Sio za serikali lakini usisahau kwamba serikali walikuwa na big interest kwa IPTL coz' tayari kulishakuwa na pesa za Escrow ambazo zilikuwa zinatoka TANESCO... hii issue ilikuwa not yet resolved hususani tukiangalia suala la capacity charge. Kwahiyo, ingawaje IPTL haikuwa na sio ya serikali lakini serikali ilikuwa na nafasi yake ndani ya IPTL. Sio hivyo, kama nilivyosema hapo awali, tayari IPTL iliwekwa chini ya Mufilisi... na mufilisi ni RITA ambae pia ni serikali... kwa mara nyingine, bado utaona ushawishi wa serikali kwa IPTL. Sasa basi, bado tunarudi kule kule...ndani ya Escrow account (resulted from IPTL Saga) kuna billions of Tanzanian shilings zinazotoka kwenye sekta ya nishati halafu tena tunaona Rugemalila analipa millions of Tanzanian Shillings kwa government officials ambao kwa kiasi kikubwa wanahusika na ama sekta ya nishati au mikataba ya serikali...NO, there must be something!! Come on man, we ain't talking of petty cash here but millions of Tanzanian shillings no one can offer it for free! I know you
jMali... u're not this blind... user ID yangu inaweza kukuchanganya lakini kama unaweza kusoma between the lines, kwa makusudi kabisa wala sijabadilisha sauti yangu... ukiwa makini utajua unaongea na nani... you're not that blind tunapokutana kwenye mijadala ya Rwanda vs Tanzania!! Aidha, ni kweli kabisa kwamba Ruge haku-deal na serikali lakini kalipa millions of $ kwa government officials unless kama statement zinazotolewa hapa si za kweli... ana biashara gani nao hawa?
Sijakuelewa unaposema hata ukiangalia timeline, utagundua deal ya Ruge na Seith ilikuwa before Escrow? Before Escrow kivipi? I hope this's not your first time to know Escrow started to operate since 2006... but if you mean before Escrow Saga, then the answer is simple... Escrow Saga ilikuja baada ya mambo ya ajabu ajabu kufanyika... mosi, pale ilipogundulika IPTL ambayo ilikuwa chini ya mufilisi inapigwa bei, pili, Mechmar yenyewe walikuwa na kesi na creditor wao (Standard Chartered Bank Hong Kong) na hivyo hawakutakiwa kuuza IPTL... lakini baada ya kuzama zaidi, tukakuta wale wale waliopewa jukumu la IPTL ndio hao hao ndio waliopewa millions of money na Ruge... mbaya zaidi, wakati Ruge na 30% yake analipwa Millions of Dollar na PAP, IPTL inauza 70% yake kwa dola chini ya elfu nne... kisha tena unakuta Ruge yule yule kamlipa millions of shillings officer wa TRA ambae aliwajibika kujiridhisha na thamani rasmi ya hisa za IPTL ili tupate capital gain tax inayostahili!!! Nachelea kujaza kurasa ningefafanua intuition yangu kuhusu mchezo ambao ulichezwa na Seth kwa kushirikiana na Ruge! Kwa kifupi tu, kuna uwezekano mkubwa kwamba pesa ambayo ingetumika na seth kulipa Capital Gain ndiyo iliyotumika kumlipa Ruge na hili mchezo ufanyike, ndipo Ruge akaamua kumpa chake ofisa wa TRA.
Hapana... hatujalubaliana na hatuwezi kukubaliana! Nilichosema ni kwamba, ingawaje ni kweli Ruge pesa ni yake na ana haki ya kutumia anavyotaka yeye lakini tunapoona kawalipa maofisa wa serikali ambao kwa kiasi kikubwa wanahusika kwenye saga lililopo, NO... lazima tu-question hayo matumizi!
Hapa nakubaliana na wewe lakini as long as Escrow akaunti imekuwa emptied to IPTL shareholders with $ 0 to TANESCO bila kuambiwa mgogoro wa service charge umeishaje, hiyo ni sababu tosha kabisa kuonesha kwamba kuna tatizo, tena si dogo!!! Sasa inapotokea taarifa kwamba XYZ amelipwa na Ruge kwa biashara isiyofahamika, tena XYZ wenyewe ni wale wale ambao, ikiwa lengo ilikuwa ni kuchafua watu tu, basi wengine wala wasingeonekana. Mathalani, why should you include Paul Kimiti? Why should the bank statement show hadi watoto wa Ruge... nature ya majina inatufanya wengine tuamini kwamba the uploded bank statements might be legit.
Hawa ni miongoni mwa wale wanaoonekana kwenye uploaded bank statements:
1. Kuna watu wawili wa RITA... IPTL iliwekwa chini ya mufilisi (RITA) kwahiyo huwezi kuiuza IPTL bila kuihusisha RITA
2. Kuna watu wawili wa TRA... tunaambiwa kwamba PAP imemenua 70% ya hisa za IPTL kwa pesa isiyofika hata sh. milioni kumi! Hapa mtu anaweza kusema, ikiwa IPTL ni mali binafsi basi wana haki ya kuuza bei yoyote waitakayo... jibu HAPANA... hawawezi! Anyway, mali ni yao kwahiyo wanaweza kuuza hata kwa $ 100 lakini ikitokea hivyo, TRA watakachofanya ni ku-revalue mali iliyouzwa (for this context IPTL). Kama thamani say inakuwa $ 100 million , watakachofanya TRA ni kusema "we no problem na wewe ikiwa umeuza kampuni yako kwa dola 5000 lakini kodi yetu utalipa sawa na mali iliyouzwa $ 100 million!!!" Why? Kwa sababu isije mtu anasema amenunua kwa $ mia moja ili akwepe kulipa kodi stahiki! Hata watu wadogo kama sisi tukiangiza hata gari ya $ 10,000/- ukifika pale custom TRA watakuambia, NO... hii gari thamani yake ni $ 20,000 na utalipa kodi kama gari yenye thamani ya $ 20,000!!!
3. Chenge: Huyu alipata kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali... huyu itakuwa amehusika sana na issues za IPTL enzi zake kwahiyo kilichopo sasa ni reward for job well done in those old days! Same applies to Daniel Yona na William Ngeleja ambao walipata kuwa mawaziri wa nishati hapo kabla!
4. Watu kama akina Tibaijuka inawezekana zilitoka in goodwill but 1.6 billion is a questionable amount... haiwezi kuachwa tu ipite hivi hivi kwa kisingizio kwamba imetolewa hadharani! Come on jMali, tell me something... hivi katika hali ya kawaida, leo hii braza Ruge aende kwa Tibaijuka kumtaka apewe upendeleo wa XYZ kwenye wizara ya Tibaijuka, hivi kweli Anna anaweza kuwa na ujasiri wa kukataa pamoja na miela yote ile aliyoichukua hata kama haikuingia kwenye a/c binafsi?
Wakati nipo benki kuna mteja mmoja alinipa elf 10 in goodwill! Alinikera sana lakini alinipa katika mazingira ambayo, kama ningeikataa, kuna watu wangeona nazuga naona aibu macho ya watu na wapo ambao wangeona ni embarrassment kwa mteja!Nikaipokea kwa shingo upande! You know what happened next? Several weeks later akaja yule mteja (nilikuwa nimemshasahau). Ndani kulikuwa na foleni ya kawaida sana lakini alichofanya ni kunipa kadi yake nikamchukulie hela kwenye akaunti yake! Nikamjibu mbona foleni sio kubwa...panga tu foleni! Unajuaje aliniulizaje? "Umenisahau?" Baada ya kuniuliza, nikamwangalia kwa makini, nikakumbuka kwamba ni yule mama ambae alinipa buku 10!!! Kwa shingo upande mzee, nishakula vya watu nitafanyaje... nikaenda kumchukulia hela but at the same time nika-deposit sh.10,000 kwenye kaunti yake nikampelekea na vocha... hadi natoka hakunifuata tena yule mama!! Kwahiyo hizi pesa zinazotolewa in "goodwill" baadae zina impact kubwa sana!!