Klabu ya Simba yatakiwa kuomba radhi kwa tukio linalodaiwa kudhalilisha watu wenye ualbino kwenye tamasha lao

Nyakijooga

Senior Member
Dec 9, 2018
123
202
Chama cha Watu wenye ualbino Tanzania (TAS) na Kituo cha Sheria na haki za binadamu (LHRC), wamelaani vikali kitendo kinachodaiwa kufanyiwa siku ya Augosti 6, 2023 siku ya 'Simba Day' kumtumia mtu mwenye ualbino mithili ya mtu aliyekuwa katika hali ya nusu utupu na aliyevaa nepi ya mkojo jukwaani mbele ya kadamnasi ya maelfu kwenye uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam.

Wadau hao ambao wamekuwa wakitetea haki za watu wenye ulemavu wamedai kuwa tukio la aina hiyo ambalo wamedai ni udhalilishaji lilijitokeza kwenye tamasha la Simba Day mwaka jana 2022, ambapo Klabu ya Simba walidaiwa kutumia jeneza, msalaba na kumnasibu mtu mwenye Ualbino kama msukule.

Kufuatia mfululizo wa vitendo hivyo wamedai kuwa vinatweza utu wa watu wenye ualbino nchini na kuwa vinapelekea kuwepo kwa mjadala mingi katika jamii ikiwemo kwenye mitandao ya kijamii inayoonesha dhihaka kwa watu wenye ualbino kinyume na haki za binadamu.

Katika tamko lao ambalo wamelitoa leo Augosti 9, 2023 wamesisisitiza kuwa katika jamii nyingi watu wenye ualbino wamekuwa wahusishwa na mila na tamaduni mbaya zinazotweza utu wao, hivyo wamedai kuwa kuendelea kwa vitendo hivyo ni kudidimiza juhudi za Serikali, Mashirika ya Watetezi wa Haki za Binadamu na wadau binafsi wanaoelimisha jamii kuhusu ualbino.

Wadau hao wametoa wito kwa kuitaka klabu ya Simba kuomba radhi kwa watu wenye ualbino na umma wa watanzania kwa vitendo vinavyodaiwa kutweza utu wa watu wenye ualbino na wameiomba Serikali pamoja na Shirikisho la soka Tanzania (TFF) kusimamia jambo hilo.

Wamesisitiza kuwa klabu ya Simba wasipoitikia wito huo unaowataka kuomba radhi watachukua kwenye vyombo vya kisheria.

LHRC 1.PNG

LHRC 2.PNG
 

Attachments

  • Kulaani_matukio_ya_udhalilishaji_wa_utu_wa_watu_wenye_ualbino.pdf
    134.6 KB · Views: 1
Chama cha atu wenye Ualbino Tanzania (TAS) na Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu wameitaka klabu ya Simba kuomba radhi kwa tukio waliloita la udhalilishaji.

Tukio hilo lilitokea Agosti 6, 2023 kwenye sherehe ya tamasha la siku ya Simba yaliyofanyika uwanja wa Taifa wa Benjamini Mkapa jijini hapa kwa kumpandisha mtu mwenye ulemavu wa ngozi akiwa amevishwa taulo ya watoto (baby diaper).

Msemaji wa Simba Ahmed Ally alipoulizwa kwa simu leo, amesema wamesikia na wapo tayari kufanya hivyo.

β€œWamesema tuombe radhi? Basi sawa. Kwa sasa tuko busy na mechi ya kesho, akili yetu yote ipo kwa kwa ajili ya kesho. Haya mambo mengine tukianza kujibu tutavuruga utaratibu. Nitamuuliza CEO tuone tunafanya nini,” amesema.

Maoni yangu: mbunifu wa Simba sc katika matamasha hafai na hafai kabisa kiufupi anaichafua taasisi hii kwa kudhani kuwa anawafurahisha watu kumbe anadharirisha watu.

Hilo linapaswa kukemea kwa hali na Mali Tena kwa sauti kuu katika mpira wetu huu Tanzania.
 
Hata wabunge wanachama wa Simba wanapenda Sana kutumia majeneza Kwenye Mikutano yao

Simba ni Wachawi Wachawi Sana yule mchezaji wao Hussein Tindwa wallazimisha kubeba hirizi akafia uwanjani

Makolo Wana Unyani mwingi πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ”₯
 
Moderator weka mnawafurahisha fanyeni haraka kuedt vichwa vya habari maana imekua kero sana kuedt mpaka mnachukua siku mbili



Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
Lakini na wewe ulipaswa kuwa na utulivu,ukahakikisha makosa kwa kichwa cha habari hayapo.Hakukuwa na sababu ya kukimbilia kupost na makosa mengi kisha lawama uwatupie Moderators kwa kuchelewa ku edit makosa yako ya uandishi.
 
Hao wenye Ualbino kwao Ruksa kutania na kudhalilisha wenzao wakitaniwa wao ni kosa! Hili nalo mkalitizameπŸ“Œ
 
Lakini na wewe ulipaswa kuwa na utulivu,ukahakikisha makosa kwa kichwa cha habari hayapo.Hakukuwa na sababu ya kukimbilia kupost na makosa mengi kisha lawama uwatupie Moderators kwa kuchelewa ku edit makosa yako ya uandishi.
Wanakosea BBC na CNN na wanakuambia kumradhi Mimi Nani nisikosee.

Jikite kwenye hoja.

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
π”Έπ•π•“π•šπ•Ÿπ•  π•Ÿπ•š π•“π•šπ•Ÿπ•’π••π•’π•žπ•¦ π•‘π•šπ•’ π•œπ•  π•’π•Ÿπ•’π•¨π•–π•«π•’ π•—π•’π•Ÿπ•ͺ𝕒 𝕝𝕠𝕝𝕠π•₯𝕖 π•Ÿπ•’ π•šπ•œπ•’π•¨π•’ π•œπ•’π•¨π•’π•šπ••π•’ π•₯𝕦 π•žπ•«π•–π•–...vipi kama angekua mtu wa kawaida?je mngehoji?basi wasipwe fursa maana wakipewa wanasema ni udhalilishaji.
 
Back
Top Bottom