Its Pancho
JF-Expert Member
- Sep 21, 2018
- 14,238
- 22,643
Wandugu,
Hii team kwa kweli inatia huruma sana. Kwa sasa sio Simba ile ya kushtua, Simba amekuwa MBUZI. Hata ushindi wenyewe wanapata kwa kuokoteza, team haina morali, pesa, udhamini mbovu, uchawi sasa wnatoboaje kwa mfano?
Yule CEO ndiye chanzo cha yote haya lakini kaamua mwakani akimbie, yaani kavua nguo hataki kuoga!
Timu ina matatizo mengi;
~Uchawi- walimtuma gadiel matokeo yake kafungiwa.
~ Njaa- kwa sasa wachezaji hawapati mshahara kwa wakati tajiri naye kasusa mpaka wakapige magoti kwake.. Na wasilalamike kwake ndio anataka.
~ Usafiri- timu kubwa inatembelea Costa utadhani daladala la manzese. Poor poor.
~ Udhamini- walikataa udhamini na sportpesa sababu dau dogo walilopewa kuliko yanga, hawakujua kuwa yanga ni kubwa sasa Africa mashariki hapa matokeo yake wanadunduliza na mkataba wa kubumba wa mbet.
~ Utawala mbovu/uongozi- CEO na wenzie hawana tofauti na walevi wa wanzuki kilabuni, wanaamua mambo kwa mihemko sana na kukurupuka matokeo yake team haiendi mjini.
Wakaleta kocha wa kuunga unga mtoto wa town mgunda kwa kigezo cha kuwa wazalendo, si wangesema ukweli kuwa hawana pesa Basi?
Kwa mujibu wa takwimu Yanga ndiyo iliyofatilwa zaidi mitandaoni hapa Africa imeshika nafasi ya pill huku Simba ikikamata ya tatu..
Hii ni taa nyekundu kwa Simba kuwa sasa Yanga inakwenda kuwaacha mbali. Ni muda wa simba kushindana na kina Mtibwa na Prison.
Hii team kwa kweli inatia huruma sana. Kwa sasa sio Simba ile ya kushtua, Simba amekuwa MBUZI. Hata ushindi wenyewe wanapata kwa kuokoteza, team haina morali, pesa, udhamini mbovu, uchawi sasa wnatoboaje kwa mfano?
Yule CEO ndiye chanzo cha yote haya lakini kaamua mwakani akimbie, yaani kavua nguo hataki kuoga!
Timu ina matatizo mengi;
~Uchawi- walimtuma gadiel matokeo yake kafungiwa.
~ Njaa- kwa sasa wachezaji hawapati mshahara kwa wakati tajiri naye kasusa mpaka wakapige magoti kwake.. Na wasilalamike kwake ndio anataka.
~ Usafiri- timu kubwa inatembelea Costa utadhani daladala la manzese. Poor poor.
~ Udhamini- walikataa udhamini na sportpesa sababu dau dogo walilopewa kuliko yanga, hawakujua kuwa yanga ni kubwa sasa Africa mashariki hapa matokeo yake wanadunduliza na mkataba wa kubumba wa mbet.
~ Utawala mbovu/uongozi- CEO na wenzie hawana tofauti na walevi wa wanzuki kilabuni, wanaamua mambo kwa mihemko sana na kukurupuka matokeo yake team haiendi mjini.
Wakaleta kocha wa kuunga unga mtoto wa town mgunda kwa kigezo cha kuwa wazalendo, si wangesema ukweli kuwa hawana pesa Basi?
Kwa mujibu wa takwimu Yanga ndiyo iliyofatilwa zaidi mitandaoni hapa Africa imeshika nafasi ya pill huku Simba ikikamata ya tatu..
Hii ni taa nyekundu kwa Simba kuwa sasa Yanga inakwenda kuwaacha mbali. Ni muda wa simba kushindana na kina Mtibwa na Prison.