Kubenea na siasa za Kyela

Status
Not open for further replies.
Unajua Mwakalinga mbona kile kikundi ambacho kilikuwa kina jinadi kuwa kimeahidiwa laptop mbona hukukanusha na wala hukuwakataa kama ndo wapiga debe wako sasa hawa ndo walio chafua hali ya hewa.
Fidel80,

Mbona nilikanusha hilo la laptop? Hakuna shule au mtu yeyote niliyemwahidi laptop, unajua JF watu wanakuza mambo mpaka unacheka.

Hata huko jimboni wakati mwingine inabidi uwe mkali. Unakuta mtu uliyeongozana naye amesema jambo ambalo mpaka unaona aibu. Inabidi ukitoka hapo umwambie, mambo kama hayo hutaki. Mtu anatangazia umma kwamba una uwezo wa kujenga mbingu, wakati hata uwezo wa kutengeneza baiskeli huna.

Siasa za TZ zinatakiwa mabadiliko makubwa sana hasa upande wa kusema ukweli. Wapambe wanaweza kufikiri wanamjengea mtu kumbe wanambomoa. Mimi kule Kyela baada ya siku ya kwanza, nikawatoa wapambe kwenye utangulizi maana walikuwa wanawaambia wananchi uwongo ambao nisingependa kusikia.

Ukiwaambia hapana tusifanye hivyo, wanakumabia mambo mengine utarekebisha baada ya kupata. Ukiwakataza tayari ni ugomvi, wanaanza kudai huwaamini, unaleta mambo ya Ulaya nk.

Ni kazi kweli kweli, muhimu ni kutokukubali kubadili maadili au misimamo yako kirahisi. Wakati mwingine ni bora ushindwe huku umebaki na maadili yako kuliko kutafuta ushindi kwa njia zozote zile.

Siasa za TZ ni ngumu mno kwa mtu anayeamini. Mwenyewe nimejiuliza mara nyingi, natafuta nini hapa? Lakini pia unaona opportunities za kuweza kusaidia zilizopo na kwa matatizo ya kule vijijini, hata ukiweza kuwasaidia watu 20 kubadili maisha yao huenda ni bora kujaribu.
 
Fidel80,

Mbona nilikanusha hilo la laptop? Hakuna shule au mtu yeyote niliyemwahidi laptop, unajua JF watu wanakuza mambo mpaka unacheka.

Hata huko jimboni wakati mwingine inabidi uwe mkali. Unakuta mtu uliyeongozana naye amesema jambo ambalo mpaka unaona aibu. Inabidi ukitoka hapo umwambie, mambo kama hayo hutaki. Mtu anatangazia umma kwamba una uwezo wa kujenga mbingu, wakati hata uwezo wa kutengeneza baiskeli huna.

Siasa za TZ zinatakiwa mabadiliko makubwa sana hasa upande wa kusema ukweli. Wapambe wanaweza kufikiri wanamjengea mtu kumbe wanambomoa. Mimi kule Kyela baada ya siku ya kwanza, nikawatoa wapambe kwenye utangulizi maana walikuwa wanawaambia wananchi uwongo ambao nisingependa kusikia.

Ukiwaambia hapana tusifanye hivyo, wanakumabia mambo mengine utarekebisha baada ya kupata. Ukiwakataza tayari ni ugomvi, wanaanza kudai huwaamini, unaleta mambo ya Ulaya nk.

Ni kazi kweli kweli, muhimu ni kutokukubali kubadili maadili au misimamo yako kirahisi. Wakati mwingine ni bora ushindwe huku umebaki na maadili yako kuliko kutafuta ushindi kwa njia zozote zile.

Siasa za TZ ni ngumu mno kwa mtu anayeamini. Mwenyewe nimejiuliza mara nyingi, natafuta nini hapa? Lakini pia unaona opportunities za kuweza kusaidia zilizopo na kwa matatizo ya kule vijijini, hata ukiweza kuwasaidia watu 20 kubadili maisha yao huenda ni bora kujaribu.
tutashinda!....................
 
- Well kama kawaida yetu, huwa tunataka kwanza kusikia toka upande wa pili yaani hapa umebaki upande wa Kubenea, sasa yeye aliwahi kusema hapa upanga ni kwa upanga, ajitokeze ili tujue ukweli ulipo!

- Ingawa sio siri kwamba baadhi ya habari zake katika hii article, knowing Mwakalinga as I do zina walakini, lakini bado tutnampa the benefit of the doubt kama demokrasia inavyotaka, sasa ajitokeze tuone jinsi upanga kwa upanga, kama kweli ni theory of the truth au ni majungu at best!

Respect.

FMEs!

Ninakuunga mkono FMEs kwa 100%.Kubenea ajitokeze kujibu haya madudu aliyoandika.
 
- Well kama kawaida yetu, huwa tunataka kwanza kusikia toka upande wa pili yaani hapa umebaki upande wa Kubenea, sasa yeye aliwahi kusema hapa upanga ni kwa upanga, ajitokeze ili tujue ukweli ulipo!

- Ingawa sio siri kwamba baadhi ya habari zake katika hii article, knowing Mwakalinga as I do zina walakini, lakini bado tutnampa the benefit of the doubt kama demokrasia inavyotaka, sasa ajitokeze tuone jinsi upanga kwa upanga, kama kweli ni theory of the truth au ni majungu at best!

Respect.

FMEs!
.

Good fms!.ajitokeze.nafikiri sasa imefikia muda watu wajulikane kwa majina yao halisi.
 
Movie;

Be aware!

na magazeti ya Kubenea na Kibanda kwenye chaguzi za vyama mbalimbali, na nafasi yao katika jamii!-HATARI!

Ikiwa tunapiga kelele Mengi na vyombo vyake vya habari! mara RA na vyombo vyake vya habari!

Then haya magazeti ya akina Kubenea na Kibanda hayana tofauti na ya akina RA na Mengi, wote wanafanya kitu kile kile.AFADHALI mara mia Mengi na RA!

Kwa waandishi wa habari wahariri kuonyesha personal interest kutumia nafasi zao ni hatari zaidi, hasa katika jamii ambayo hapo kwanza iliwahi kuwaamini! Ulimwengu alishafannya kama haya alijuta baadaye na Rai yake

semeni yote; Kubenea and Kibanda is another ticking bomb, simply kwa sababu walificha makucha yao, wakaiteka jamii sasa wanajifunua wazi wazi ni akina nani!

Yaani nchi hii kila mtu atakuwa na gazeti lake sasa!
Tatizo la Tanzania ni kwamba uandishi wa habari wanadhani ni seheme ya kujipatia utajieri hivyo wamekuwa ni mamluki kwa kuhongwa fedha kwa ajili ya kumchafua mtuu thats why wa tz tunadharauliwa sana katika taaluma zetu
 
George Mwakalinga sio kijana kama unavyotaka kuonyesha, ana miaka 44 ambayo ni zaidi ya kuwa kijana.





Mwakalinga alimaliza shule mwaka 1997. Aliajiriwa na Lucent Technologies miezi michache kabla ya kumaliza shule yake. Baada ya kufanya kazi Lucent miaka minane, December 2005 alihamia Huawei Technologies ambako yuko mpaka sasa. Mwakalinga hajawahi kukosa kazi hata siku moja tokea alipomaliza masomo 1997. Sasa huo ni uanafunzi gani baada ya miaka 12? Lengo ni lile lile kudanganya watu waone Mwakalinga ni kijana tu! ni mwanafunzi tu.



George Mwakalinga hakufuatwa London na Mwakipesile au Mwang'onda. Sijui hata kama Mwakipesile amewahi kuwa London miaka ya karibuni. Mwakalinga aliamua kugombea ubunge tokea mwaka 2007 na March mwaka huo alituma watu kuonana na mwenyekiti wa CCM wilaya ya Kyela, bwana Mwakasumi na kumwambia dhamira ya Mwakalinga kugombea ubunge Kyela mwaka 2010. Picha na uthibitisho mwingine wa mkutano huo ambao ulifanyika pale Sativa Kyela vipo. Kumbuka hiyo ilikuwa mwaka mmoja kabla hata report ya Richmond kusomwa bungeni.

Mwakilishi wa Mwakalinga alikutana na Mwakipesile mwaka 2009, February kumwambia kuhusu dhamira ya Mwakalinga kugombea ubunge Kyela. Hiyo ni miaka miwili tokea Mwakalinga aanze harakati za kuwaambia baadhi ya wadau wa Kyela kwamba ana mpango wa kugombea. Team Mwakalinga iliamua kumwona Mwakipesile baada ya kupata uhakika wa kiasi kwamba Mwakipesile hana mpango wa kugombea. Kabla ya hapo hakukuwahi kuwa na mawasiliano yoyote kati ya Mwakalinga na Mwakipesile. Kuna watu wengine mbalimbali wa Kyeala, wanasiasa na wasio wanasiasa ambao team mwakalinga imekutana nao kuwaambia juu ya dhamira yake ya kugombea. Kama kukutana na mwana Kyela yeyote London au TZ ni makosa, si wataje wote niliowahi kukutana nao wakiwemo waliotumwa kunishawishi nisigombee? Watajeni akina Kifukwe, na wazito wengine huko jeshini.



Wana JF wanajua maana hiyo safari ilijadiliwa vikali hapa JF. Mwakalinga alikuwa Kyela kwa siku sita. Alifika yeye pamoja na familia yake siku ya Jumatatu (24/07/09) na kuondoka Kyela Jumamosi usiku (30/07/09). Kwahiyo, mwezi August Mwakalinga hakuwa Kyela wala hakukaa Kyela mwezi mzima.


Mwakalinga kila mara anaporudi nyumbani na familia yake yote hufanya sherehe ya pamoja kama njia ya familia yote kukutana pamoja maana kunakuwa hakuna muda wa kutembelea kila mtu katika siku hizo chache. Mwaka 2003 pia alipoenda na familia yake alifanya sherehe nyumbani na kuhudhuriwa na ndugu wote pamoja na majirani. Mwaka huu pia alienda nyumbani na familia ikiwa ni pamoja na mtoto wake wa mwisho ambaye alifika nyumbani kwa mara ya kwanza. Sherehe ya mwaka huu ikaongezewa nguvu na uamuzi wake wa kutangaza nia ya kugombea ubunge. Sherehe ilihudhuriwa na ndugu na wananchi wengine wa maeneo ya jirani. Hakukuwa na speeches wala maneno ya kwamba anaingia vitani.


Uongo! alitembelea kata 19 kati ya 21. Hakutoa msaada wowote wakati wa ziara nzima. Mwakalinga anatoa misaada mashuleni kwa muda wa zaidi ya miaka 15 sasa. Kuna kitabu cha misaada yote kiko pale Kyela Business Center (KBC) na anayetaka kuangalia anaweza kuhakiki na kuona lini alitoa msaada gani na wapi. Misaada yote hutolewa kiuwazi ila bila sherehe maana muda wote alikuwa hataki publicity.


I wish Mwakalinga angelikuwa na pesa zote hizo. Uwongo mkubwa sana! Hakuna hata mwananchi mmoja wa Kyela anayeweza kuthibitisha kwamba alipewa pesa kati ya shilingi 10,000 na 100,000. Kama yupo aende polisi kutoa taarifa. Tunamtafuta huyo Edson Matai ili kama kweli ni raia basi tumsaidie kumpeleka polisi ili akatoe ushahidi. Tumechoka Kyela kusingiziwa mambo ya ajabu. Inabidi tuanze kuwashughulikia wale wanaoona wanaweza wakasema au kuandika lolote bila ya chembe ya ukweli.



Hata ukimwuliza kichaa Kyela anajua kuna sehemu panaitwa KBC. Sasa mwandishi gani huyu na uchunguzi wa muda mrefu hata hajui kwamba hiyo kampuni inaitwa Kyela Business Center (KBC)? Hiyo KDC labda ni kampuni ya Kubenea ya kufikirika. Unajua habari za kupewa na watu wengine huwezi kuwa sahihi nazo.

Sasa huyo Mwakipesile, yeye mwenyewe anagombea ubunge na mara anaratibu shughuli za ubunge za Mwakalinga, mbona hayo maajabu?

Ni aibu kwa mtu kama Kubenea ambaye unajifanya mpiganaji, kuanza kutumia gazeti lako kuchafua watu wengine bila sababu zozote. Najua ni msomaji wa JF na kwa vyovyote unajua anayeongelewa kuhusu siasa za Kyela ni Mwakalinga mwana JF. Umeshindwa nini kuniuliza mimi Mwakalinga aka Mtanzania kujua ukweli? Mmezunguka kutafuta uchafu wowote na mmeshindwa sasa mnataka kumchafua mtu kwa kumhusisha kwa karibu na watu ambao mnawaona wachafu. Tatizo lenu ni kwamba hamuwezi hata sehemu moja kupata mahali ambapo Mwakalinga yuko karibu au hata anafahamiana na akina Lowassa, RA, Karamang au huyo Patel.

Mlianza na kusema Mwakalinga amepewa milioni 400. Mmeona wana Kyela wote wamewadharau baada ya kuona hizo milioni 400 hawazioni na hakuna mtu hata mmoja ambaye anaweza hata akasema amepewa laki moja na Mwakalinga. Sasa mnaanza majungu mengine ya kijinga, lakini na yenyewe yataishia patupu maana hamna data na uongo haudumu hata siku moja.

Acheni majungu na fitina; waache wana Kyela wachague kiongozi wanayemtaka kwa utashi wao. Kama mna ugomvi na Mwakipesile, pelekeni nguvu huko, kuanza kujaribu kumhusisha kila mtu haitawasaidia maana wana Kyela sasa wanajua nani anasema ukweli na nani anakimbilia magazetini kila saa kupaka wana Kyela wenzake.

Kumbe ndio maana watu wengine mnamwagiwa tindikali shauri ya kuandika majungu ambayo hayana ukweli hata mdogo. Ni taaluma gani hizo za kutumiwa na wanasiasa kuandika kila wanalotapika?

Shame on You Kubenea and your Newspaper!

Wana Kyela sio nyie peke yenu mnaomuunga mkono Mwakipesile wapo Wanakyela wengine ambao wako nyuma ya Mwakyembe vile vile.

Mie sioni lolote baya aliloandika KUBENEA zaidi ya kueleza kwa kina hali halisi ya kisiasa na jinsi ambavyo Mwakyembe anapigwa vita.
Watanzania tufike mahali tuelewe maana yademokrasia na kwamba kila mtu anao uhuru wa kusema lile analowaza, analojua, alilosikia n.k. bila kuonekana kwamba ana majungu dhidi ya watakaoguswa!

Je kubenea amevunja sheria gani kwa kueleza yale aliyoyasikia na yanayozungumzwa na wananchi kuhusu yanayotokea Mkoani Mbeya? Mwacheni Kubenea atuhabarishe tujue jinsi nchi inavyovurugwa na watu wenye uchu wa madaraka ambao kwao wao uongozi hununuliwa kwa fedha na kwa kuwachafua wenzao kwa kutumia fedha zao.
 
Ndugu yangu Mwakalinga mpaka sasa umejifunza nini katika mchakato mzima huu? Sijui kama unaelewa kuwa siasa za Bongo ni maji taka, kama unaelewa je nn lengo lako hasa la kutaka kugombea ubunge?
 
Kumbe ndio maana watu wengine mnamwagiwa tindikali shauri ya kuandika majungu ambayo hayana ukweli hata mdogo. Ni taaluma gani hizo za kutumiwa na wanasiasa kuandika kila wanalotapika?

Shame on You Kubenea and your Newspaper!

Kama unaweza kupongeza uhalifu wa namna hiyo ni dalili kwamba hujakomaa kisiasa.

Jifunze ustahimilivu vinginevyo watu watajiuliza mara mbilimbili!

Nikutakie mpambano mwema lakini jiandae kukabilia na changamoto kali zaidi ya hiyo.
 
Nimesoma George siasa za huko kwenye ni mbaya sana lakini umeamua kuingia kucheza ngoma za kikwenu kaza buti na kwa kuwa unagombea ama una mapenzi na chama kinacho tumaliza sis watanzania basi tuta kumulika maana labda ungali enda upinzani japokuw abado ni haki yako kuingia CCM tungaliona nia yako ya kutaka kukokomboa watanzania wa huko unakosema .Ila uko ndani ya CCM haya twende na karibuni mwaka 2010
 
huyu sio tu ni upande wa mwakalinga, ndiye mwakalinga haswaaaaa
soma hapa najua ni msomaji wa JF na kwa vyovyote unajua anayeongelewa kuhusu siasa za Kyela ni Mwakalinga mwana JF. Umeshindwa nini kuniuliza mimi Mwakalinga aka Mtanzania kujua ukweli?

Mwakalinga has taken out his veil and announced that he is our JF'S Mtanzania!! Mwakyembe inasemekana yeye anaingia humu JF kwa majina mengi tu lakini si la Mwakyembe; will he be courageous enough like his nemesis to announce his true identity hapa ukumbini? hiyo itatusaidia kujua kama ninani anaetoa hoja badala ya sasa ambapo wahusika ndio wanaoandika nasi tunadhani ni wapambe wao!! Mtu yeyote anaeandikaka kitu anachokiamini na si majungu hawezi kujificha kwa kutumia majina bandia; mbona sisi wengi tunatumia majina yetu humu janvini!!
 
Mtasikia mengi ukifika hasa huo mwaka 2010,huu ni mwanzo tu na hilo ni jimbo moja tu bado yale mambo ya wazee wa Singida wanaotaka kijana fulani toka USA arudi ili "Kukomboa" jimbo la singida mjini!!!
 
Nafikiri wengi mliotoa comment ni wepesi sana wakusahau hapa tulipo leo asingekuwa kubenea na Mwakyembe sijui kama tungefika maana hata JF sina uhakika kama tulikuwa huru kutamka mafisadi kama tunavyotamka sasa. Wao ndio wame-risk maisha yao kwaajili ya maslahi ya umma. Tanzania kuna mashujaa watatu walioweza kujitoa ktk kupambana na Mafisadi hao sio wengine ni Dr. Slaa, Dr. Mwakyembe na Kubenea....

Ninawaomba wana JF wenzangu tuwaheshimu hawa jamaa na tuachane na majungu ambayo hayana msingi na tupunguze hasira tutumie busara na hekima.
 
Wana JF toeni hoja acheni kutukanana kupitia thread. Kama mna visa vyenu pelekeni uswahilini. Pinganeni kwa hoja si kwa matusi! Mf."Shame on You Kubenea and your Newspaper!" by Mtanzania, na "3.Wapo maswahiba wake hapa(MWAFRIKA NA MASANILO) watatufafanulia zaidi kuhusu Ujinga wa mbunge huyu mwenye mdomo mkubwa.Kulia kwenye media ndiyo kutatua matatizo yake." by Samwel Let the JF be The Home of Great Thinkers and not rigmaroles.
 
Mengine uliyoandika ni safi......however this one

....................Kumbe ndio maana watu wengine mnamwagiwa tindikali shauri ya kuandika majungu ambayo hayana ukweli hata mdogo. Ni taaluma gani hizo za kutumiwa na wanasiasa kuandika kila wanalotapika?

Shame on You Kubenea and your Newspaper!

Yes wewe ni binadamu kama wengine lakini..........that one........speaks volume..........

Hebu msome Mangi hapa chini........

Waungwana ni bora tubandike hoja kwa hoja na tuachane na mambo personal. Sidhani kama ni jambo la busara kuhusisha crime aliyofanyiwa mtu na mpambano wa hoja hapa JF,binafsi naamini hiyo ni foul...Kama Kubenea angekuwa amepigwa kisu ama risasi,basi huwezi kuja hapa na kusema kuwa ndiyo maana ulipigwa risasi ama ulichomwa kisu,ni sawa na mnapodai kuhusu kumwagiwa tindikali,kama hayo ya kumwagiwa tindikali hayahusiani na dhumuni hasa la mjadala huu ama hoja zake,basi si vyema kuzi bring up kwa style hiyo kwasababu ni kama uonevu,kwani kumwambia kuwa alifanyiwa shambulizi la kinyama kwa kukosa hoja ni sawa na kumdiscourage na yeye kutoa hoja zake hapa JF,na kama shambulizi hilo alifanyiwa kwasababu nyinginezo kama inavyokuwa speculated kuhusu mke wa mtu,je hilo linahusiana kivipi na uandishi wake?Ama uwezo wake wa kuchangia hapa JF?ama linahusiana vipi na makala yake hiyo kuhusiana na kina Mwakalinga?Na kwahiyo watu mnaojiita great thinkers mnakubaliana na watu kujichukulia sheria mkononi?Kuna mtu humu ndani ambaye hajawahi kumuudhi mtu mwingine the same way Kubenea alivyomuudhi mshambuliaji wake?Na kama wamo watu ambao wameshawaudhi wengine kwa namna moja ama nyingine,je muna encourage kuwa wajichukulie sheria mkononi?Na kwahivyo basi hata yule aliyem mwagia tindikali Kubenea kama na yeye anapita hapa JF basi anafurahia tu na kuona amefanya jambo la maana.

So naamini kabisa ujumbe ungekuwa umefika bila ya kum "Blackmail" victim wa crime kwenye mijadala,hiyo ni personal issue,ni shambulizi lililomwathiri kwa kiasi kikubwa na si ustaarab kufurahia mabaya yanayompata mtu na on top of that unam nyanyapalia.
Ma two cents.

.........notwithstanding the above.......Nakutakia kila la Kheri Mwakalinga aka Mtanzania wa JF
 
Mwakalinga has taken out his veil and announced that he is our JF'S Mtanzania!! Mwakyembe inasemekana yeye anaingia humu JF kwa majina mengi tu lakini si la Mwakyembe;

Inasemekana wapi, kwenye kijiwe cha gahawa au kwenye kilabu cha ulanzi pale kwa mama Gwakugole?

will he be courageous enough like his nemesis to announce his true identity hapa ukumbini? hiyo itatusaidia kujua kama ninani anaetoa hoja badala ya sasa ambapo wahusika ndio wanaoandika nasi tunadhani ni wapambe wao!!

Atumie jina lake ili iweje? na itakusadia wewe na nani?

Mtu yeyote anaeandikaka kitu anachokiamini na si majungu hawezi kujificha kwa kutumia majina bandia; mbona sisi wengi tunatumia majina yetu humu janvini!!

Bulesi, mbona wewe unatumia majina bandia? ni kwa vile unaandika majungu au kwa vile hauko courageous enough?
 
Wana JF toeni hoja acheni kutukanana kupitia thread. Kama mna visa vyenu pelekeni uswahilini. Pinganeni kwa hoja si kwa matusi! Mf."Shame on You Kubenea and your Newspaper!" by Mtanzania, na "3.Wapo maswahiba wake hapa(MWAFRIKA NA MASANILO) watatufafanulia zaidi kuhusu Ujinga wa mbunge huyu mwenye mdomo mkubwa.Kulia kwenye media ndiyo kutatua matatizo yake." by Samwel Let the JF be The Home of Great Thinkers and not rigmaroles.

Bwa ha ha ha,

Mdomo huo ni mkubwa kama wa Haruna au kama wa Malima?
 
Mengine uliyoandika ni safi......however this one



Yes wewe ni binadamu kama wengine lakini..........that one........speaks volume..........

Hebu msome Mangi hapa chini........



.........notwithstanding the above.......Nakutakia kila la Kheri Mwakalinga aka Mtanzania wa JF

Mwakalinga kafulia big time kwenye hii kampeni yake. Yaani mambo anayoandika hapa (na wapambe wake) utadhani kama hakusomea shule ya IT kule Porrrrrrraaaandi.

Usijekucheza na pesa za kifisadi toka Monduli, zinageuza kila kitu.
 
.

1.Mwakyembe ka-divorce na Mengi na sasa ameoana na Kubenea.Huyu bwana ndiyo maana alimwagiwa tindikali usoni.Ata gazeti lake limeanza kukosa ubora tena.Limejaa majungu,unafiki na uongo.

Great,

Kama Mwakyembe ka-divorce na Mengi (big if...), je timu Mwakalinga itafunga rasmi ndoa na fisadi Rostam lini?

2.Inasemekana Mwanadishi wa nakala hiyo ni Mwakyembe mwenyewe na hiyo ni tabia yake.Alikuwa akiifanya ata kwenye gazeti la Nipashe bila kutaja jina la mwandishi.Sasa huko wamemshitukia alipoandika habari za uzushi kuhusu kuchomwa kisu ili watu waamini eti anaandamwa na mafisadi.

Ha ha ha,

inasemekana wapi? porrraaandi?

3.Wapo maswahiba wake hapa(MWAFRIKA NA MASANILO) watatufafanulia zaidi kuhusu Ujinga wa mbunge huyu mwenye mdomo mkubwa.Kulia kwenye media ndiyo kutatua matatizo yake.

Bwa ha ha ... huu mdomo ukubwa wake ni nusu au robo ya mdomo wa Samwel?
 
Mengine uliyoandika ni safi......however this one



Yes wewe ni binadamu kama wengine lakini..........that one........speaks volume..........

Hebu msome Mangi hapa chini........



.........notwithstanding the above.......Nakutakia kila la Kheri Mwakalinga aka Mtanzania wa JF

Ogah,

Ni rahisi sana ukiwa pembeni kuandika kama ulivyoandika. Lakini kwa mtu ambaye sasa miezi minne anatolewa kwenye magazeti ya nchi kwamba ni fisadi, kibaraka wa mtu, katuma vijana kuchoma mtu kisu, kamwagiwa mapesa na ujinga mwingine ambao hauna hata chembe ndogo ya ukweli. Hata watu ambao hawakujui wanaanza kuamini kwamba wewe ni mwizi. Inafika sehemu unasema enough is enough, siasa za jino kwa jino nazo zinafanywa na binadamu. Fuata sheria na maadili ya kazi yako, hakuna atakayekugusa. Ni maadili gani ya uandishi wa habari hao tunaowajadili hapa wanafuata?

Mkuu nimejifunza, Nipashe waliandika mambo ya hovyo hivyo hivyo. Msamalia mmoja wa JF hapa akaniunganisha na mhariri wao na nikaamua kuwa muungwana. Nikampigia simu kumwambia habari mliyoandika haina ukweli kabisa, chunguzeni. Kesho yake ndio akatoa makubwa zaidi kwamba kuna sms zimekutwa zikionyeshwa pesa zinavyosambazwa kutoka nje kupitia Arusha. Huku akijua ni uongo mkubwa wala hakuna kitu kama hicho. Unataka mtu kama huyo nimwambie nini tena zaidi ya lugha anayostahili? Kuna siku nitamwona uso kwa uso na nimwambie lugha anayostahili.

Nimetumia jina langu ili kila mtu awe una uhakika 100% kwamba alieandika ni Mwakalinga mwenyewe..

Uzuri wote wanaotumia magazeti yao kuchafua watu wengine wanajulikana. Na kila baya mtu analofanya kuna siku utawajibika nalo tu.

Hakuna anayekataza mwandishi kumchunguza mwanasiasa na huko kugundua scandals zilizojificha na kuzianika. Lakini sio sahihi kusema umemkuta Ogah anaiba kuku, huku unajua kabisa hujamwona Ogah popote hata akiiba kitumbua.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom