Kiwanja au Biashara

Kiwanja au Biashara

Habarini wana JF poleni na majukumu ya kila siku. Moja kwa moja ningependa kwenda kwenye maada kama kichwa cha habari kinavyojieleza.

Mimi ni kijana mwenye familia ya mke na mtoto mmoja nayeendelea kupambana kila kukicha katika kibarua changu chenye malipo ya kawaida.

Nimekuwa napata shida kuamua katika jambo ambalo litafaa zaidi kwangu kuanza nalo kuendelea na hatua za mbele, kwa muda nimekuwa nikijikusanya kutafuta kiasi cha pesa ambacho nitakitumia kuanzisha biashara niliyoipanga kuanza nayo kama nitafanikiwa kufikia mtaji wa kuanza nao niliouona utatosha, wazo limekuwa siyo rahisi sana sababu kama mjuavyo maisha yetu ya kitanzania huwa hayajanyooka kwa kiasi hicho japo siyo kwa wote, unaenda hatua sita mbele changamoto inatokea unarudi tena hatua mbili nyuma.

Kiasi cha mtaji nlioupanga nishafikisha nusu mpaka sasa na nusu nyingine inaweza chukua si chini ya miezi mitano mbele.

Kuna muda nakuwa naona kama muda wa kufikia kiasi cha pesa lengwa unaweza ukaongezeka tofauti na malengo au nikapata changamoto mbele nikarudi nyuma zaidi ndiyo napata wazo labda ninunue kwanza kiwanja halafu malengo yangu nianze upya.

Hela iliyopo inaweza tosha kiwanja.
Ningependa kupokea ushauri kwa mtu aliyewahi pitia hii hali au kwa yeyote mwenye mawazo ya kujenga anisaidie kunipa uelekeo utakaofaa. Ahsanteni na karibuni

Nunua Kiwanja, ila usijegenge; Kama Bado utakuwa na passion ya biashara, unaweza kiuza baadae kwa faida ukafikiq malengo
 
Hela iliyopo inaweza tosha kiwanja.
Ningependa kupokea ushauri kwa mtu aliyewahi pitia hii hali au kwa yeyote mwenye mawazo ya kujenga anisaidie kunipa uelekeo utakaofaa. Ahsanteni na karibuni
Kama kipato chako ni cha uhakika, hiyo hela uliyo nayo ifanye mtaji wa kuanzia. Anza biashara mdogo mdogo. Ukiona mwenendo wa biashara unaridhisha, tafuta Microfinance nenda ukope kiasi cha kujazilizia huo mtaji wako. Endelea na biashara huku unalipa mkopo na ukipata hela za ziada pia zitumie kulipa mkopo ili umalize mapema. Ukimaliza kulipa unakopa tena unapanua biashara
 
Nakupa mfano mmoja:-
Benki iliamua kuwapa mkopo bwana A, na bwana B; kila mmoja kiasi cha milioni 5, na kila mmoja alitakiwa kuzirejesha pesa hizo baada ya miaka 2.​
  • Bwana A aliamua kuwekeza pesa zile kwenye biashara yake ya uuzaji wa bia na soda; kwa sababu bidhaa alizokuwa auza si za kuharibika, aliweza kuziuza na kupata faida.​
  • Bwana B aliamua kuchukua pesa ile na kununua kiwanja, bila kufanya uzalishaji wowote.​
Muda wa marejesho ulipofika, bwana A aliweza kurudisha na kubaki na faida, ila bwana B hakuwa na pesa ya kurudisha zaidi ya kile kiwanja; kutokana na kutakiwa kurudisha lile deni kwa haraka, ilibidi bwana B auze kile kiwanja kwa bei ya hasara ili aweze kurejesha mkopo.

Swali; Je, Bwana A na Bwana B ni nani aliyetumia akili zaidi?​
 
Back
Top Bottom