Wazo Langu
JF-Expert Member
- Mar 21, 2011
- 1,381
- 842
JMali mbona jina lako kama James rugeMALIla?
Na mimi naombeni mgao nikaezeke kibanda changu kule kikongo.
Na mimi naombeni mgao nikaezeke kibanda changu kule kikongo.
jamaa hakuiba directly, alitumia mbinu ili watu kama wewe msiweze kuelewa. alijua pesa za escrow zinaenda tanesco na hisa zake zingeshuka sana thamani. ndiyo akaanza michakato ya kutoa hela kwa kushirikiana na aliowalipa ili anunuliwe. PAP wasingenunua hisa zake kama asingewahakikishia kwa kupata pesa. ni kama mwanamke aliyejitolea mahari sema hapa hiyo mahari anakuwa kaiba.FACTS:
1. James rugemalira alikuwa anamiliki 30% ya IPTL kupitia kampuni yake ya VIP. Asingeziuza hizo hisa, mpaka leo angekuwa bado anamiliki 30% ya IPTL KIHALALI kabisa, hivyo kuwa mbia mwenza wa PAP.
2. James rugemalira aliuza hizo share zake kwa kampuni ya PAP kwa dola milioni 75. Uuzaji wa hizi hisa ulifuata taratibu zote kisheria including ulipaji kodi.
MASWALI:
1. Huyu ndugu anaitwa mwizi kivipi? Amelipwa fedha kutokana na kuuza hisa, tatizo liko wapi hapo? Kisheria angeweza kumuuzia yoyote yule tofauti na PAP hizo hisa kama wangeafikiana bei! PAP wamefikia dau na yeye kawauzia, where is the problem hapo? IPTL sio kampuni ya umma, PAP sio kampuni ya umma, VIP sio kampuni ya umma. This is purely a private sector transaction. Mbona Rostam aliuza share zake vodacom kwa mabilioni tena kupitia nje ya nchi lakini hakuitwa mwizi (kwa kukwepa kodi among other things), badala yake akasherehekewa kwa front-page news? Naomba kufahamishwa kwa hoja tafadhali, uharamia wa James Rugemalira upo wapi.
ni njama ya wizi mkubwa kati ya maofisa wakuu serikalini wawekezaji wanasiasa na wanasheria. makosa ya ruge yanahitaji kubainishwa wazi ili ashtakiwe. upo ushahidi tele wa kutoa rushwa na taarifa za uongo.
jamaa hakuiba directly, alitumia mbinu ili watu kama wewe msiweze kuelewa. alijua pesa za escrow zinaenda tanesco na hisa zake zingeshuka sana thamani. ndiyo akaanza michakato ya kutoa hela kwa kushirikiana na aliowalipa ili anunuliwe. PAP wasingenunua hisa zake kama asingewahakikishia kwa kupata pesa. ni kama mwanamke aliyejitolea mahari sema hapa hiyo mahari anakuwa kaiba.
Mkuu jMali,
Braza Ruge tunambana hapa!
- Mosi, yeye ni mtu anayeifahamu IPTL in and out kwa sababu amekuwa nao kwenye biashara kwa muda mrefu. Ushahidi unaonesha wazi kwamba PAP imepata 70% ya hisa za IPTL kwa magumashi. Inasemekana baada ya Singh kuingia nchini, Ruge alimpinga huyu bwana... Aidha, kuna kila dalili kwamba hata hiyo PAP yenyewe ni ghost company. Pamoja na yote hayo, bado Braza Ruge akawauzia PAP hisa zake 30%. Sasa ikiwa Ruge alikuwa anaifahamu IPTL na Menchmar in and out to the point kwamba ilikuwa ni rahisi kwake kama kufumba na kufumbua kufahamu ikiwa kweli PAP waliuziwa 70% za Menchmar ambazo inaonesha kwamba hawakuuziwa ama wameuziwa kimagumashi.... sasa je, huoni Ruge nae ameuza hisa zake kwa mtu ambae bila shaka alifahamu kwamba ni mwizi tu na bado akawa tayari kufunika kombe... PAP wachukue pesa zetu zilizokuwa Escrow wakati anafahamu haikuwa sahihi?
- Umwagaji wake pesa kwa viongozi na watendaji wa serikali na wale ambao walipata kuitumikia serikali ni jambo ambalo halipaswi kuachwa hivi hivi. Ni kweli, pesa ni zake na ana haki za kutumia apendavyo lakini inapoonekana kwamba wengi wa waliolipwa wanatoka sekta ile ile ya nishati huku wengine wakiwa hawapo tena kwenye system, lakini ile tu kuwa walipata kuwamo MEM, tayari nao anawapa mamilioni ya pesa... hili si jambo dogo... Si hivyo tu, hata wale ambao ni wahusika katika mikataba ya serikali, AGs... Chenge ambae ameshastaafu kwenye hiyo nafasi long time ago lakini nae kamegewa mzigo wa kutosha! Kuna yule wa RITA ambae RITA ndio wanahusika kwenye masuala mazima ya ufilisi huku Braza Ruge nae alipeleka kesi mahakamani kutaka IPTL ifilisiwe... hili ni jambo ambalo hutakiwi kulipuuza hata kidogo! Kama nilivyosema hapo awali, pesa ni zake na ana haki ya kutumia apendavyo lakini anapomwaga mamilioni kwa watendaji wa serikali ambao kwa kiasi kikubwa wanahusika na IPTL in one way or another... NO PLEASE, tunahitaji maelezo yasiyopinda pinda na atuambie amefanya nao biashara gani! ALWAY, I repeat, ALWAYS, there's only one money related business between government officials and business executives especially if such transaction isn't done on public... what's the business? The answer is simple: CORRUPTION! Here's the Theory: "To Every Corrupt Government Official, There's a Corrupt Business Executive Behind Him!"
jamaa hakuiba directly, alitumia mbinu ili watu kama wewe msiweze kuelewa. alijua pesa za escrow zinaenda tanesco na hisa zake zingeshuka sana thamani. ndiyo akaanza michakato ya kutoa hela kwa kushirikiana na aliowalipa ili anunuliwe. PAP wasingenunua hisa zake kama asingewahakikishia kwa kupata pesa. ni kama mwanamke aliyejitolea mahari sema hapa hiyo mahari anakuwa kaiba.
Mkuu,
Soma hapa ndo utaelewa:
Facts on IPTL deal ahead of the tabling of escrow scam report - National - thecitizen.co.tz
Ndugu usishangae sana kuhusu sisi Watanzania na mimi nikiwemo. Na tunadhihirisha na tafiti zilizofanywa tukaonekana Tanzania tuna watu wa IQ ndogo sana na ndio maana badala ya kujadili issue tunajadili watu . Badala ya kujiuliza zile 70% of shares zilikuwa halali kuuzwa TZS6m? Was due process followed to the letter? Badala yake tunaletelwa list ndefu ya majina tena tunashupalia yale ambayo tunayajua kwa maana ya judges na mawaziri. Inakuwaje mmiliki wa 30% aliyeuza share kuahalali mchana kweupe katika jua la utosi na kulipa kodi ndio tunataka kumsulibisha. Tumeruka toka kwenye fedha kuchukuliwa na singasinga sasa tunataka kutundika wa 30%. Tumeama badala ya kuagnalia due process tunajadili majina kuwa wamegawiwa pesa kama njugu. Is this really our concern? Do we have a process that governs monetary transactions. is it viable? Does it need improvement? Is the country protected? Are our local investors protected by laws and policies? Watanzania lets think bigger. Wakati wa Richmond tudanganywa na wanasiasa kwa sababu ya chuki zao za kukosa vyeo. Bwana Lowasa wakati anakubali kujiuzuru alitoa speech lakini hatukuagalia context yake kuwa " shida ni uwaziri mkuu" . Sote ni mashahidi baaada ya kumtosa yuleyule aliyeliazisha Samwel Ssita kasema mjadala umefungwa yeye akaja kuuendeleza nje ya bunge baada ya jinamizi la Dowans na kuamuliwa kuwa lazima tuwalipe. Haya yote yanatokea na kwa hii Escrow yatatokea maana we are discussing people and not the process neither the issue
Go deep you are trying to ask light questions for serious problem.issue si kuuza share.hicho ni kitu cha kawaida kabisa kwa wale wanaojua mambo fedha.Tatizo linaanzia tanesco ambalo ni shirika la umma.tanesco na iptl wana mkataba wa kuuziana umeme.Regemalila yuko ndani ya iptl na akaunti yake imetumika ktk kukwapua pesa benki kwenye account ya escrow.sasa basi ebu jiongeze mwenyewe kuanzia hapo au fuatilia vizuri huo mjadala bungeni utajua nn kimefanyika
Umejipanga kuja kuongeza hasira za watu! bila shaka ni sababu ya nguvu ya hiyo hela vinginevyo tutakuja na version ya Rugemalira baada tu yahili la watumisi wetu kukaa sawa.
Only the court of law can give best answers to your questions! Again , is Tanzania judiciary credible?
...
Acha uzembe cag na wengine hawakuliona hilooo.
Mkuu kutetea kote huko unaweza kukuta hukuambulia hata elfu10 ya vocha.
Mkuu unaonekana upo mbali na ukweli na hata haufuatilii issue nzima ilivyo. Kwa taarifa yako JR aliwahi kuiandikia Wizara ya Nishati na kupeleka nakala kwa taasisi 23 ikiwemo BoT, kwamba PAP imlipe pesa zake kwanza kabla ya kupewa fedha za ESCROW.Ajabu PAP wakalipwa ndiyo JR ndiyo akapewa chake. Huhitaji kwenda shule kujua kuwa JR alilipwa pesa za ESCROW. Hizo fedha kuna kodi ndani yake, lakini inasemekana ni haki ya Tanesco. Kosa la JR ni kupokea malipo ya fedha zenye utata ambazo yeye mwenyewe alitahadharisha kabla ya kulipwa. Lakini baada ya kulipwa inatia shaka kwa hao wanaogaiwa. Ni wateule Fulani hivi. Ni sawa JR kauza hisa zake, lakini namna alivyouza, source ya fedha na hao anaowagaia ndiyo tatizo
Tusijibu juu juu hii hoja. Hata mimi niliposoma katika gazeti la The Citizen mtiririko wa matukio yote ya hili sakata, niliona kama vile JR hana kosa, kwani aliuza hisa zake kabla hata fedha za ESCROW hazijaruhusiwa kugawiwa IPTL. Naomba tujibu hoja kwa hoja, sio kusema tu kuwa mleta mada ametumwa bila ya kujenga au kujibu hoja
Kama nimelewa vyema, Regemalila alikwisha maliza biashara yake na PAP, kwani PAP walinunua IPTL yote ikiwa ni pamoja na hisa 30% za Rugemalila kupitia VIP Engineering, maana hata tranfer ilifanyika na caiptal gain Tax zililipwa.... sasa inakuwaje anapata mgao katika EScrow ambayo ilitolewa BOT kwa maana ni hela za PAP sio za IPTL ambayo Rugemalila ndio alikuwa na mslahi huko? maana yake Regemalila inawezekana alitumika kugawa rushwa na ndio litakuwa kosa lake
Mkuu ukiangalia hizo hisa utakwama kwenye tope hawa jamaa wamegawana pesa siyo zao na bado wanadaiwa Bilioni 15 na Tanesco, sijui kama umenielewa ndiyo maana Takukuru na CAG wameingia kwenye ili sakata.