KM OWM - TAMISEMI: Kuna shida gani kuruhusu uhamisho wa kufuata Mwenza?

KM OWM - TAMISEMI: Kuna shida gani kuruhusu uhamisho wa kufuata Mwenza?

Enthusiastic

JF-Expert Member
Joined
Dec 21, 2023
Posts
347
Reaction score
691
Kuna ule msemo unaosema "ajira ni utumwa" kuna ukweli katika msemo huu sana sana kwa TAMISEMI na OR-Utumishi.
1. Hawajali kabisa ustawi wa mtumishi. Mtumishi hawezi kuwa na utulivu kazini kama yuko mbali na Mwenza tena kwa kazi yenye mshahara tu bila marupurupu.

2. Kuna kisingizio cha msawazo na upungufu wa watumishi. Hii hoja haina mashiko. Hakuna mahali ambapo watumishi wamewahi tosha hata huko anakotaka kuhamia kuwaweza kukawa na upungufu mkubwa kuliko anakotoka. Mbona wakistaafu hamuwazuii? Mbona wakifa hamuwafufui?

3. Vyama wa wafanyakazi TALGWU na TUGHE havitetei ustawi wa watumishi ambao ni wanachama. Wanachojua ni kula michango ya wanachama.

4. Ukiendelea kukomalia kuhamia unaambiwa chagua kazi au ndoa. Kuna watu maofisini wamekula maharage wameshiba wanajibu shombo.

5. "KAZI NA UTU" sio halisi.
Dr. Mwigulu Nchemba ofisi yako mnatusumbua. Wewe ni Mkristo, maandiko yanasema, "ndoa na iheshimiwe na watu wote......" Waebrania 13:4. Imagine mtumishi aliye Mbeya DC anataka kuhama kumfuata Mwenza wake Chato DC! Unamzungusha asihame!! Unataka ndoa yake ivunjike?
Nina mengi ya kuandika but kwa leo naomba niishie hapa.

Mods please msiunganishe uzi huu
 
Mnazuia watu kufuata wenza wao, mnafanya familia ziishi kwa taabu, mnasababisha malezi ya watoto kuwa compromised. Badilikeni, Mungu atawalaani
 
Hii serikali ndugu haina utu katika lolote, kama wanaweza kuua maelfu ya watu halafu wanajikausha kama hakuna kilichotokea ndio ujue hakuna wanachojali.

Kazi ya HR yeyote ni kuhakikisha demand na supply ya Human resource inabalance,Hakuna sababu yoyote ya kuzuia mtumishi kuhama kwa sababu za ajabu zinazotolewa, kwanza inasaidia kuleta brain mpya kwenye maeneo wanayohamia,Inaongeza motivation ya kazi pia

Kumshikilia mtu ambaye akili yake yote inawaza familia yake mda wate inashusha ari ya kazi hata ufanisi hauwi mzuri, ndio maana watu wanaingia kusaini wanaenda kutafuta supu akirudi saa nne ishafika anafanya kazi saa 2 anaenda lunch akirudi karibu muda wa kutoka, anajibu wateja anavyojisikia, halafu bado unahesabu una mtumishi hapo.

Ma HR wanashindwa nini kutengeneza Forum ambapo kila halmashauri au idara Inaweka wazi kada inazohitaji kuhamia,kwamba mtumishi akitaka Kuhama anaingia humo kuangalia anajua kabisa nahitajika huko na huku anakoondoka wanajua kabisa kwamba akiondoka kuna mtumishi wa kada yake tunamkubalia anakuja kujaza nafasi.
Hapo kazi ya HR inakua kuangalia kipaumbele tu nani tumpe uhamisho kwanza mwingine asubiri kutokana na unyeti wa sababu.

Mahitaji ya kuhama hayataisha kamwe na ni haki ya mtumishi na kuzuia yana madhara sana ila sababu sio tangible hakuna anayejali, hata huu wizi na udokozi sometimes ni retaliation za watumishi tu kunyimwa haki zao anaona bora niibe tu kumkomoa mwajiri.
 
Hii serikali ndugu haina utu katika lolote, kama wanaweza kuua maelfu ya watu halafu wanajikausha kama hakuna kilichotokea ndio ujue hakuna wanachojali.

Kazi ya HR yeyote ni kuhakikisha demand na supply ya Human resource inabalance,Hakuna sababu yoyote ya kuzuia mtumishi kuhama kwa sababu za ajabu zinazotolewa, kwanza inasaidia kuleta brain mpya kwenye maeneo wanayohamia,Inaongeza motivation ya kazi pia

Kumshikilia mtu ambaye akili yake yote inawaza familia yake mda wate inashusha ari ya kazi hata ufanisi hauwi mzuri, ndio maana watu wanaingia kusaini wanaenda kutafuta supu akirudi saa nne ishafika anafanya kazi saa 2 anaenda lunch akirudi karibu muda wa kutoka, anajibu wateja anavyojisikia, halafu bado unahesabu una mtumishi hapo.

Ma HR wanashindwa nini kutengeneza Forum ambapo kila halmashauri au idara Inaweka wazi kada inazohitaji kuhamia,kwamba mtumishi akitaka kuhamia anajua kabisa nahitajika huko na huku anakoondoka wanajua kabisa kwamba akiondoka kuna mtumishi wa kada yake tunamkubalia anakuja kujaza nafasi.
Hapo kazi ya HR inakua kuangalia kipaumbele tu nani tumpe uhamisho kwanza mwingine asubiri kutokana na unyeti wa sababu.

Mahitaji ya kuhama hayataisha kamwe na ni haki ya mtumishi na kuzuia yana madhara sana ila sababu sio tangible hakuna anayejali, hata huu wizi na udokozi sometimes ni retaliation za watumishi tu kunyimwa haki zao anaona bora niibe tu kumkomoa mwajiri.
Kwenye kuiba anachoibiwa sana mwajiri ni muda. Mtu akienda likizo ya wiki nne kwa mwenza anajiongezea wiki mbili.
 

Hiyo Sasa Ndio Maana Kamili Ya"Kazi Na Utu"
Ingekuwa "Utu Na Kazi"Ungehama Wallah Wabillah Sheikh....!!
 
Back
Top Bottom