Kituo cha Mabasi Ubungo kutokuhamishwa

Kituo cha Mabasi Ubungo kutokuhamishwa

Hayo tuliyategemea hasa baada kujengwa kwa ofisi mpya za kukatishia tiketi.

Hili ni jambo limelazimishwa baada ya kuona wametumia fedha nyingi kujenga daraja la kifahari pale ubungo stendi ya mkoa, sasa kubakiza kituo pale ni kujaribu kuficha pumba walizofanya za hilo daraja. Wanaogopa wakati wa uchaguzi wangelipuliwa maana ingeonekana daraja la kifahari lakini halitumiki. CCM na serikali yao wamerogwa maana hata wasomi walioko huko wanafanya mambo kama wendawazimu.
 
Hiyo ndio kete ccm inataka kutumia kuvichafua vyama pinzani? Kwani fedha serikali iliikabizi kwa nani hata ameikula? Unafikiri chama pinzani kingekuwa kimevurunda hapa kungekuwa kimya hivi? CCM msikwepe kuwajibika semeni nani kala hizo fedha, hao mwendo kasi walikuwa na fungu lao, hizi za kituo cha mabasi ya mkoa mbezi alikabidhiwa nani?
Nimekusoma mkuu TGInnocent, inawezekana Mh. Masaburi kakiri kwa kujua kuwa hii siri isingeliweza kuendelea kufichika na kaona kila mhusika anajifanya kukaa kimya. anajua kuwa Mh. Mnyika atalitolea ufafanuzi usio na walakini hilo swala, all in all kuwajibika hapa ni lazima hata kama hawa jamaa hawana utamaduni huo!

 
Tatizo ni siasa kuingilia taaluma za watu, mambo yanakwenda kulingana na Matakwa (o) ya wanasiasa.Kwani hawakufanya tahmini kabla ya kuanza mipango ya kukihamisha?? Poor tz
Nchi ya magumashi hii jomba, nikwambie kitu hakikisha unakitambulisho cha kupiga kura alafu uwatandike ambao unaona hawafai.
 
Pamoja na matatizo mengi ila Mkapa kwa kiasi chake alijitahid. Wakat ule stend zilikuwa ovyo kabisa pale kisutu na mnaz mmoja. Hata hivyo wasanii wakaja na mirad ya ujanja ujanja na kuvunja kituo kabla ya uhakika wa fedha. Matokeo yake ni hasara kwa Taifa. Pili ni adha ambayo wasafir wameipata katika kipindi cha miaka miwili bila ya sehem ya abiria na shida ya washroom. Lakin cha ajab ushuru ulitozwa kama kawaida wakat huduma zilifutwa, ni ajab kwa kweli!

Wakwere wasipewe tena uongozi wa kitaifa kwa sababu hawana vision pana.
 
Kwahyo mpango wa kuhamishia stend ya mkoa mbezi mwisho kwisha kazi
Kila ukiangalia lile daraja walilojenga pale la wavuka kwa miguu inabidi ucheke, kwa maana KONOIKE walishatujengea la kwanza pale Manzese na tuli proof kuwa hii kitu kwa mswahili ni ngumu kutumika lakini wanarudia yaleyale.
Yaani kwa ccm ukiwasikiliza mipango yao utadhani wanaona mbele kwa miaka mia lakini practically plans zao zinaona si zaidi ya miezi sita sana sana mwaka mmoja wakijitahidi! Never trust these creatures.

 
Kihalisia central hub ya usafiri inatakiwa iwe katikati ya mji! Then unalink njia zote hapo! Train na town buses! Sasa ubungo ndio perfect location! Train ya mwakiembe, bus za dart na up country busses! Sijui walitumia akili gani kufanya huo uamuzi ulioshindikana

Wewe ccm fikiria jiji la miaka 50 ijayo, umejifungia chumbani kwako bado unawaza dsm kama kijiji. Unatambua hizo adha wanazozipata wasafiri ubungo kwa sasa? Baadhi ya sababu kwa nini isiwe ubungo
1. Ni pafinyu hapakidhi uwingi wa mabasi yaliyopo na yajayo
2. Kuna mitambo mingi ya gesi jirani na kituo, ni hatari kwa wasafiri na mitambo yenyewe
3. Ubungo sio katikati ya jiji, pale crock tower ndio centre ya jiji kwa ramani ya dar, labda sasa stesheni ya reli ya kati iunganishwe na stend ya mabasi
4. Miundo mbinu ya ubungo (especially barabara) imezidiwa kwa msongamano, pia vituo vya daladala vimewekwa mbali na stendi, mfano vya kuelekea buguruni au mwenge. Mbezi pana kituo cha daladala jirani na kuna barabara zinazo tawanyika pande zote nne za dsm

Mmechemka hapo
 
Kwa kumbukumbu zangu, huu mradi umefeli Kwa sababu wafadhili wamegoma kutoa fedha ya kufinance huu mradi!

Wahisani wanataka stand ibaki pale pale UBUNGO, jiji wanataka ihame kutoka ubungo kuipeleka wapotaka!

Msisingizie wafadhiri, mmekula fedha nyie. Kwa nini kituo cha mbezi hakikuanza kutengenezwa mara tu fungu lilipotengwa mpaka mkasubiri barabara za mwendo kasi (a scapegoat)?
 
Msisingizie wafadhiri, mmekula fedha nyie. Kwa nini kituo cha mbezi hakikuanza kutengenezwa mara tu fungu lilipotengwa mpaka mkasubiri barabara za mwendo kasi (a scapegoat)?

Hapana mkuu!
Uhusiano kati ya mimi na hao unaosema wamekula hela ni sawa sawa kabisa na uhusiano kati ya wewe na wale wehu wa BMK Dodoma!
 
Afadhari ujenzi kushindikana. Kuhamisha UBT ilikuwa ni kiama kwa walalahoi
 
wote waliohusika kukibomoa wakamatwe kabla hakujakucha , hatuwezi kuvumilia upuuzi huu .
sina hakika kama meya hatakanusha tena hayo aliyoyasema. Kama kituo hakitaondoka pale siamini kama huu mradi tunaoambiwa wa magari yaendayo kasi kama utafanya kazi kama ulivyotegemewa. Tumekuwa tukiambiwa kwamba pale ni kituo kikuu cha magari yaendayo kasi sasa leo Meya anasema kituo cha magari ya mikoani hakitoki, hatuambii kituo cha magari yaendayo kasi kitakuwa wapi. Ni kwamba hawakuwa na mipango au ndio wanataka huo mradi wao wa magari yaendayo kasi uwe white elephant investment?
 
Serikali ya kukurupuka haya ndiyo matokeo yake. For a responsible government nadhani wahusika wangewajibishwa kwa kulitia Taifa hasara. Haiingii akilini unavunja nyumba yako huku ukijua huna uhakika wa kujenga mpya. Ni upuuzi usiopaswa kuvumiliwa hata kidogo.

Nimekuwa nikiingia Ubungo kupokea na kusafirisha ndugu zangu lakini hali ni mbaya sana. Hakuna pahala salama pa mapumziko, hakuna mpangilio wowote na baadhi ya huduma za kijamaii kama dispensary hakuna. Au wasafiri hawana haki ya afya wawapo stand? Vyooni ni aibu tupu lakini charges/ushuru wanachukua.

Kuwa mwanachama wa mshabiki wa ccm ni sawa na mtu aliyetupiwa jini na mtupaji kafa!

Hakuna kinachoniuma kama kulazimishwa kutoa 200 halafu unaishia kukanyaga vumbi na tope. Jiji warudishe 200 za wananchi wanazotoza pale getini kwa lazima
 
Jimbo ni la chama gani......??? Kila kitu ccm acheni mawazo mgando

kwa taarifa kituo cha mabasi cha Ubungo kinasimamiwa na Halmashauri ya Jiji la Dar linaloongozwa na Nstahiki Meya Masburi wa CCM.Na si Manispaa ya Kinondomi.
 
Nalikubali wazo isipokuwa sio lazima awe mwenye taaluma ya usafirishaji, bali awe na uwezo wa kuwekeza kwenye biashara hiyo. Hao wengine huwa ni waajiriwa tu, wapo wengi wenye taaluma mbalimbali.

Wazo lako zuri saana.Wahusika waingie huku wapate ushauri.
 
Nchi ya magumashi hii jomba, nikwambie kitu hakikisha unakitambulisho cha kupiga kura alafu uwatandike ambao unaona hawafai.
Huo ndo mpango, kataa wanasiasa uchwara wote bora ifike mahali kama kuna mtu na jiwe, tuchague jiwe tu liongoze
 
Wewe ccm fikiria jiji la miaka 50 ijayo, umejifungia chumbani kwako bado unawaza dsm kama kijiji. Unatambua hizo adha wanazozipata wasafiri ubungo kwa sasa? Baadhi ya sababu kwa nini isiwe ubungo
1. Ni pafinyu hapakidhi uwingi wa mabasi yaliyopo na yajayo
2. Kuna mitambo mingi ya gesi jirani na kituo, ni hatari kwa wasafiri na mitambo yenyewe
3. Ubungo sio katikati ya jiji, pale crock tower ndio centre ya jiji kwa ramani ya dar, labda sasa stesheni ya reli ya kati iunganishwe na stend ya mabasi
4. Miundo mbinu ya ubungo (especially barabara) imezidiwa kwa msongamano, pia vituo vya daladala vimewekwa mbali na stendi, mfano vya kuelekea buguruni au mwenge. Mbezi pana kituo cha daladala jirani na kuna barabara zinazo tawanyika pande zote nne za dsm

Mmechemka hapo
Hii inaonesha huenda uwezo wako wa kupambanua mambo kuna walakini mkubwa!! au Hujawahi kutoka Nje ya Tanzania! Unatoa suluhisho ambalo Halinamantic Mbele yake!! Kukimbia matatizo sio suluhisho. Katika hali ya kawaida ubungo ndio the most appropriate location!! Kuna njia nyingi za kufanya eneo litoshe!! Kwanza ni kufidia maeneo yanayozunguka gharama ambayo kwa haraka hata 5billion inatosha ikiwa inahusisha na barabara ya kuunganisha hii stendi iliyopo uchochoroni simu 2000! Pia ujenzi wa decka (Overhead packing lot) ujenzi ya kujenga barabara ya juu kutoka stend na kuingia bila kuhusisha ubungo junction.
 
Back
Top Bottom