Buchanan
JF-Expert Member
- May 19, 2009
- 13,199
- 1,969
WanaJF,
Nimekuwa na tatizo kidogo ndani ya familia yangu, hasa wakati huu wa michuano ya Kombe la Dunia inayoendelea kule Afrika ya Kusini. Mimi napenda kuangalia michuano hiyo kupitia runinga, especially zinapocheza timu za Afrika lakini "ubavu wangu" unapenda sana kuangalia tamthiliya! "Katatizo" hako kako kwenu jamani au ni mimi tu jamani! Natamani niwe naangalia kwa jirani lakini naona haipendezi, inawezekana huko nako kuna "tatizo" kama hilo. Jana niliangalia kipindi kwenye Channel 5 nako walizungumzia "tatizo" hilo na ilisemekana kwamba kuna mama wa familia moja aliamua kununua TV yake mwenyewe ili aendelee kuangalia tamthiliya, huku baba na wakaka wakiangalia michuano ya kombe la dunia! Ama kweli kuna mambo!
Nimekuwa na tatizo kidogo ndani ya familia yangu, hasa wakati huu wa michuano ya Kombe la Dunia inayoendelea kule Afrika ya Kusini. Mimi napenda kuangalia michuano hiyo kupitia runinga, especially zinapocheza timu za Afrika lakini "ubavu wangu" unapenda sana kuangalia tamthiliya! "Katatizo" hako kako kwenu jamani au ni mimi tu jamani! Natamani niwe naangalia kwa jirani lakini naona haipendezi, inawezekana huko nako kuna "tatizo" kama hilo. Jana niliangalia kipindi kwenye Channel 5 nako walizungumzia "tatizo" hilo na ilisemekana kwamba kuna mama wa familia moja aliamua kununua TV yake mwenyewe ili aendelee kuangalia tamthiliya, huku baba na wakaka wakiangalia michuano ya kombe la dunia! Ama kweli kuna mambo!