Kuanzia leo nasimamisha !

Kuanzia leo nasimamisha !

Judgement

JF-Expert Member
Joined
Nov 13, 2011
Posts
10,326
Reaction score
4,787
Baasi nimechoka , imetosha nasimamisha research hii kuanzia leo .

Mwaka juzi nikiwa maskani na washirika wangu wa karibu , palitokea ubishi mkubwa baina yetu .
Mada ilikua ni kuwahusu ndugu zetu wa jamii ya Kimasai , ambao miongo ya karibuni walichapuka kuhamia mijini kwa shughuli zao kuu za Ulinzi , Ususi na Madawajadi .

Issue ilikua , mbona hawa jamaa ni wengi na tumechanganyikana nao jamiini , lakini hakuna baina yetu aliyewahishuhudia kwa macho Masai wanaenda kumzika Masai mwenzao .

Ndipo mie nilipo weka nadhiri ya kulitafiti hilo , huu leo umegota mwaka wa 3 utafiti wangu haujapata chanya!
Zaidi nilichoambua ni negative results.
Sijafanikiwa ktk utafiti wangu kupata jibu .
Wagonjwa wa kimasai nimeshawaona ! Jeneza la Masai nimechemka kuliona .
Baas leo nasimamisha rasmi utafiti .
Staki tena .
 
Mkuu nimeshawahi kushuhudi vifo kadhaa vya wamasai.

Huwa ndugu yao akifa wanamkabidhi kwa wahuni wa kijiweni wakamzike...
 
Kiukweli sijawah kushuhudia jeneza au masai kwenda kuzika masai mwenzake.au wao hawafi?au labda kwakua jamii inahusishwa na jamii fulani?
 
Mkuu nimeshawahi kushuhudi vifo kadhaa vya wamasai.

Huwa ndugu yao akifa wanamkabidhi kwa wahuni wa kijiweni wakamzike...

Ndiyo kusema wanawalipa wahuni husika cost za burial au? Na huko makwao pasipokua na wahuni wanazikiwa na ?
 
Kiukweli sijawah kushuhudia jeneza au masai kwenda kuzika masai mwenzake.au wao hawafi?au labda kwakua jamii inahusishwa na jamii fulani?

Bora nimepata mwenzangu !
 
Mhhh!wamasai baadhi wamestaarabika sikuhizi,kuna wabarbaigi,hawa wanaishi porini,mwenzao akifa wanahama kwny lile boma wanamuacha huko,wanaenda mbali kuanza maisha,eti wanaogopa maiti
 
Basi watakuwa dili ngoja niwatonye wazee wa migodi
 
Kichwa cha habari kimenishtua asee nikasema hee shem wangu yamemkuta yapi. Kumbe ni ishu ya wamasai kweli hata mi sijashuhudia ila maiti nimeona ya mmasai sbbu ya kazi yangu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom