Kiwanja au Biashara

Kiwanja au Biashara

Gawa iyo ela katikati nunua kiwanja nusu ingine endelea kudunduliza hadi ifikie lengo lako kununua kiwanja kwa ajili ya kujenga ni kuzika pesa kwahiyo inatakiwa uzike pesa iliyokufa kwa maana ambayo haina kazi au ambayo hata isipokuwepo huwezi ijutia

Lakini pia ukinunua kiwanja huwezi jenga Leo wala kesho ukamaliza otherwise ujenge kijumba tu cha kujistiri chumba kimoja na sebule iyo ela unaweza tosha tofauti na hapo lazima ufanye biashara na kazi nyingine ili upate ela ya kujengea
 
Nakupa mfano mmoja:-
Benki iliamua kuwapa mkopo bwana A, na bwana B; kila mmoja kiasi cha milioni 5, na kila mmoja alitakiwa kuzirejesha pesa hizo baada ya miaka 2.​
  • Bwana A aliamua kuwekeza pesa zile kwenye biashara yake ya uuzaji wa bia na soda; kwa sababu bidhaa alizokuwa auza si za kuharibika, aliweza kuziuza na kupata faida.​
  • Bwana B aliamua kuchukua pesa ile na kununua kiwanja, bila kufanya uzalishaji wowote.​
Muda wa marejesho ulipofika, bwana A aliweza kurudisha na kubaki na faida, ila bwana B hakuwa na pesa ya kurudisha zaidi ya kile kiwanja; kutokana na kutakiwa kurudisha lile deni kwa haraka, ilibidi bwana B auze kile kiwanja kwa bei ya hasara ili aweze kurejesha mkopo.

Swali; Je, Bwana A na Bwana B ni nani aliyetumia akili zaidi?​
Hapa Kuna taarifa haujatupatia. Hawa jamaa walikuwa na kipato kingine kabla hawajachukua huo mkopo. Hiki ndo kiliwaaminisha bank kuwa wataweza kurejesha hiyo mikopo. Je chanzo Cha bwana B Cha mapato kiliyumba? Hata kama mkopo ni WA miaka 2 unatakiwa kurudisha kidogo kidogo either Kila wiki ama mwezi. Naamini labda bwana B chanzo chake kilipata shida ndo maana aliuza kiwanja. Bwana A anabahati biashara yake ilienda pouwa. Hujawahi ona watu biashara wanafunga? Sio Kila mtu anaweza Fanya biashara ni kipawa/ passion kama zilivyoshughuli nyingine kama kilimo au ku beti
 
Habarini wana JF poleni na majukumu ya kila siku. Moja kwa moja ningependa kwenda kwenye maada kama kichwa cha habari kinavyojieleza.

Mimi ni kijana mwenye familia ya mke na mtoto mmoja nayeendelea kupambana kila kukicha katika kibarua changu chenye malipo ya kawaida.

Nimekuwa napata shida kuamua katika jambo ambalo litafaa zaidi kwangu kuanza nalo kuendelea na hatua za mbele, kwa muda nimekuwa nikijikusanya kutafuta kiasi cha pesa ambacho nitakitumia kuanzisha biashara niliyoipanga kuanza nayo kama nitafanikiwa kufikia mtaji wa kuanza nao niliouona utatosha, wazo limekuwa siyo rahisi sana sababu kama mjuavyo maisha yetu ya kitanzania huwa hayajanyooka kwa kiasi hicho japo siyo kwa wote, unaenda hatua sita mbele changamoto inatokea unarudi tena hatua mbili nyuma.

Kiasi cha mtaji nlioupanga nishafikisha nusu mpaka sasa na nusu nyingine inaweza chukua si chini ya miezi mitano mbele.

Kuna muda nakuwa naona kama muda wa kufikia kiasi cha pesa lengwa unaweza ukaongezeka tofauti na malengo au nikapata changamoto mbele nikarudi nyuma zaidi ndiyo napata wazo labda ninunue kwanza kiwanja halafu malengo yangu nianze upya.

Hela iliyopo inaweza tosha kiwanja.
Ningependa kupokea ushauri kwa mtu aliyewahi pitia hii hali au kwa yeyote mwenye mawazo ya kujenga anisaidie kunipa uelekeo utakaofaa. Ahsanteni na karibuni
Yote sawa Mkuu, kiwanja Huwa hakishuki bei,na biashara ukienda vizuri tunanunua kiwanja na viwanja,pia ukianza na kiwanja, biashara ikidoda unauza kiwanja biashara inaendelea!Kwa hiyo inategemea na moyo wako unataka Nini!
 
Habarini wana JF poleni na majukumu ya kila siku. Moja kwa moja ningependa kwenda kwenye maada kama kichwa cha habari kinavyojieleza.

Mimi ni kijana mwenye familia ya mke na mtoto mmoja nayeendelea kupambana kila kukicha katika kibarua changu chenye malipo ya kawaida.

Nimekuwa napata shida kuamua katika jambo ambalo litafaa zaidi kwangu kuanza nalo kuendelea na hatua za mbele, kwa muda nimekuwa nikijikusanya kutafuta kiasi cha pesa ambacho nitakitumia kuanzisha biashara niliyoipanga kuanza nayo kama nitafanikiwa kufikia mtaji wa kuanza nao niliouona utatosha, wazo limekuwa siyo rahisi sana sababu kama mjuavyo maisha yetu ya kitanzania huwa hayajanyooka kwa kiasi hicho japo siyo kwa wote, unaenda hatua sita mbele changamoto inatokea unarudi tena hatua mbili nyuma.

Kiasi cha mtaji nlioupanga nishafikisha nusu mpaka sasa na nusu nyingine inaweza chukua si chini ya miezi mitano mbele.

Kuna muda nakuwa naona kama muda wa kufikia kiasi cha pesa lengwa unaweza ukaongezeka tofauti na malengo au nikapata changamoto mbele nikarudi nyuma zaidi ndiyo napata wazo labda ninunue kwanza kiwanja halafu malengo yangu nianze upya.

Hela iliyopo inaweza tosha kiwanja.
Ningependa kupokea ushauri kwa mtu aliyewahi pitia hii hali au kwa yeyote mwenye mawazo ya kujenga anisaidie kunipa uelekeo utakaofaa. Ahsanteni na karibuni
Kwanini Ulioa? KATAA NDOA
 
Back
Top Bottom