Viol
JF-Expert Member
- Dec 15, 2009
- 25,426
- 18,228
Dah nakumbuka nilipokuwa mtoto hvi nilikuwa mtundu kimtindo,siku moja mbwa anakatiza mtaani,nikaanza kumfukuza,akisimama na mimi nasimama,akianza kutembea na mimi namfuata,mbwa alipoona namfuatilia sana akageuka na kunikimbiza huku amekenua meno.dah niliogopa yaani moyo ulidunda haraka...nikajisahau nikaanza kumsemehesha huku nakimbilia juu ya mti...''oya acha basi mtu wangu,acha hizo nakutania tu'''kama siyo kupanda juu ya mti leo ningekuwa na jeraha.
Lingine nilienda kwa babu ,pale jirani kwa babu walikuwa wanafunga kondoo,kumbe watoto wa jirani wamefundisha kondoo dume wao kupiga watu kwa kichwa,kwahiyo ukijisahau ukasimama hivyo unakuta kondoo anasogea kinyume nyume hatua kama 15 hivi halafu anakutifua kwa kichwa,akikupata anaweza akakuvunja kiuno au miguu.
Sasa siku moja niliona kama kondoo wamelala halafu nikajisahau,kumbe kondoo akaamka taratibu nakuanza kusogea nyuma,akaja kwa speed ile kushtuka naona ameshakaribia,nilichofanya ile karibia ananipiga kichwa mi nikaruka juu na kuachia msamba ye akapiga hewa mpaka akaangua mwenyewe..
Je ni hatari gani au mchezo gani mbaya ulipokuwa mtoto unakumbuka?
Lingine nilienda kwa babu ,pale jirani kwa babu walikuwa wanafunga kondoo,kumbe watoto wa jirani wamefundisha kondoo dume wao kupiga watu kwa kichwa,kwahiyo ukijisahau ukasimama hivyo unakuta kondoo anasogea kinyume nyume hatua kama 15 hivi halafu anakutifua kwa kichwa,akikupata anaweza akakuvunja kiuno au miguu.
Sasa siku moja niliona kama kondoo wamelala halafu nikajisahau,kumbe kondoo akaamka taratibu nakuanza kusogea nyuma,akaja kwa speed ile kushtuka naona ameshakaribia,nilichofanya ile karibia ananipiga kichwa mi nikaruka juu na kuachia msamba ye akapiga hewa mpaka akaangua mwenyewe..
Je ni hatari gani au mchezo gani mbaya ulipokuwa mtoto unakumbuka?