Mkuu Kubenea,
Najua ni mwana JF; hata kama una mapenzi na mtu mmoja kwenye siasa za Kyela lakini magazeti yako hayana haki kuingia kuchafua watu wengine bila sababu zozote. Ulichoandika kwenye makala hii hasa kuhusu Mwakalinga ni majungu na uongo mtupu. Nitafafanua zaidi hapo chini.
UBUNGE WA MWAKYEMBE SHAKANI - kutoka gazeti la Mwanahalisi
Nguvu kubwa na za kifedha na mikakati ya kisiasa, zinatumika kuhakikisha John Mwakipesile, Mkuu wa Mkoa wa Mbeya anaingia katika kinyang'anyiro cha Ubunge mwaka kesho katika Jimbo la Kyela.
Lengo ni kutaka kumtokomeza kisiasa Mbunge wa sasa wa jimbo hilo, Dk. Harrison Mwamyembe, imefahamika.
Taarifa zinasema Mwakipesile anajengwa kisiasa na kiuchumi na mtandao mpana wa wanasiasa na wafanyabishara wakubwa nchini.
Miongoni mwa waliotajwa kumusimika Mwakipesile, aliyewahi kuwa mbunge wa Jimbo hilo ni mfanyabiashara na Mbunge wa Igunga Rostam Aziz, Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa, Mbunge wa Bukoba Vijijini Naziri Karamagi na mfanyabaishara Shubash Patel.
Rostam, Lowasa na Karamagi ni baadhi ya majeruhi wakuu wa kashifa ya mkataba wa kufua umeme kati ya serikali na Kampuni ya Richmond Development Company (LLC) aliyoibuliwa na Kamati Teule na Bunge, chini ya Mwakyembe.
Ni kamati ya Mwakyembe iliyomzamisha kisiasa Lowassa na Karamagi, Februari 2008, huku ikimuacha Rostam katika majeraha makubwa ya kisiasa na kiuchumi.
Wengine wanotajwa kuwa nyuma ya Mwakipesile ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa w a Mbeya, Nawab Mullah na Katibu Mkuu wa CCM, Yusuph Makamba.
Baadhi ya vijana waliohojiwa mjini Kyela wamemtaja pia Mkurugenzi Mstaafu wa Idara ya Usalama wa Taifa, Cornel Apson Mwang'onda.
Matokeo haya ya uchugnuzi wa muda mrefu yamesaidia kubaini uteuzi wa mwakipesile kuwa Mkuu wa Mkoa ule ule aliopotezea ubunge 2005, kuwa kiini cha haraka zake nyingi Wilayani kyela, ambazo zimeibua malalamiko kutoka kwa Mbunguw a sasa. Dk. Mwakyembe kuwa anahujumiwa kisiasa.
Alipoulizwa juu ya juhudi hizi za kumg'oa Mwakyembe alisema kwa ufupi, "Nimekuwa nikifanya kazi za umma ulionituma. Sitishiki na yeyote anayetaka nafasi hii. Wananchi ndio waamuzi."
Haraka za Mwakipesile kuingia kwenye kinyang;anyiro cha Ubungu mwakani zimechochea mwawazo hasi Mkoani Mbeya dhidi ya Rais Kikwete.
Kwa kumwacha Mwakipesile Mkoani Mbeya muda wote huu, kuna wanaomwona Kikwete kuwa ni "Mtu wa Visasi" na asiyepend akuzungukwa na wenye mawazo tofauti.
Rais Kikwete ameonyesha hampendi Mbunge wetu na sababu tunazijua. Mbunge wetu alimuunga mkono Profesa Mwandosya (Mark) kwenye kura za maoni za Urais mwaka 2005. Hivyo, alimteua Mwakipesile na kumbakiza Mbeya ili awakwamishe Mwakyembe na Mwandosya," anasema mfanyabiashara katika somo kuu la Kyela, jailo Mwangego.
Madai ya Mwangego yaliungwa mkono na wafanyabaishara wengine katika soko hilo, hasa wanawake, ambao walipandisha sauti zao wakidai kuwa Rais kikwete "anamwonea" Mbunge wao na kukemea kwa kusema juhudu za kumwangusha kwa kura mwakani "zitashindwa".
Baadhi ya wananchi waliohojiwa mjini Kyela, wanawataja madiwani wanane kuwani mawakala wa mwakipesile, ambao kazi yao kubwa ni kuzunguka Wialya nzima wakigawa magazeti bure yanayochapishwa kwa lengo la kumchafua mwakyembe na kumnadi Mwakipesile na "Vijana" wake.
Vijana wanotajwa kuwa wanafaa kuchukua ubungu wa Kyela ni George Mwakalinga, Hunter mwakifuna na Elias Mwanjala. Hata hivyo, inadaiwa kuwa mwakipesile yuko nyuma ya vijana hao.
George mwakalinga ni mwanafunzi na mjasiriamali anayeishi Uingereza. Inadaiwa alifuatwa London na Mwakipesile na Mwang'onda kuombwa agombee ubungu Kyela. Mwakalinga alifika Kyela Agosti mwaka huu na kuendesha kampeni ya kujinadi kwa mwezi mzima.
"Alifanya karamu kubwa kijijii kwao katumba, Songwe, kwa kuchinja Ng'ombe , kutangazia wananchi kuwa anaingia vitani. Alitembelea kata zote na kutoa misaada ya mabati na sementi.
Taarifa kuwa aligawa fedha kuanzia shs. 10,000 hadi 100,000 kwa uongozi wa CCM wa Vijiji na Kata, hazikuweza kuthibitishwa ingawa Edson matai wa Kasumul, mpakani na Malawi anadai anajua hili kuwa ni kweli.
Kwa mujibu wa nduguzake wanaoendesha baishara kwenye jengo la Kyela Devcelopment Corporaiton (KDC) mjini Kyela, Mwakalinga alirejea London September mwaka huu na hadi leo hajarudi Kyela. Aliacha nyuma "Kamati ya kampeni" inayodiwa kuratibiwa na Mwakipesile.
Hunter mwakifuna ni Mwenyekiti wa Umoja wa Viajna wa CCM (UVCCM) wa Wilaya, ambaye vile vile ni daktari Mfawidhi wa Kituo cha Afya cha Ipinda.
Mwakifuna anandamwa na tuhuma za kushusha umri wake kutoka miaka 35 hadi 28 ili kugombea nafasi hiyo ya vijana. Analalamikiwa pia na wakazi wa kata ya Ipinda kuwa anatumia muda mwigni kufanya siasa kuliko kazi yake.
Elias mwanjala, ni mfanyababishara maarufu anayeishi Dar es Salaam na ni mpwa wa Dk. Mwakyembe, ambaye inadaiwa ameungana na kundi linalomwandama mjomba wake. Haijafahamika ni kwa mapatano gani./
Mwanjala hakupatikana kuzungumzia hilo, bali inadaiwa ameachana na baishara ya malori ya uchukuzi na kwamba hivi sasa anaendesha baa iitwayo Stereo, Kinondoni, Dar es Salaam na anaagiza matairi ya magari kutoka Dubai.
Uchunguzi wa gazetiumethibitisha kuwa mwakipesile anatumia muda mwingi Wilayani Kyela kuliko Kituo chake Kikuu cha Kazi mjini Mbeya.
Taarifa zinasema Mwakipesile amekuwa akifnaya mikutano nyumbani kwake na hata kwa marafikizake wakubwa wawili waliotajwa kwa majina ya Glaswel mwakalulwa wa Kijiji cha Talatala na mahamudu Silwamba wa kijiji cha isaki.
Baadhi ya watumishi wa serikali Wilayani Kyela wanamtetea Mwakipesile kuwa pamoja na safari zake kyela kuwa nyingi, bado huko ndiko nyumbani kwa wazazi wake an baadhi ya asafri ni za "Kiserikali," ingawa wanashindwa kueleza iweje kila ziara ya kikazi iwe ya kumpiga vijembe Mbunge Mwakyembe.
Madai makuu ya mwakipesile dhidi ya Dk. Mwakyembe ni kuwa Mbungu huyo ni mgomvi na kwamba hakumtendea haki aliyekuwa Waziri Mkuu aliyeachia ngazi, Edward Lowassa, katika kashfa ya Richmond.
Inadaiwa kuwa Lowassa ni rafiki wa karibu wa Mwakipesile, ambaye inaaminika alifanya kazi kubwa kumshawishi Rais Kikwete kumpa wadhifa huo wa Mkoa wa Mbeya.
Madiwani wa Kyela wanaodaiwa kuwa mstari wa mbele kumnadi mwakipesile na "vijana wake ni Christopher Mullemwa wa Ipinda, Zuhura Omari wa Viti Maalum, Frida, Frida Mwampiki wa Matema, Viski Mahenge wa Kyela, edimasta Mwakibinga wa Ikama, Solomon Mwangalaba wa Ipande, I. Mwaipaja wa Lusungo na Watson Majuni wa Kajunjumele.
Magazeti wanayogawa ni yale yanayobeba ujumbe kuwa Mwakyembe hafanikiwi vile amegombana na viongozi wenzake, akina rostam, Lowassa, karamagi na Mwakipesile na kwamba " Rais Kikwete hamtaki," anadai Godwin Mwaipopo wa Ipinda, ambaye alidai kuhudhuria baadhi ya mikutano yao.
Msaidi wa Mbunge wa Kyela, Emmanuel Kiketelo Mwamlinge, amepuuzia madai hayo na kusema yanatokana na uelewa mdogo wa taratibu za bunge kwani maamuzi juu ya Richomond hayakuwa ya Dk. Mwakyembe bali ya bunge.