- Thread starter
- #41
Fidel80,Unajua Mwakalinga mbona kile kikundi ambacho kilikuwa kina jinadi kuwa kimeahidiwa laptop mbona hukukanusha na wala hukuwakataa kama ndo wapiga debe wako sasa hawa ndo walio chafua hali ya hewa.
Mbona nilikanusha hilo la laptop? Hakuna shule au mtu yeyote niliyemwahidi laptop, unajua JF watu wanakuza mambo mpaka unacheka.
Hata huko jimboni wakati mwingine inabidi uwe mkali. Unakuta mtu uliyeongozana naye amesema jambo ambalo mpaka unaona aibu. Inabidi ukitoka hapo umwambie, mambo kama hayo hutaki. Mtu anatangazia umma kwamba una uwezo wa kujenga mbingu, wakati hata uwezo wa kutengeneza baiskeli huna.
Siasa za TZ zinatakiwa mabadiliko makubwa sana hasa upande wa kusema ukweli. Wapambe wanaweza kufikiri wanamjengea mtu kumbe wanambomoa. Mimi kule Kyela baada ya siku ya kwanza, nikawatoa wapambe kwenye utangulizi maana walikuwa wanawaambia wananchi uwongo ambao nisingependa kusikia.
Ukiwaambia hapana tusifanye hivyo, wanakumabia mambo mengine utarekebisha baada ya kupata. Ukiwakataza tayari ni ugomvi, wanaanza kudai huwaamini, unaleta mambo ya Ulaya nk.
Ni kazi kweli kweli, muhimu ni kutokukubali kubadili maadili au misimamo yako kirahisi. Wakati mwingine ni bora ushindwe huku umebaki na maadili yako kuliko kutafuta ushindi kwa njia zozote zile.
Siasa za TZ ni ngumu mno kwa mtu anayeamini. Mwenyewe nimejiuliza mara nyingi, natafuta nini hapa? Lakini pia unaona opportunities za kuweza kusaidia zilizopo na kwa matatizo ya kule vijijini, hata ukiweza kuwasaidia watu 20 kubadili maisha yao huenda ni bora kujaribu.