Kubadili majina baada ya kuolewa

Kubadili majina baada ya kuolewa

Habari zenu wakuu,

Natamani kufanya hivyo baada ya harusi yangu na mr right wangu. Mama yangu alibadili majina baada ya kuolewa na baba na mpaka sasa bado anatumia majina ya baba.

Pia nimechunguza sana mama zetu wengi wanaitwa kwa majina ya waume wao mfano regina lowasa, Salma Kikwete na wengineo.Naona kama ni heshima sana kwa mume but sijajua madhara ya kufanya hivyo. Pia wazazi sijui watamind mimi kufanya hivyo.

Naombeni busara zenu wandugu.

Matusi hayaruhusiwi please.

Asanteni

Mambo ya kawaida huku kwetu. Inakuwa rahisi kurithi mali ya mumeo endapo atatangulia.
 
Teh sent ni la baba bana. Nikiolewa sehemu ambazo sitahitajika kutumia documents zangu kama vyeti na hati basi ntakuwa na extend jina la mzee... Mrs De Souz, kuonesha kuwa now nimeunganishwa na mtu mwingine. Lakini itakapohitajika kutumia any of my documents , ntaacha tu heaven sent jamani. Ila if my hubby akipendelea zaidi nibadili, basi I won't object ( I belong to my husband's clan now, ndo maana hata nikifa, ntazikwa kwao)

Me nafikiri ni uamuzi wenu nyie wanandoa kuwa mke abadili jina or not. Mkiona abadili sawa, Mkiona asibadili ni sawa pia... Yani ni choice yenu tu as long as hamtoanza kugombana kisa majina

Ila Sidhani kama inadhuru kitu chochote ukibadili jina unless jina la mke ni trademark yake mfano "ritha paulsen" akiolewa na paulo then kuitwa ritha paulo itamuharibia biashara zake. Naona kuextend jina la mumeo iko poa zaidi kwangu.

Smart lady. You should have my babies, you know?! Let's go make 'em.

Hapo kwa mfano wa RP inawezekana kuongeza jina pia. Kama Mrs. Beyonce Knowles Carter.
 
Wajuzi wa mambo twasema maza hakua na mahaba kwa mzee madiba ndo maana hakuchange jina

Graca Machel alikuwa mke wa rais wa Mozambique, Samora Machel. Aliolewa na Madiba baada ya mumewe kufariki.
 
Smart lady. You should have my babies, you know?! Let's go make 'em.

Hapo kwa mfano wa RP inawezekana kuongeza jina pia. Kama Mrs. Beyonce Knowles Carter.
Hahaha nani kakutuma uedit jina langu la mrs. Hapo kwa RP niliongelea tu if akiamua kubadili jina lake totally. Honestly inakuwa poa zaidi kwangu nikiliongezea to Mrs heaven sent ikemefuna lol....as jina langu la ukoo na la mume yatakuwepo yote. So sijapoteza identity yangu as wengi hawataki kupoteza ID zao.
 
Kama unaona ina faida kwako au utaadd chochote badili tu

Binafsi naona ubadili au usibadili wewe ni mkewe na utaendelea kuwa mkewe untill further notice...
 
Zamani akina baba walikuwa wameenda shule wakati wakina mama walikua shule ndogo, ndio maana waliona fahari kuitwa mrs fulani, hata familia ya mwanamke walikuwa wanaona fahari mtoto wao kutumia jina mrs fulani tu kwasababu labda mwanaume ana pesa au cheo nk.

Tofauti na siku hzi, wanawake wanaenda shule sambamba na wanaume, kweli mwanaume kanikuta nipo kazini nianze kuangaika kubadili jina, khaa!!! Natafuta tuzo???

Mahaba sio kwenye jina hata.

Hahahahahha
 
Nani kasema anataka maana ya mahari kwenye Uislam?

Hiyo fasiri ya mahari ya kwenye Uislam inatumiwa na kila mtu?

Hivi akija mpagani anataka umme fasiri ya mahari kwa mujibu wa serikali utampa hayo makabrasha ya Uislam?

Hehehe
 
Zamani akina baba walikuwa wameenda shule wakati wakina mama walikua shule ndogo, ndio maana waliona fahari kuitwa mrs fulani, hata familia ya mwanamke walikuwa wanaona fahari mtoto wao kutumia jina mrs fulani tu kwasababu labda mwanaume ana pesa au cheo nk.

Tofauti na siku hzi, wanawake wanaenda shule sambamba na wanaume, kweli mwanaume kanikuta nipo kazini nianze kuangaika kubadili jina, khaa!!! Natafuta tuzo???

Mahaba sio kwenye jina hata.

Asipokukuta uko kazini uko tayari kubadili?
 
yeah ndo hiko hivyo... ila kwa kizazi cha wanawake wasomi wataona ni uonevu na hawastahiri kufanya hivyo!!! sometimes education ruins us

Hakuna usomi hapo, kwani michele obama hakusoma,au laura bush hakusoma au hillaryclinton?
 
Pia Imelda Mwamanga Mtunga.

But huu utamaduni wa kutumia jina la mume kwa mwanamke alieolewa ni wa kimagharibi zaidi. Hasa ni utamaduni wa kikristo.

Wachagga kiasili kwa mfano, mwanamke alikoolewa wanaendelea kumuita jina la wanawake wa ukoo alikotokea. Hawatumii la ukoo wa mume katu.

Kuhusu kuachika, kwa wazungu baada ya talaka mwanamke akiolewa tena angeongezea jina la mume mpya mbele ya la wazamani!

Kwa sasa wanawake wengi hupenda kutumia yote. La ukoo wake na la mume. Kale mwanamke angetumia la Baba yake then la mume.
 
Hivi nilivyo ni kwa sababu ya baba yangu, kubadili jina ni kama kumsaliti. As a tribute to him, i will never change my name.
 
Ngoja nimuulize Atoto Atakubali Kuitwa Mrs Ibrah Ama?
 
Smart lady. You should have my babies, you know?! Let's go make 'em.

Hapo kwa mfano wa RP inawezekana kuongeza jina pia. Kama Mrs. Beyonce Knowles Carter.
Namkubali Sana Heaven Sent Yaani mpaka naishiwa hata la kuongea... kama utampata basi nakuomba umtunze na Kuutendea haki moyo wake na hisia zake, Ukimshindwa nijulishe
 
Ubinafsi ndo wafanya akina fulani wasitake itwa majina ya waume zao......
 
Namkubali Sana Heaven Sent Yaani mpaka naishiwa hata la kuongea... kama utampata basi nakuomba umtunze na Kuutendea haki moyo wake na hisia zake, Ukimshindwa nijulishe

Haha. atoto umemwacha? Ila kama unamkubali Heaven Sent kiasi hicho, fanya mambo tu mzee. May the best man win, patner.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom