Rais ingilia kati suala la Uhamisho kwa watumishi, tumechoka kuibiwa na Maafisa wa Tamisemi

digba sowey

JF-Expert Member
Mar 1, 2017
7,872
14,294
Wakuu hamjambo,ni matumaini Yangu kuwa hamjambo,mnaendelea na ujenzi Wa taifa kama kawaida.

Naomba twende kwenye hoja Yangu,nimekuwa nikifatilia swala la uhamisho kwa watumishi Wa umma na urasmu uliopo,ni ukweli usiopingika kuwa kuna haja ya Serikali kutoa tamko kuwa uhamisho umefungwa na nikosa kwa mtumishi kuhama au serikali itamke wazi kuwa kuanzia sasa watu wafuate taratibu za uhamisho na waruhusiwe kuhama na kwenda kufanya kazi maeneo wanayopenda wenyewe.

Hii ni kwasabu maofisaa Wa TAMISEMI wamekuwa miungu watu,na wamehodhi zoezi la uhamisho kwa watumishi Wa umma ili kujipatia kipato,ni ukweli usiopingika kuwa usipokuwa na laki nane hadi millioni moja kamwe huwezi kuhama,nina watu wangu wengi tu ambao wamekuwa wakihama bila kufuata taratibu,ila wapo waliokamilisha taratibu mfano uhamisho Wa kubadilishana,mtu kapata mtu Wa kubadilishana vituo vya kazi lakini hapewi ruhusa ya kuhama,lakini kuna wenye pesa ,hawa huhama hata bila kumjulisha mkurungezi ,yaani barua hutoka TAMISEMI moja kwa moja ,kwa vile mkurugenzi hana mamlaka ya kuhoji barua toka juu basi watu hawa huhama,kituoni kwangu kuna watumishi wawili walihama baada ya kutoa kitu kidogo kwa maafisaa Wa TAMISEMI na kuhama,huku wapo wengi tu ambao wamekamilisha vigenzo vya kuhama lakini hawapewi vibari vya kuhama.

Nashauri rais wetu mpendwa atoe tamko, watumishi waanze kuhama mara moja ili kuepusha huu utapeli unaofanywa na watumishi Wa TAMISEMI,Na hii itasaidia kuamuasha Ari na morali ya watumishi Wa umma, maafisaa wanawaibia wananchi ,ili khali pesa ni ngumu kuipata ,hebu fikiria kununua haki yako kwa milioni moja na kwenda kushibisha Tumbo la jamaa huku ukiacha familia yako ikilalama kwa shida

Naimani kubwa kabisa kuwa waziri husika na rais watatoa tamko ili kuacha nafasi kwa watumishi waliokidhi vigezo wawezi kuhama.

#kaziIendelee.
 
Tatizo hii nchi matamko mengi ufuatiliaji sufuri ndiyo maana watu wanapuyangapuyanga tu.
 
Mkuu, umeanzia juu sana hali ni mbaya kuanzia halmashauri wakurugenzi wanajitungia viutaratibu vya hovyo na kugoma kusaini barua za watumish mouaka watakapojisikia wao.

Mtu alie haribu zoezi la uhamisho ni waitara bichwa baya na makatibu wakuu wake kish kuzalisha upenyo wa rushwa huku Jiwe aka mwendazke akifumbia macho watumishi wakiteseka kukaa mbali na wake/waume zao au afya mbovu.

Ngoja mama apige chini baadhi ya wakurugenzi ili wajue kuwa cheo ni dhamana.

Mi nina matumaini na Umi mwalimu, ameisha ambiwa tamisemi ni jalala la mafisadi na wala rushwa kuna mkurugenzi akipigwa chini nitanunua nyama niikange nijichane maana anajifanya mungu mtu.
 
Safi brother. You are coming to ur senses..
Tungekuwa pamoja hivi tangu awali hakika tulishafika mbali sasa.
 
Serikali yangu ya jiwe ya awamu ya 5 imemaliza ukiritimbaaaaaaa.

Nasema hivi mambo ya uhamisho kwa wafanyakazi ni marufuku, wafanyakazi chapeni kazi ikishindikana acha kazi.

KAZI INAENDELEAAAAA...
 
Kwani wewe unataka kuhamia wapi mkuu
Laki nane wape tu au unasubiri rais wa Wanyonge arudi?
 
Watu wanahama mkuu,Jana majina 2000+ yametoka

Sent from my TECNO KB7j using JamiiForums mobile app
Wanapewa na hela zao? Au ndo wanahama tu mwisho wa siku serikali ijikute na malimbikizo ya madeni? Namkumbuka Magu aliwaambia wakurugenzi ukisaini uhamisho basi umpe na hela yake hapohapo unaemuhamisha maana serikali ilikuwa inadaiwa mno kutokana na kuhama ovyo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu, umeanzia juu sana hali ni mbaya kuanzia halmashauri wakurugenzi wanajitungia viutaratibu vya hovyo na kugoma kusaini barua za watumish mouaka watakapojisikia wao.

Mtu alie haribu zoezi la uhamisho ni waitara bichwa baya na makatibu wakuu wake kish kuzalisha upenyo wa rushwa huku Jiwe aka mwendazke akifumbia macho watumishi wakiteseka kukaa mbali na wake/waume zao au afya mbovu.

Ngoja mama apige chini baadhi ya wakurugenzi ili wajue kuwa cheo ni dhamana.

Mi nina matumaini na Umi mwalimu, ameisha ambiwa tamisemi ni jalala la mafisadi na wala rushwa kuna mkurugenzi akipigwa chini nitanunua nyama niikange nijichane maana anajifanya mungu mtu.
Naona huyo Ummy nae amezidisha tatizo eti watu wasihamie majiji na manispaa. Aibu kubwa mabega yapo juu TAMISEMI imevamiwa
 
Mkuu, umeanzia juu sana hali ni mbaya kuanzia halmashauri wakurugenzi wanajitungia viutaratibu vya hovyo na kugoma kusaini barua za watumish mouaka watakapojisikia wao.

Mtu alie haribu zoezi la uhamisho ni waitara bichwa baya na makatibu wakuu wake kish kuzalisha upenyo wa rushwa huku Jiwe aka mwendazke akifumbia macho watumishi wakiteseka kukaa mbali na wake/waume zao au afya mbovu.

Ngoja mama apige chini baadhi ya wakurugenzi ili wajue kuwa cheo ni dhamana.

Mi nina matumaini na Umi mwalimu, ameisha ambiwa tamisemi ni jalala la mafisadi na wala rushwa kuna mkurugenzi akipigwa chini nitanunua nyama niikange nijichane maana anajifanya mungu mtu.
Yupo mungumtu mmoja alikua tanga ameliwa kichwa kwasasa nasikia anasomatu magazeti kwa katibu tawala.
Alijifanya ametoka kanda fulani akafanya alivyotaka ila Mungu ametenda
 
Utumishi kuhama ni simpo sana..konekisheni na mzigo mezani..ukijua hizi sheria hata ikulu utahamia kutokea huko nanyamba.

Ummy anademka tu.

#MaendeleoHayanaChama
 
Yupo mungumtu mmoja alikua tanga ameliwa kichwa kwasasa nasikia anasomatu magazeti kwa katibu tawala.
Alijifanya ametoka kanda fulani akafanya alivyotaka ila Mungu ametenda
Mkuu mtaje jina na cheo chake cha awali kabla ya kutumbuliwa ili tumjue huyo aliyekuwa Mungu mtu.Ahsante.
 
Wakuu hamjambo,ni matumaini Yangu kuwa hamjambo,mnaendelea na ujenzi Wa taifa kama kawaida.

Naomba twende kwenye hoja Yangu,nimekuwa nikifatilia swala la uhamisho kwa watumishi Wa umma na urasmu uliopo,ni ukweli usiopingika kuwa kuna haja ya Serikali kutoa tamko kuwa uhamisho umefungwa na nikosa kwa mtumishi kuhama au serikali itamke wazi kuwa kuanzia sasa watu wafuate taratibu za uhamisho na waruhusiwe kuhama na kwenda kufanya kazi maeneo wanayopenda wenyewe.

Hii ni kwasabu maofisaa Wa TAMISEMI wamekuwa miungu watu,na wamehodhi zoezi la uhamisho kwa watumishi Wa umma ili kujipatia kipato,ni ukweli usiopingika kuwa usipokuwa na laki nane hadi millioni moja kamwe huwezi kuhama,nina watu wangu wengi tu ambao wamekuwa wakihama bila kufuata taratibu,ila wapo waliokamilisha taratibu mfano uhamisho Wa kubadilishana,mtu kapata mtu Wa kubadilishana vituo vya kazi lakini hapewi ruhusa ya kuhama,lakini kuna wenye pesa ,hawa huhama hata bila kumjulisha mkurungezi ,yaani barua hutoka TAMISEMI moja kwa moja ,kwa vile mkurugenzi hana mamlaka ya kuhoji barua toka juu basi watu hawa huhama,kituoni kwangu kuna watumishi wawili walihama baada ya kutoa kitu kidogo kwa maafisaa Wa TAMISEMI na kuhama,huku wapo wengi tu ambao wamekamilisha vigenzo vya kuhama lakini hawapewi vibari vya kuhama.

Nashauri rais wetu mpendwa atoe tamko, watumishi waanze kuhama mara moja ili kuepusha huu utapeli unaofanywa na watumishi Wa TAMISEMI,Na hii itasaidia kuamuasha Ari na morali ya watumishi Wa umma, maafisaa wanawaibia wananchi ,ili khali pesa ni ngumu kuipata ,hebu fikiria kununua haki yako kwa milioni moja na kwenda kushibisha Tumbo la jamaa huku ukiacha familia yako ikilalama kwa shida

Naimani kubwa kabisa kuwa waziri husika na rais watatoa tamko ili kuacha nafasi kwa watumishi waliokidhi vigezo wawezi kuhama.

#kaziIendelee.
pole sana mkuu, ila tatizo watu wana roho mbaya kuliko hata wanyama, sio TAMISEMI TU ni kila mahala kuna mashetani.
labda Yesu arudi.
 
Back
Top Bottom