Kubemendwa: Hiki kitu kweli kipo?

Kubemendwa: Hiki kitu kweli kipo?

Malila

JF-Expert Member
Joined
Dec 22, 2007
Posts
5,372
Reaction score
5,124
Kule uswahilini mara nyingi ndiko kunakosikika hili neno,naomba kuuliza, jambo lenyewe ni kubemenda mtoto. Sijawahi kuona mtoto aliyebemendwa. Hivi ni kweli kitu hicho kipo? na kinasababishwa na nini hasa? Kwa anayejua tafadhali mwaga hapa.
 
kubemenda mtoto ni ile hali ya kufanya mapenzi na mama mjamzito aliyekaribu kujifungua say miezi 7.5 hadi 9, na kutoa mbegu za kiume ambazo huweza kumwathiri mtoto tumboni
mara nyingi mtoto aliyebemendwa anakua na mabaka mwilini meusi hivi, mara nyingi tumboni, kwenye mbavu au sehemu za mikono(watoto nilio wahi kuwaona)
 
kubemenda mtoto ni ile hali ya kufanya mapenzi na mama mjamzito aliyekaribu kujifungua say miezi 7.5 hadi 9, na kutoa mbegu za kiume ambazo huweza kumwathiri mtoto tumboni
mara nyingi mtoto aliyebemendwa anakua na mabaka mwilini meusi hivi, mara nyingi tumboni, kwenye mbavu au sehemu za mikono(watoto nilio wahi kuwaona)

George_Porjie, Mimi nilidhani kummbemenda mtoto kunatoka na mama kufanya mapezi wakati akiwa na mtoto mchanga, kumbe nilikuwa na tafasiri isiyo sahii, Asante mkuu.
 
kubemenda mtoto ni ile hali ya kufanya mapenzi na mama mjamzito aliyekaribu kujifungua say miezi 7.5 hadi 9, na kutoa mbegu za kiume ambazo huweza kumwathiri mtoto tumboni
mara nyingi mtoto aliyebemendwa anakua na mabaka mwilini meusi hivi, mara nyingi tumboni, kwenye mbavu au sehemu za mikono(watoto nilio wahi kuwaona)

Are you SURE???

nimesoma kwamba mwanamke mjamzito anashauriwa afanye mapenzi ili njia ya uzazi iweze kupanuka na iwe tayari kwa mtoto kupita!!! Sasa unaposema hii ndo kubemenda then i think most or all the children have been bemendwad!!!

Ni hatari... any one with relevant info wasaidie wazazi
 
Last edited:
George_Porjie, Mimi nilidhani kummbemenda mtoto kunatoka na mama kufanya mapezi wakati akiwa na mtoto mchanga, kumbe nilikuwa na tafasiri isiyo sahii, Asante mkuu.

George_Porjie you are wrong, The farmer you half correct:

Kubemeda mtoto ni matokeo ya Mama na Baba wenye kichanga kufanya zinaa (kutembea nje ya ndoa yao) wakati kichanga kile bado kinanyonyeshwa. Hii dhana kwa tafsiri ya kisasa maana yake ni "malnutrition".

Endapo Mama ataendekeza ebeneke wakati anayonyesha most likely lishe kwa mtoto itapungua sana and equally endapo Baba ataendekeza "nyumba ndogo" kipindi hicho Mama atakuwa stressed na hataweza kumpatia mtoto lishe ya kufaa (esp kama anamnyonyesha unakuta hata maziwa hayatoki ifaavyo).

Kubemenda = Kwashakoo

Weekend Njema
 
Kubemenda mtoto ni ile hali ya mama akiwa ananyonyesha mtoto alafu kitoto bado kidogo anapigwa mimba ingine basi mtoto hapo unambemenda.
 
George_Porjie you are wrong, The farmer you half correct:

Kubemeda mtoto ni matokeo ya Mama na Baba wenye kichanga kufanya zinaa (kutembea nje ya ndoa yao) wakati kichanga kile bado kinanyonyeshwa. Hii dhana kwa tafsiri ya kisasa maana yake ni "malnutrition".

Endapo Mama ataendekeza ebeneke wakati anayonyesha most likely lishe kwa mtoto itapungua sana and equally endapo Baba ataendekeza "nyumba ndogo" kipindi hicho Mama atakuwa stressed na hataweza kumpatia mtoto lishe ya kufaa (esp kama anamnyonyesha unakuta hata maziwa hayatoki ifaavyo).

Kubemenda = Kwashakoo


Weekend Njema

Baba enock you are almost true.

Kwa kuongezea tu ni kwamba kubemenda si tu kutembea nje ya ndoa kwa wazazi wote wawili;unaambiwa kwamba utamubemenda mtoto endapo utafanya mapenzi aidha ndani ya ndoa au nje ya ndoa halafu bila hata kufanya usafi toshelezo ukaamua kwenda kumshika mtoto au kumnyonyesha mtoto na shombo za majasho basi atakuwa affected hna hiyo malnutrition.

Hivyo si kwamba lazma uende au utoke nje ya ndoa ila hata ndani inaweza kutokea kama hakuna usafi mara tu mmalizapo shughuli zenu.

Unashauriwa mnapomalizo shughuli zenu unashauriwa kuwa msafi kabla hata kumnyonyesha mtoto kwa mama na kwa baba kumshika au kumbeba mtoto.
 
Bonge la somo leo,sasa hapa kipi ni kipi, usafi,uzinzi,lishe(malnutrition), mimba kabla ya muda kwa mtoto aliyetangulia,hata hivyo bado naomba tuendelee kukata issue. leo mmenifumbua macho.
 
nadhani kubemenda ni mtoto kukosa matunzo na afya kudorora,haijalishi utoke au uingie katka ndoa
 
George_Porjie you are wrong, The farmer you half correct:

Kubemeda mtoto ni matokeo ya Mama na Baba wenye kichanga kufanya zinaa (kutembea nje ya ndoa yao) wakati kichanga kile bado kinanyonyeshwa. Hii dhana kwa tafsiri ya kisasa maana yake ni "malnutrition".

Endapo Mama ataendekeza ebeneke wakati anayonyesha most likely lishe kwa mtoto itapungua sana and equally endapo Baba ataendekeza "nyumba ndogo" kipindi hicho Mama atakuwa stressed na hataweza kumpatia mtoto lishe ya kufaa (esp kama anamnyonyesha unakuta hata maziwa hayatoki ifaavyo).

Kubemenda = Kwashakoo

Weekend Njema

Kubemendwa sio malnutrition. Wala havina uhusiano. Mtoto anaweza akawa anapata chakula vizuri kabisa na bado akabemendwa. Kwangu mimi na ambavyo nafahamu ni ile hali ya mama kufanya mapenzi na kumnyonyesha mtoto baada ya muda usio mrefu. Inakuwaje. Mama anayenyonyesha anapofanya mapenzi (katika hali ya kawaida, yaani staili ya kifo cha mende) kutakuwa na msuguano kati ya mwili wake (na hasa sehemu za matiti) na ule wa mwanaume. Msuguano huo utasababisha joto la maziwa ndani ya matiti kuongezeka (kwa lugha nyingine maziwa hayo yanakatika, yanakuwa hayako katika hali ya kawaida ya utulivu). Sasa kabla maziwa hayo ndani ya matiti hayajakaa sawa, mtoto akanyonyeshwa, lazima ataharisha, tena ataharisha maziwamaziwa. Kitendo cha kuharisha maziwamaziwa hivi ndio kinaitwa kubememdwa. Kwa hiyo inawezekana kabisa baba na mama ndani ya ndoa wakambemenda mtoto.
 
George_Porjie you are wrong, The farmer you half correct:

Kubemeda mtoto ni matokeo ya Mama na Baba wenye kichanga kufanya zinaa (kutembea nje ya ndoa yao) wakati kichanga kile bado kinanyonyeshwa. Hii dhana kwa tafsiri ya kisasa maana yake ni "malnutrition".

Endapo Mama ataendekeza ebeneke wakati anayonyesha most likely lishe kwa mtoto itapungua sana and equally endapo Baba ataendekeza "nyumba ndogo" kipindi hicho Mama atakuwa stressed na hataweza kumpatia mtoto lishe ya kufaa (esp kama anamnyonyesha unakuta hata maziwa hayatoki ifaavyo).

Kubemenda = Kwashakoo

Weekend Njema

Very correct and insightful. Ni maneno yenye tafsida. Kwa wengine hupitishwa kizazi na kizazi bila kujua maana. One has to think outside the box sometimes
 
kubemenda mtoto ni ile hali ya kufanya mapenzi na mama mjamzito aliyekaribu kujifungua say miezi 7.5 hadi 9, na kutoa mbegu za kiume ambazo huweza kumwathiri mtoto tumboni
mara nyingi mtoto aliyebemendwa anakua na mabaka mwilini meusi hivi, mara nyingi tumboni, kwenye mbavu au sehemu za mikono(watoto nilio wahi kuwaona)

Mtoto akiwa tumboni anakuwa yuko ndani ya kifuko, mbegu zinaingia ingiaje tena na kumwathiri?! Uliyoyasema kuhusu mtoto kuwa na mabaka mabaka, sidhani kama sababu ndiyo hiyo, sidhani. In fact uliyoyasema mimi naona ni aina mojawapo ya mwendelezo wa imani zilizokuwa unfounded zenye lengo la kunyanyapaa baadhi ya watu (wenye mabakamabaka). Kwani naamini kuna jambo lingine kabisa tofauti na hiyo sababu uliyotoa inayosababisha hayo mabakamabaka.
 
Jf, the home of great thinker? Hii inatia shaka kwa majibu hapo juu. Waliogusia malnutrition na malezi hafifu wako right, walioongelea ngono , hizo ni misconception. Nimefanya thesis kwa hii kitu. Mwanzo wa neno ni pwani, ni inatokana na malezi hafifu ya kimlo kwa mtoto baada ya kuingiliwa na mapenzi mapya au stress kwa mlezi wa mtoto.
Haina tofauti na maana ya kwashiorkor, ambayo mwanzo wake ni ghana, ikiwa na maana ya mtoto aliyetelekezwa baada ya mama kupata mtoto mwingine kabla ya aliyefuatishwa kukua, au kuweza kutokuwa tegemezi. Ingieni google wakubwa.
IELEWEKE KUWA KUFANYA MAPENZI NA MAMA MJAMZITO, HAKUNA UHUSIANO NA MTOTO ATAKAYE ZALIWA KAMA YAI LILISHATIWA KIINI CHA KIUME. MADHARA PEKEE NI KAMA MAMA ANACERVICAL INCOPETENCE[SHINGO YA KIZAZI ILIYOLEGEA] . JF HII IWE MADA MAALUMU TUWATOE WATU MITONGOTONGO.
 
Jf, the home of great thinker? Hii inatia shaka kwa majibu hapo juu. Waliogusia malnutrition na malezi hafifu wako right, walioongelea ngono , hizo ni misconception. Nimefanya thesis kwa hii kitu. Mwanzo wa neno ni pwani, ni inatokana na malezi hafifu ya kimlo kwa mtoto baada ya kuingiliwa na mapenzi mapya au stress kwa mlezi wa mtoto.
Haina tofauti na maana ya kwashiorkor, ambayo mwanzo wake ni ghana, ikiwa na maana ya mtoto aliyetelekezwa baada ya mama kupata mtoto mwingine kabla ya aliyefuatishwa kukua, au kuweza kutokuwa tegemezi. Ingieni google wakubwa.
IELEWEKE KUWA KUFANYA MAPENZI NA MAMA MJAMZITO, HAKUNA UHUSIANO NA MTOTO ATAKAYE ZALIWA KAMA YAI LILISHATIWA KIINI CHA KIUME. MADHARA PEKEE NI KAMA MAMA ANACERVICAL INCOPETENCE[SHINGO YA KIZAZI ILIYOLEGEA] . JF HII IWE MADA MAALUMU TUWATOE WATU MITONGOTONGO.

asante mkuu kwa mchango wako,ngono na ukuaji wa mtoto anayepata lishe ya nguvu uhusiano uko wapi hapo.
Mkuu leta nyingine,ili tukiunganisha na wenzetu tunapata jibu safi.
 
Kubemendwa sio malnutrition. Wala havina uhusiano. Mtoto anaweza akawa anapata chakula vizuri kabisa na bado akabemendwa. Kwangu mimi na ambavyo nafahamu ni ile hali ya mama kufanya mapenzi na kumnyonyesha mtoto baada ya muda usio mrefu. Inakuwaje. Mama anayenyonyesha anapofanya mapenzi (katika hali ya kawaida, yaani staili ya kifo cha mende) kutakuwa na msuguano kati ya mwili wake (na hasa sehemu za matiti) na ule wa mwanaume. Msuguano huo utasababisha joto la maziwa ndani ya matiti kuongezeka (kwa lugha nyingine maziwa hayo yanakatika, yanakuwa hayako katika hali ya kawaida ya utulivu). Sasa kabla maziwa hayo ndani ya matiti hayajakaa sawa, mtoto akanyonyeshwa, lazima ataharisha, tena ataharisha maziwamaziwa. Kitendo cha kuharisha maziwamaziwa hivi ndio kinaitwa kubememdwa. Kwa hiyo inawezekana kabisa baba na mama ndani ya ndoa wakambemenda mtoto.

sahihi kabisa congo, ningependa kuongezea

mama ambaye ananyonyesha akishamaliza kufanya mapenzi anatakiwa ayakamue yale maziwa machafu (maziwa yanayokatika) mpaka maziwa masafi yaanze kutoka, alafu aoge(au ajikoshe sehemu za matiti na kifuani) kabla ya kumnyonyesha mwanawe.
mama akiweza kufanya hivi hambemendi mtoto hata siku moja na kama hawezi kufanya hivi ni bora amwenyeshe mtoto wake maziwa ya chupa
 
Last edited:
...kwa jinsi mlivyoelezea naona Fidel80 pekee ndiye yupo 'njia' sahihi.

Kubemenda mtoto ni ile hali ya mama akiwa ananyonyesha mtoto alafu kitoto bado kidogo anapigwa mimba ingine basi mtoto hapo unambemenda.

...kichanga kinahitaji sana maziwa ya mama hususan kutokana na lishe bora yatokanayo na maziwa hayo na psychological bonding.
 
Lakini mbona mambo haya yapo zaidi uswahilini? Siyasikii sana maeneo mengine!
 
sijui maana halisi ya mnachokiengelea,lakini bado napata wakati mgumu kuelewa hizo 'imani' za wengi.maana naona maelezo mengi hayaelezei ukweli.
mmh ngoja tusubiri tuone wengine watasemaje huenda ukweli ukaja baadaye.
 
Jamani mimi ni mgumu kuamini mambo mengine. Ukweli hapa inabidi kutenganisha athari za kiafya na zile za kiimani potofu. Kwa mfano sitetei mzazi kutoka nje, lakini hii haimanishi kumuathiri mtoto, ila kama hiyo itapunguza matunzom kwa mtoto ndiyo inaathiri.
Mtu anaweza asitoke nje ya ndoa na asimtunze mtoto. Japo ukweli ni kwamba kutoka nje ya ndoa mara nyingi(sio mara zote) huathiri ku-care familia.
 
Back
Top Bottom