Bakari Maligwa
Member
- Aug 18, 2010
- 65
- 22
...Siasa ni "ka-mchezo" ka ujanja! Nadhgani nikitumia maneno haya ya kijinga Mh. Rostam anaweza kunielewa vema. Simfahamu sana Rostam Aziz ila kwa kumsoma kwenye "kafsha" mbalimbali na ushiriki wake kwenye siasa za CCM na kwa jinsi alivyoweza kumsaidia Jakaya Kikwete kwenye Uchaguzi Mkuu wa 2005 na hatimaye JK kupata ushindi wa "kimbunga". Rostam Aziz anadai siasa za CCM ni "uchwara" kwa kuwa ameharibikiwa na biashara zake za kitaifa na kimataifa...! Hii ni sawa na shairi la "KAKA SUNGURA" lililokuwa linasomwa na wanafunzi wa darasa la tatu enzi zile elimu ilivyokuwa na thamani...sizitaki mbichi hizi, naona nafanyakazi bila faida kujua...! Haya ni maneno ya mtu aliyeshindwa kupambana na kasi ya mabadiliko ya ndani na hanikizo la nje ya chama (CCM) kwa kuwa Riostam amekuwa akijihusisha na siasa kwa kuzinufaisha biashara zake. Hakuna uandishi utakayeacha kumuandika Rostam Aziz kwa jinsi alivyoshiriki kwenye siasa za kifisadi na kuendesha ujambazi wa kiserikali kwa kutumia nafasi zake kwenye CCM na IKULU ambapo ana ushawishi mkubwa sana! Tuachane naye kwani aliwahi kunipigia simu na kuniambia, "kama nataka siasa niache ualimu wa chuo kikuu niingie kwanye siasa; na yeye (Rostam) amekuwa tajiri kutokana na urithi wa wazazi wake na ujanja wake kibiashara..."...Binafsi maneno haya yaliniudhi sana kwa vile mwanasiasa hawezi kutumia nafasi yake kufanya ufisadi...na hata maana ya neno hilo, yaani siasa, ni mwendo murua wa kuwatumikia watu bila ya kufisidi mfumo na au ndani ya mfumo! Kuwapa misaada wananchi wa Igunga na kwengineko huku unafanya ufisadi si siasa bali ni si-hasa inayoambatana na ujambazi wa kiserikali.