Kituo cha Mabasi Ubungo kutokuhamishwa

Kituo cha Mabasi Ubungo kutokuhamishwa

Halafu siku hizi hakuna bawacha hata mmoja mwenye adabu make hata wewe umekuwa mbugila kabisa.



Hawa jamaa wanashida kubwa,wameacha fungu hilo ili litumike kuwatawanya wale wajumbe 11 kuzunguka Nchi nzima ili kuwarubuni waNEC watakaompigia kura Mr x
 
wanataka ihame ili Vienna vyao viongezeke thamani...
 
Tatizo mipango mibovu ndio inagharimu miradi mingi hapa nchini kutofanyika kwa mafanikio makubwa na kudorola mfano mzuri soko la karume "machinga complex"
 
ndio maana baadhi yetu tulipendekeza wakuu wa mikoa na mameya wachaguliwe moja kwa moja na wananchi ili wawajibike kwao sio kwa wanasiasa. nani anawasemea watu wa Dar
 
Ni katika taarifa ya habari ya saa 2 usiku, Meya wa jiji la Dar katoa tamko kuwa kituo cha Mabasi Mikoani na nchi jirani cha Ubungo hakitahama.

Sababu kuu ni ukosefu wa hela. Hela waliyotarajia kuendeleza kituo kipya cha Mbezi zilipelekwa kwenye mradi wa mabasi yaendayo kasi (DART).

Chanzo: ITV

SWALI: Je, jiji kuvunja vibanda na miundo mbinu ya Ubungo huku wakijua hawana fedha za kukihamisha si dhuluma, au ni ulimbukeni na kukurupuka?
Fedha wanayokusanya ubungo ni nying sana, wanapeleka wapi?
 
Mwone huyu naye, wewe un as ona sawa tu walicjofanya? Kuvunja kiyuo jalaf leo unasema juna hela za kukigamisha,Pumbaf!

sijaelewa hapa, inaonekana keyboard yako haina baadhi ya herufi...
 
Mmawia.....kwa upeo wangu Azam anao uwezo mzuri wa kifedha,isitoshe anao uzoefu katika nyanja ya usafirishaji,anao wataalamu wa kigeni ambao ni wazuri ktk logistics za usafirishaji.Hayo ni mawazo yangu tu na niko tayari kusahihishwa kama nitakuwa nimekosea.Kilimanjaro hali kadhalika yuko serious ktk nyanja hii ya usafirishaji hali kadhalika scandanavia

Mkuu Scandinavia alishajifia zamani sana.
 
Hizo pesa zitakuwa zimeliwa tu haiwezekani eti zimepelekwa DART wakati nayo ina bajeti yake.
 
ukishaona hivyo washapata mwekezaji hapo, kutajengwa vibanda vipya na maduka mapya na watu wataanza kupangswa upya,
by the way hii si mali ya UDA pia?
 
Lakini wakuu, dizaini kama kuna pesa zilitengwa kwa ajili ya "kuhamisha" hiyo kitu UBT. Sasa zoezi limesitishwa, je mapene yatarejeshwa? Au ndo yale yaliyotumika kuhonga laki nane nane ya "heri ya Krismas" kwa wajumbe wote wa NEC(CCM) Taifa? Tumepigwa tena!
 
Kwani diwani na mbunge wa ubungo wapo au wapo likizo kuna mengi yatafanyika hapa,mdudu rushwa ataingia sehemu yake,tatizo mnyika hana msaidizi,diwani wake ana kazi kuu ya kuongea ila utekelezaji ni zero,hata hili suala halijui.Dah maskini chadema mnakimbizwa bila kujitambua.
 
Atakuwa anafikria kwa kutumia
11001797_698245036951278_1774318577912669736_n.jpg


yeye mwenyewe, haiwezekani kiongozi ahalibu mazingira na kupoteza pesa za walipa kodi na kuishia kuomba samahani tu.
 
Mawazo yangu tu....kituo kibinafsishwe kwa mwekezaji wa ki Tanzania mwenye taaluma ya usafirishaji.Awe na uwezo wa kukijenga na kukiendesha..Taboa kama wamejipanga wanastahili kupewa nafasi ya kwanza,Scandanavia express,kilimanjaro bus,azam hao wafikiriwe kama Taboa hawatakuwa tayari.

Nalikubali wazo isipokuwa sio lazima awe mwenye taaluma ya usafirishaji, bali awe na uwezo wa kuwekeza kwenye biashara hiyo. Hao wengine huwa ni waajiriwa tu, wapo wengi wenye taaluma mbalimbali.
 
Jimbo ni la chama gani......??? Kila kitu ccm acheni mawazo mgando

Hiyo ndio kete ccm inataka kutumia kuvichafua vyama pinzani? Kwani fedha serikali iliikabizi kwa nani hata ameikula? Unafikiri chama pinzani kingekuwa kimevurunda hapa kungekuwa kimya hivi? CCM msikwepe kuwajibika semeni nani kala hizo fedha, hao mwendo kasi walikuwa na fungu lao, hizi za kituo cha mabasi ya mkoa mbezi alikabidhiwa nani?
 
Nilivyomuona Mh. Massaburi akiongelea jinsi walivyo divert US $100 kuzipeleka kwenye mradi wa mabasi yaendayo kasi ndio nikakumbuka wakati fulani JK alivyokuwa akipokea msaada wa US $800,000 (laki nane) siku moja Marekani.
Yaani raisi anaweza kwenda kupokea msaada kama huo lakini dola 100m zinaelekezwa kwenye mradi mwingine bila hata ya maelezo! Hii nchi hata tukipewa nini bila ya kubadilika au kuwabadilisha watawala hawa haiwezi kupia hata hatua moja katu!
 
Back
Top Bottom