Kapokeeni ubwabwa Lumumba kazi mmeimaliza
 
Wewe unaona swali lako inalandana na hii mada? Changia mada, sio kujua umri wa Watu hapa; haga ukifahamu hakuna ukachofaidika.
Wakati mwingine uelewa wa mambo unaenda sanjari na umri wa mtu ingawa sio lazima. Natilia shaka uelewa wako wa suala unalojadili!
 
Back
Top Bottom