Korea Kaskazini: Taifa hatari Kuliko Yote Duniani

Korea Kaskazini: Taifa hatari Kuliko Yote Duniani

Leo hii ukimuuliza mtu ni nchi gani ambayo si salama kuishi duniani? Wengi watakuambia ni Somalia,ni kweli ila Somalia ni ya tatu duniani kutokuwa salama,North Korea inaongoza,wananchi wa taifa hili wanaishi maisha magumu kuliko mwananchi yoyote ktk sayari hii ya dunia,hawaruhusiwi kwa namna yoyote ile kuikosoa serikali,na kama ukijaribu basi unafungwa wewe na watoto wako hadi kizazi cha tatu,vijana wanafanya kazi bure ktk viwanda vya serikali na migodi na kuishia kula na kutibiwa bila mshahara,na unatakiwa ufanye kazi hadi siku ya kufa,wanaume wote hawaruhusiwi kunyoa staili zao,wote hutakiwa kunyoa pank kama rais wao Kim Jong Un,uchumi wa taifa hilo unategemea zaidi ktk kuuza silaha kwa mataifa ya ki dikteta na madawa ya kulevya pamoja na Viagra feki,rais wa taifa hilo na baadhi ya viongozi wanaishi maisha ya anasa wakiagiza chakula kutoka nje ili wale wao tu na familia zao,wananchi hawaruhusiwi kuwasiliana na watu nje ya taifa lao iwe kwa simu au email,Kim Jong Un ni mlevi na anapenda sana ngono,ni katili.

Acha kuwa sehemu ya propaganda za kimangaribi ....TAIFA masikini linaweza vipi kuwa na nguvu ya kisayansi na teknelojia ...au umekariri ...Ndio maana Tanzania tunanunua hadi chupi
 
We acha kuwa na mtazamo potofu, unazani wamarekani wanapenda nchi yeyote dunian kuwa juu yao kwa taarifa za kiusalama, KK ni moja ya nchi zinazohogopwa na kufiwa na marekani, hvyo wanajitaidi kwa namna yeyote ile kuinyong'onyesha serikali hiyo kwa kuichafua
 
flamini unataka kuniambia Pyongyang hamna international flights ziingiazo na kutoka?
zipo from china na sijui russia kitu kama hiko..ila wale raia wenyewe hawaruhusiwi kutoka kama sio government official..kuna familia kutoka south and north korea ambazo zimetengana kutokana na vita basi zinakutanishwa mara moja kwa mwaka tena mipakani kwa masaa alafu wanaaachana tena sasa kama wangeweza kutoka si hata wangehamia south korea kwa familia zao wengine..
 
Ni kweli kabisa, North Korea mtu akipatikana na kosa, basi familia yake yote hadi ndugu wanapewa adhabu sawa na mtenda kosa!
 
Mm kuhusu. Yule bwana mdogo korea siwezi kubisha sana anamambo ya kijinga kijinga anaweza fanya lolote na wakati wowote na bila kufikiria
 
​nilishangaa Kim kununua dege la kisasa na kifahari......sasa nikajiuliza hili atakuwa anasafiria nalo masafa ya mbali waapi

Hilo dege ni bosheni tu,hawezi kusafiri nalo,safari ya kim mwisho ni china,na huko hapandi ndege,anapanda treni au msafara wa magari,ndege anaogopa wamarekani wanaweza kuilipua ikiwa angani.
 
Wise boy naona hii habari umeisoma kwenye site yenye chumvi nyingi, watu wa korea wanasafiri, ila kweli nchi hio iko kidictator.. wananstyle tatu tu za kunyoa nywele, na adhabu za kifo ni kitu cha nje, yule kiongozi wao ni spoilt brat mwenye utoto, mf ile safari ya Moscow titular state ndo alisafiri badala yake, viongozo wake apri walitoka nje ya kikao cha UN kile cha human rights, soma juzi tar 1 wamesema wanafunzi wa north korea walioko UK watapiga kura kwa mara ya kwanza(democracy) so ume kuza sana facts thou kweli Kim ni mwehu na katili
 
Acha kuwa sehemu ya propaganda za kimangaribi ....TAIFA masikini linaweza vipi kuwa na nguvu ya kisayansi na teknelojia ...au umekariri ...Ndio maana Tanzania tunanunua hadi chupi

Kuwa na nguvu za kisayansi na technology siyo kuwa na nguvu za kiuchumi,hawa kaskazini wame invest nguvu zao ktk jeshi,wanatumia uwezo wao wa sayansi na teknoloji ktk kutengeneza vifaa vya vita na nyuklia,kwa mfano Urusi,ina vifaa vya kisasa vya vita na ina uwezo mkubwa sana wa kijeshi na pia ina sayansi na teknoloji ya hali ya juu sana,lakini haina uchumi imara kama US,UK,Canada,Germany na inazidiwa uchumi na wachina,wewe ndo umekariri kila jambo la kweli eti ni western propaganda,ni South korea ndo wana uchumi mzuri sana,hao ndo wanazalisha bidhaa za Samsung duniani na magari yote ya Hyundai,niambie jamaa zako North korea wanazalisha nini? Watu hatukurupuki ku post mada bila utafiti wa kina na ushahidi.
 
mkuu hayo mambo yalikuwepo toka kitambo au yameanza baada ya kufa kwa rais aliyepita ?
 
1430804128609.jpg 1430804150739.jpg 1430804166477.jpg
Angalia miji yao, hapa nyie hata kupanga mji vizuri tu mmeshindwa alafu mnasema maskini mvua ikinyesha kidogo tu mafuriko.
 
Back
Top Bottom