Kubenea ampa onyo kali Nape

Kubenea ampa onyo kali Nape

Aaaaah!, NAPE!!!!! KUMBE ndiyo wewe puppet wa CCM msimu wa JK. Ngoja panga ligeuke then uisome namba, watu WANANG'ATA NA KUPULIZA: Then wanachungulia kwa dirisha!!.
 
Kuna point za muhimu katika suala hili:
  1. Kubenea anasema Nape alikuwa mwandishi na chanzo cha habari wa Mwanahalisi wakati hana cheo ndan ya CCM. Kwa Kebenea hili ni kosa kubwa maana mwandishi mueledi hawezi kutaja jina la source yake hata akishurutishwa na wanausalama.
  2. Wanahojiwa Wahariri wa lililokuwa gazeti la Mawio. Kama Gazeti limeshafungiwa wanahojiwa nini? Ilitakiwa kuanza na kuwahoji na kuwafungulia mashtaka ya uhalifu au kulifungia gazeti? Kama gazeti limefungiwa, mhariri anatoka wapi?
Mwanahalisi na Tanzania Daima nao wamekalia kuti kavu. Walipaswa kutambua kuwa baada ya Nape kupewa ile Wizara, walikuwa wameshika makali. Walitakiwa walau wapaze sauti zao kupingwa kuteuliwa kwa propagandist wa chama kusimamia wizara hiyo.
 
Serikali hii ya Tanzania inavunja record dunia nzima kwa kutaka kusifiwa tuu na vyombo vya habari!viongozi wengi ambao sio waadilifu hawataki vyombo vya habari vifichue maovu yao,hivi tutafika kweli?mbona inchi zingine hazifanyi ivyo?yani kiongozi anataka aibe mali za watanzania mwandishi akimfichua anapelekwa mahakamani?hivi wapo kwa ajili ya kusifia tuu serikali?kwa staili hii hatutakomesha ufisadi ndani ya inchi hii,ndio maana wanaichi wanawajua wahalifu wanaogopa kutoa taarifa police kwa kuwa wanaweza kamatwa na wao wakaambiwa wachochezi!Ila sishangai huenda ikawa ndio agenda kuu ya serikali kufungia vyombo vya habari vinavyosifia upinzani!
 
nashangaa eti Standard seven leaver Kubenea, mzee wa elimu ya hapa na pake anampa onyo msomi Nape. Hapa kweli ni kazi tu! ! we need to change ! hatutaendelea kwa mtindo huu....
 
Mkuu, nafikiri bado bunge halijaanza na nafikiri pia hiyo ni fani yake.

Inaonekana una-miss the point regarding the matter in question...
 
Kusema ukweli tukiacha unazi wa uchama na kiupinzani...gazeti la MAWIO lilikuwa likiandika habari zake kinyume na maadili ya kiundishi...ingawa sikubaliani na suala kufungiwa kwake lilipaswa kupewa onyo tu....
Mkuu kulingana na maelezo ya Nape mawio wamepewa onyo zaidi ya mara tisa..!
 
Serikali hii ya Tanzania inavunja record dunia nzima kwa kutaka kusifiwa tuu na vyombo vya habari!viongozi wengi ambao sio waadilifu hawataki vyombo vya habari vifichue maovu yao,hivi tutafika kweli?mbona inchi zingine hazifanyi ivyo?yani kiongozi anataka aibe mali za watanzania mwandishi akimfichua anapelekwa mahakamani?hivi wapo kwa ajili ya kusifia tuu serikali?kwa staili hii hatutakomesha ufisadi ndani ya inchi hii,ndio maana wanaichi wanawajua wahalifu wanaogopa kutoa taarifa police kwa kuwa wanaweza kamatwa na wao wakaambiwa wachochezi!Ila sishangai huenda ikawa ndio agenda kuu ya serikali kufungia vyombo vya habari vinavyosifia upinzani!
Hata kusema Zanzibar kuwaka Moto nayo ni uovu pia..!
 
Mkurugenzi wa Kampuni ya Hali
Halisi Publishers, Saed Kubenea
pamoja na Mwenyekiti wa
Jukwaa la Wahariri Tanzania
(TEF) Absalom Kibanda
wameionya serikali juu ya
uamuzi wa kulifuta gazeti la
MAWIO uliochukuliwa hivi
karibuni.
Kupitia tangazo la serikali lenye
notisi namba 55, serikali
ilichukua uamuzi wa kulifungia
MAWIO, Januari 15, 2016 huku
Waziri wa Habari, Utamaduni,
Sanaa na Michezo, Nape Nnauye
akisema gazeti hilo limekuwa
‘sugu’ kwa uchochezi tangu
2013.
Kubenea na Kibanda walikuwa
katika kituo cha Polisi cha Kati
ambapo ndiyo Makao Makuu ya
Kanda Maalum ya Dar es Salaam
wakiwasindikiza wahariri Jabir
Idrissa na Simon Mkina
walioitikia wito wa uliotolewa na
jeshi hilo siku tatu zilizopita.
Kibanda amewambia
wanahabari kuwa kitendo cha
jeshi la polisi kuwasaka ili
kuwakamata Jabir na Mkina
ambao ni wahariri ili kuwahoji
huku gazeti la MAWIO likiwa
limefungiwa, kinalenga
kuwatisha waandishi wa habari
nchini na kuzima uhuru wa
habari.
Ameulezea uamuzi huo wa
Waziri mwenye dhamana ya
masuala ya Habari, Nape, kama
uamuzi uliolishitua TEF na
wamewasiliana naye wakielezea
mshituko na masikitiko yao.
“Hatuwezi kuvumilia kufungiwa
kwa vyombo vya habari,
kukamatwa na kunyanyaswa
kwa waandishi, miaka miwili
iliyopita nilitakiwa kujisalimisha
makao makuu ya polisi,
nikafikishwa mahakamani na
nikashinda kesi, naelewa
maumivu ya mapambano haya,”
ameeleza Kibanda.
Kwa upande wake Kubenea,
amesema Serikali kupitia Nape
imechukua uamuzi wa kikatili
dhidi ya gazeti la MAWIO ili
kuzima sauti ya wananchi kwa
hoja zisizo na mashiko ikiwemo
ile ya uchochezi ambayo
imekuwa kisingizio cha
watawala kwa muda mrefu.
“Katika toleo la MAWIO lilimnukuu
Maalim Seif akijitangaza mshindi,
yeye hakuitwa mchochezi, Jecha
amefuta uchaguzi wakati hana
mamlaka ya kisheria wala ya
kikatiba hakuitwa mchochezi ila
gazeti kuandika ushindi
uliotangazwa na Seif
limefungiwa,” ameeleza Kubenea.
Kubenea ameongeza kuwa,
ubovu wa sheria ya magazeti ya
mwaka 1976 umekuwa
ukitumiwa na serikali kuviadhibu
vyombo vya habari vinavyofichua
maovu, huku mahakama
ikithibitisha mara kadhaa kuwa
madai ya uchochezi
yanayotolewa na serikali hayana
mashiko.
“Jabir ni Mwandishi aliyebobea
kitaaluma na uzoefu, ameandikia
magazeti ya Uhuru, Mzalendo,
Majira na New Habari huko kote
hakuitwa mchochezi wala
hakukamatwa.
“Nape alikuwa mmoja wa
waandishi na vyanzo vya taarifa
za MwanaHALISI kipindi hana
madaraka CCM, mbona
alishirikiana na sisi kuibua
maovu kama sisi ni
wachochezi?” alihoji Kubenea.
Jabir na Mkina wamekuwa
wakitafutwa na jeshi la polisi
kwa siku tatu mfululizo tangu
Jumamosi kwa tuhuma za
uchochezi huku jaribio la
kuwakamata likishindikana mara
kwa mara kutokana na kutojua
walipo mpaka walipoamua
kujisalimisha jana.
Mbali ya Kubenea na Kibanda,
walisindikizwa pia na Mhariri
Mtendaji wa gazeti la
MwanaHALISI, Ansbert Ngurumo
pamoja na wakili wao, Fredrick
Kihwelo.
Kubenea ana "ubavu"gani wa kumpa onyo Nape?(sio ubavu wa mieleka),au kiongozi ulitaka kuandika kinyume chake ukapitiwa?
 
Uandishi wap kama global publisher

Hawana nidhamu

Tena wasiishie kulifungia tu walizike futi 20 chini ya ardhi
 
Napinga Mawio kufungiwa
lakini naamini Mawio wana upungufu mkubwa wa maadili

Kubenea ni vizuri akajitazama na kujitathimini
ana make headlines for all the wrong reasons....

Mara vyeti vyake vimefanyaje
mara Zitto waparurane
mara yuko katikati ya uchaguzi wa Meya
mara hili.....

wapiga kura wake wanamtazama tu....wasije kumchoka so fast
I second you 100%. Kubenea anatakiwa kujitathmin kama bado ni mwanaharakati au mwanasiasa kwani yeye kwa sasa hivi ndo amekua ndo headline ya mambo mengi yenye utata
 
Ni wakati wa Kubenea kujikita kwenye ubunge kuwakilisha wapiga kura wake waliomchagua kwenda bungeni


It is high time Kubenea started chosing his battles otherwise he will burn out!! He has to be strategic by chosing the battles he can win so that he makes headlines for the right reasons!
 
Kusema ukweli tukiacha unazi wa uchama na kiupinzani...gazeti la MAWIO lilikuwa likiandika habari zake kinyume na maadili ya kiundishi...ingawa sikubaliani na suala kufungiwa kwake lilipaswa kupewa onyo tu....
Onyo wamepewa hawasikii na wanajiona wana uhuru kuliko watu wengine. Haiwezekani ukawa na uhuru bila kiwa na wajibu. Ati wanajiita sauti ya wananchi nashangaa wananchi gani hao kila kunapokucha matusi tu?
 
HUYO KUBENEA NAYE BADALA YA KUTATUA TATIZO LA MAJI UBUNGO ANAMTISHIA WAZIRI NAPE!
 
Serikali hii ya Tanzania inavunja record dunia nzima kwa kutaka kusifiwa tuu na vyombo vya habari!viongozi wengi ambao sio waadilifu hawataki vyombo vya habari vifichue maovu yao,hivi tutafika kweli?mbona inchi zingine hazifanyi ivyo?yani kiongozi anataka aibe mali za watanzania mwandishi akimfichua anapelekwa mahakamani?hivi wapo kwa ajili ya kusifia tuu serikali?kwa staili hii hatutakomesha ufisadi ndani ya inchi hii,ndio maana wanaichi wanawajua wahalifu wanaogopa kutoa taarifa police kwa kuwa wanaweza kamatwa na wao wakaambiwa wachochezi!Ila sishangai huenda ikawa ndio agenda kuu ya serikali kufungia vyombo vya habari vinavyosifia upinzani!
Mkuu acha unazi.....mawio siyo gazeti objective kukosoa serikali. Limekosa maadili ya uandishi wa habari. Ban ndo haki yake
 
Mkurugenzi wa Kampuni ya Hali
Halisi Publishers, Saed Kubenea
pamoja na Mwenyekiti wa
Jukwaa la Wahariri Tanzania
(TEF) Absalom Kibanda
wameionya serikali juu ya
uamuzi wa kulifuta gazeti la
MAWIO uliochukuliwa hivi
karibuni.
Kupitia tangazo la serikali lenye
notisi namba 55, serikali
ilichukua uamuzi wa kulifungia
MAWIO, Januari 15, 2016 huku
Waziri wa Habari, Utamaduni,
Sanaa na Michezo, Nape Nnauye
akisema gazeti hilo limekuwa
‘sugu’ kwa uchochezi tangu
2013.
Kubenea na Kibanda walikuwa
katika kituo cha Polisi cha Kati
ambapo ndiyo Makao Makuu ya
Kanda Maalum ya Dar es Salaam
wakiwasindikiza wahariri Jabir
Idrissa na Simon Mkina
walioitikia wito wa uliotolewa na
jeshi hilo siku tatu zilizopita.
Kibanda amewambia
wanahabari kuwa kitendo cha
jeshi la polisi kuwasaka ili
kuwakamata Jabir na Mkina
ambao ni wahariri ili kuwahoji
huku gazeti la MAWIO likiwa
limefungiwa, kinalenga
kuwatisha waandishi wa habari
nchini na kuzima uhuru wa
habari.
Ameulezea uamuzi huo wa
Waziri mwenye dhamana ya
masuala ya Habari, Nape, kama
uamuzi uliolishitua TEF na
wamewasiliana naye wakielezea
mshituko na masikitiko yao.
“Hatuwezi kuvumilia kufungiwa
kwa vyombo vya habari,
kukamatwa na kunyanyaswa
kwa waandishi, miaka miwili
iliyopita nilitakiwa kujisalimisha
makao makuu ya polisi,
nikafikishwa mahakamani na
nikashinda kesi, naelewa
maumivu ya mapambano haya,”
ameeleza Kibanda.
Kwa upande wake Kubenea,
amesema Serikali kupitia Nape
imechukua uamuzi wa kikatili
dhidi ya gazeti la MAWIO ili
kuzima sauti ya wananchi kwa
hoja zisizo na mashiko ikiwemo
ile ya uchochezi ambayo
imekuwa kisingizio cha
watawala kwa muda mrefu.
“Katika toleo la MAWIO lilimnukuu
Maalim Seif akijitangaza mshindi,
yeye hakuitwa mchochezi, Jecha
amefuta uchaguzi wakati hana
mamlaka ya kisheria wala ya
kikatiba hakuitwa mchochezi ila
gazeti kuandika ushindi
uliotangazwa na Seif
limefungiwa,” ameeleza Kubenea.
Kubenea ameongeza kuwa,
ubovu wa sheria ya magazeti ya
mwaka 1976 umekuwa
ukitumiwa na serikali kuviadhibu
vyombo vya habari vinavyofichua
maovu, huku mahakama
ikithibitisha mara kadhaa kuwa
madai ya uchochezi
yanayotolewa na serikali hayana
mashiko.
“Jabir ni Mwandishi aliyebobea
kitaaluma na uzoefu, ameandikia
magazeti ya Uhuru, Mzalendo,
Majira na New Habari huko kote
hakuitwa mchochezi wala
hakukamatwa.
“Nape alikuwa mmoja wa
waandishi na vyanzo vya taarifa
za MwanaHALISI kipindi hana
madaraka CCM, mbona
alishirikiana na sisi kuibua
maovu kama sisi ni
wachochezi?” alihoji Kubenea.
Jabir na Mkina wamekuwa
wakitafutwa na jeshi la polisi
kwa siku tatu mfululizo tangu
Jumamosi kwa tuhuma za
uchochezi huku jaribio la
kuwakamata likishindikana mara
kwa mara kutokana na kutojua
walipo mpaka walipoamua
kujisalimisha jana.
Mbali ya Kubenea na Kibanda,
walisindikizwa pia na Mhariri
Mtendaji wa gazeti la
MwanaHALISI, Ansbert Ngurumo
pamoja na wakili wao, Fredrick
Kihwelo.
kubenea anatak kuogelea kwenye maji ya mkondo wa MTO nungwi wakati uwezo wake ni kwenye kabeseni tu. UBUNGO WAMEPATA MBUNGE MZIGO KULIKO MAJIMBO YOTE TANZANIA.
 
Back
Top Bottom