Kubadili majina baada ya kuolewa

Kubadili majina baada ya kuolewa

Zamani akina baba walikuwa wameenda shule wakati wakina mama walikua shule ndogo, ndio maana waliona fahari kuitwa mrs fulani, hata familia ya mwanamke walikuwa wanaona fahari mtoto wao kutumia jina mrs fulani tu kwasababu labda mwanaume ana pesa au cheo nk.

Tofauti na siku hzi, wanawake wanaenda shule sambamba na wanaume, kweli mwanaume kanikuta nipo kazini nianze kuangaika kubadili jina, khaa!!! Natafuta tuzo???

Mahaba sio kwenye jina hata.

Dida shaibu
dida wa juma
dida wa yahaya
dida wa hamisi
dida wa edzen
hivi sahivi anaitwa dida wa nani?make hizo zote ni ndoa zake
 
Its optional mama,...Amua wewe mwenyewe. Na wala si dhambi kutobadili au kubadili.
 
Kuonyesha heshima kwa umpendae ni vema ukabadili.. hiyo ndio tamaduni zetu!!! mambo ya kufikiri mkiachana itakuaje sio wakati wake, we don't live expecting the worse

Teh teh..Hope for the best,prepare for the worst..
 
Zamani akina baba walikuwa wameenda shule wakati wakina mama walikua shule ndogo, ndio maana waliona fahari kuitwa mrs fulani, hata familia ya mwanamke walikuwa wanaona fahari mtoto wao kutumia jina mrs fulani tu kwasababu labda mwanaume ana pesa au cheo nk.

Tofauti na siku hzi, wanawake wanaenda shule sambamba na wanaume, kweli mwanaume kanikuta nipo kazini nianze kuangaika kubadili jina, khaa!!! Natafuta tuzo???

Mahaba sio kwenye jina hata.

Hii haikuwa sababu ya wanawake kubadili jina,sababu ipo na ina maana yake kabisa japokuwa inaweza kuea sio lazima kubadili pia....
 
Hii haikuwa sababu ya wanawake kubadili jina,sababu ipo na ina maana yake kabisa japokuwa inaweza kuea sio lazima kubadili pia....

Lakini mtu abadili jina ukubwani jamani!! Utaniambia sababu
 
Kubadili jina ni utumwa. Na hii ilifanyika sana sana zamani hasa kwa waliokuwa wameolewa na wanaume wafanyakazi kwa lengo la kupata haki za mumeo kazini kama matibabu, uhamisho n.k. Lakini iliwatesa sana pale unapoachika au kufiwa. Inatesa kisaikolojia pia kutumia jina na ukoo usio wako. Inatesa pale mwanamume anapokuwa sio mwaminifu katika ndoa.

Usibadili jina lako.
 
Lakini mtu abadili jina ukubwani jamani!! Utaniambia sababu

Unabadili kuomesha tofauti ya Status na kuonesha "unamilikiwa" na pia huleta heshima fulani hivi...

Hii haina mahusiani na kubadili dokomenti zako za zamani kama vyeti vya shule,kiwanja n.k...
 
Unabadili kuomesha tofauti ya Status na kuonesha "unamilikiwa" na pia huleta heshima fulani hivi...

Hii haina mahusiani na kubadili dokomenti zako za zamani kama vyeti vya shule,kiwanja n.k...

Nimekuelewa mpenzi.
 
Kubadili jina ni utumwa. Na hii ilifanyika sana sana zamani hasa kwa waliokuwa wameolewa na wanaume wafanyakazi kwa lengo la kupata haki za mumeo kazini kama matibabu, uhamisho n.k. Lakini iliwatesa sana pale unapoachika au kufiwa. Inatesa kisaikolojia pia kutumia jina na ukoo usio wako. Inatesa pale mwanamume anapokuwa sio mwaminifu katika ndoa.

Usibadili jina lako.
Kama inakuwa rahisi kubadili wakati akiolewa kwa nini iwe ngumu kubadili wakiachana? Mimi naona labda mtu kama hutaki usumbufu wa nenda rudi mahakamani kubadili....lakini vyoyote vile ni process rahisi tu.
 
Back
Top Bottom