Korea Kaskazini: Taifa hatari Kuliko Yote Duniani

Korea Kaskazini: Taifa hatari Kuliko Yote Duniani

1430804931454.jpg 1430804948823.jpg 1430804962789.jpg 1430804984440.jpg
 
Mtoa mada anasimulia movie iliyotengenezwa Hollywood......huko korea hukuwahi kwenda, nchi yenyewe ujui inafananaje, raisi wao mwenyewe unamuonaga kwenye tv tu tena mara chache ....za kuambiwa changanya na zako
 
Kama ni propaganda hebu jaribu kwenda Korea Kaskazini uone kama utarudi tena Tanzania,utakamatwa na kuozea jela kwa kosa la kuipeleleza nchi yao,wakati maskini umeenda kutembea tu,watasema umetumwa na Marekani.

Muulizeni Mhe. Lukuvi amewahi kwenda lakini alirudi salama mpaka leo anasema wale jamaa ni waaminifu katika vitu vyao hakuna taifa lolote Duniani kama wale.
 
Wengi wetu habari za KK tunazipata hasa kwenye vyombo vya habari vya Magharibi ambavyo vimejikita zaidi katika propaganda na si ukweli.

KK ni moja ya nchi ambayo ina usiri mkubwa sana na sio rahisi kujua wanaishije kama hujawai kufika huko.

Vyombo vya Magharibi haviwezi kumsifia Kim na nchu yake kwa sababu wa yupo nje ya Mfumo Dunia.





Tuwe wa kweli kabisa kabisa . Wazungu huwa hawadanganyi kwenye taarifa zao.
Waandishi wa habari wa nchi za magharibi wanajitolea kuandika taarifa za kiuchunguzi hata kama mwenzake ameuaja jana leo atakwenda tu.

Na pia vyombo vingi vya habari vya magharibi viko huru na havimililkiwi na serikali zao vyote .
Na wenzetu wanajua adhari ya kuandika taarifa za uongo. Kuwadanganya watu kuwa wazungu ni waongo ni kuwafanya watu wawe wajinga. Leo hii taarifa zote zimewekwa kwenye mitandao mtu anagoogle tu anapata jibu hapo hapo.Sasa kama utamfundisha mtoto wako kuwa wazungu ni waongo utamfanya ashindwe kutafuta taarifa na kujifunza mambo mengi.
Elimu yote tunayoisoma na kujifunza asilimia kubwa ni ya magharibi sasa ukisema kila kitu ni propaganda unapotosha umma.

Kwa mfano Mzungu akikuambia tarehe 25/7/2015 saa mbili asubuhi patakua na kupatwa kwa jua na mwezi basi ujue utafiti ulishafanyika.

Mzungu ameshatafiti mpaka namna mchwa ,siafu ,simba,nyoka n.k wanavyoishi na kuzaliana na hatimaye akaweka kwenye dvd na wote tunafaidi. Ukitaka uwe wa ajabu waambie watu kwamba ni tafiti za uongo.

Kama ni move au tamthilia basi wazungu wako wazi wanakuambia hii sio kweli ni igizo.

Korea sio tishio kwa nchi za magharibi kama tunavyofikiri bali ni tishio kwa baadhi ya wakorea wenye maoni tofauti na aliyonayo mfalme na serikali yake.
Ni tishio kwa watu wenye imani tofauti na imani ya dini zao za asili.

Nakumbuka wakati mh Rais wetu alipoingia madarakani alienda uingereza akakutana na kashfa ya watu wa Mwanza kula mapanki ya samaki kutokana na umaskini wa kushindwa kununua minofu ya samaki kama wanayosafirisha kwenda ulaya.
Watu walikuja juu sana akiwemo mh .Rais na kusema kuwa ni propaganda za kuchafua nchi yetu.
Lakini wale tuliokua tumeyaona hayo mapanki yakitumika kama chakula tulikua hatukushangaa.

Hata mauaji ya albino yalianza kuandikwa na vyombo vya magharibi watu wakasema ni propaganda chafu kwa watanzania.

Na pia tukumbuke kuwa vyombo vya magharibi huwa vinaandika hata taarifa za kukosoa nchi zao.
Kwa mfano kama wanajeshi wa nchi kama marekani watafanya vitendo vya kudhalilisha binadamu wengine wakati wa kufanya kazi zao ni wazi kuwa vyombo hivyo hivyo vimekua vikitoa taarifa na hatua zinachukuliwa.
 
Acha kuwa sehemu ya propaganda za kimangaribi ....TAIFA masikini linaweza vipi kuwa na nguvu ya kisayansi na teknelojia ...au umekariri ...Ndio maana Tanzania tunanunua hadi chupi



Korea ya kaskazini haina teknolojia kubwa sana.
Wamewekeza zaidi kwenye jeshi .

Korea ya kusini ndio wenye teknolojia kubwa sana kuliko hata baadhi ya nchi za magharibi.
 
Nakubariana na wewe kwenye upande wa kunyoa stail km anayonyoa yeye
 
ap_north_korea_kim_jong_jp_121217_wmain-1cff1.jpg


145884343.jpg


Wakorea wakisujudu mbele ya sanamu ya raisi Kim Jong-Un
 
Hahaha, wewe ni mpotoshaji mzuri, maana mtu analeta fact, unashindwa kupinga kwa kuleta fact zaidi ya porojo za Kimangharibi
Halafu alivyokuwa mwendawazimu anasema wananchi wa Korea kaskazini ndio wanaishi maisha magumu kuliko wengine wote hapa duniani, sijui kala maharage ya wapi huyu! Tanzania tuna maisha gani ukilinganisha na North Korea?!
 
akili yao imezoea,je wanaruhusiwa kisikiliza radio au kuangalia tv za channel za kimataifa?

Mtasikiliza redio na tv za ndani kwao tu, mitandao imekatwa huwezi kupata mitandao kama unavyojiachia sasa
 
Kuwa na nguvu za kisayansi na technology siyo kuwa na nguvu za kiuchumi,hawa kaskazini wame invest nguvu zao ktk jeshi,wanatumia uwezo wao wa sayansi na teknoloji ktk kutengeneza vifaa vya vita na nyuklia,kwa mfano Urusi,ina vifaa vya kisasa vya vita na ina uwezo mkubwa sana wa kijeshi na pia ina sayansi na teknoloji ya hali ya juu sana,lakini haina uchumi imara kama US,UK,Canada,Germany na inazidiwa uchumi na wachina,wewe ndo umekariri kila jambo la kweli eti ni western propaganda,ni South korea ndo wana uchumi mzuri sana,hao ndo wanazalisha bidhaa za Samsung duniani na magari yote ya Hyundai,niambie jamaa zako North korea wanazalisha nini? Watu hatukurupuki ku post mada bila utafiti wa kina na ushahidi.

Mkuu ww ndo umelewa zaid propaganda ulposema sourhern korea ndo wapo juu kwa sababu wanatengeneza bidhaa ulzotaja ukweli ni kwamva korea zote zina background moja hata hali zao za kiuchumi znafanana ni kama nchi moja iliyojichorea mstari kwamba nyie wa huku cc wa kule...umeleweshwa zaid na propaganda za marekan et korea kaskazin inainvest sana kwenye jeshi hao USA unaosifia kuwa ndio nchi pekee ambayo imewekeza zaid kwenye ulinzi na silaha na ndo nchi pekee ambayo bajet yake ya ulinz pekee ni kubwa kuliko bajet za nchi zote na pua nan asiyejua kama marekan wana nyuklia? Ndo mana niimkosoa mtoa mada toka mwanzo kwamba hzi ni propaganda za hollywood na hara uteuz wa ban ki moon UN kutoka korea kusini ni moja ya mbinu za kuitishia korea kaskazin....... mahali unapoipata habari panadetermine ukweli wa habari hiyo kama imetolewa na shehe atakwambia nguruwe ni mbaya sana na kama imetolewa na padre atamsifia mdudu nguruwe hana shaka
 
Hivi north Korea kuna diaspora wetu kama wapi watupe facts sio hizi hearsay
 
Acha kuwa sehemu ya propaganda za kimangaribi ....TAIFA masikini linaweza vipi kuwa na nguvu ya kisayansi na teknelojia ...au umekariri ...Ndio maana Tanzania tunanunua hadi chupi

We acha kuwa na mtazamo potofu, unazani wamarekani wanapenda nchi yeyote dunian kuwa juu yao kwa taarifa za kiusalama, KK ni moja ya nchi zinazohogopwa na kufiwa na marekani, hvyo wanajitaidi kwa namna yeyote ile kuinyong'onyesha serikali hiyo kwa kuichafua

Mmarekani kakudanganya wewe!

Hii kasumba ya nchi ambayo si magharibi kwa habari nzuri mnaisifia sana na kupiga vigeregere lakini kwa habari mbaya mnakuja hapa na kusema 'huyo ni marekani' ama propaganda za magharibi hii kasumba mmetoa wapi?! Kwa hali hii tuwalaumu wabunge kweli kwa kushindwa kutunga katiba kama na wananchi wako ivi?!
 
Back
Top Bottom