Kitimtim Bungeni: Wenje atolewa nje ya Bunge

naomba kujua juuya lissu ..anamtuhumu waziri kusema uongo upi?....naomba kujua huo uongo


huyo mwenyekiti wa leo ''MABUMBA'' huyu ni mzaliwa wa ukerewe...huko dole kazamia tu lakini ni mkerewe pure wa pale nakisirila
angalia page ya kwanza kwenye post no.15-utaelewa
 
Hii hoja ni nzuri kwamba nini kinafanyika baada ya hoja kuwasilishwa.
huu mwaka kitaeleweka tu,yetu macho na masikio,na mala nyingi ushahidi huo huwa hausomwi wala kuchukuliwa hatuwa yeyote ile,sasa hakuna maana ya kutowa ushahidi kama wanakalia hata shahidi zilizo pita
 
hivi huyo Lawrence katembelea/kaalikwa na bunge, kuna uhusiano gani kati ya Lawrence na huyo mwenyekiti wa leo wa kutoka Dole na mwisho kuna bifu gani kati ya Lawrence na Wenje ?? naomba mnieleweshe tafadhalini Wakuu wangu
bifu kati ya Laurence na Wenje ni matokeo ya uchaguzi mwaka jana. Bifu kati ya Wenje na Mwenyekiti ni uccm na Peoples Power
 
watoa mada mjitahidini kueleza vizuri wengine tunatumia simu KWETU umeme ni mambo ya anasa hatupaswi kuwa nao hivyo TV hazina mashiko tena
 
Ngugu wana JF,

Kuna thread ilianzishwa hapa kuhusu yaliyojiri bungeni leo kuhusu Wabunge Wenje, Moses na Tundu Lissu. Ni kweli Tundu Lissu amesema Naibu Waziri kadanganya bunge na yeye na ushahidi. Kilichotokea ni kwamba Tundu Lissu alikatishwa kumwaga radhi hadharani. Baada ya maswali na majibu, kabla ya Waziri David Mathayo kuanza kusoma bajet yake, ndo Mwenyekiti wa bunge kamtaka Tundu Lissu atoe uthibitisho saa tano na kama hana afute kauli yake. Ndipo Moses na Wenje walipoibuka na malumbano kuhusu Tundu Lissu kuongezewa muda. Mwisho wa yote, Wenje katolewa nje. Ninachoona kwa tafsiri yangu ni kama ifuatavyo;
  1. Kulikuwa na ulazima gani wa wabunge Wenje na Moses kumkingia kifua kumtetea Lissu kuongezewa muda wakati Lissu mwenyewe hajadai kuongezewa muda? Tena Lissu alikuwa yatari kutoa ushahidi wake papo hapo? Nionavyo mimi baadhi ya wabunge wa CHADEMA wanatafuta cheap popularity.
  2. Rafiki yangu Wenje hakujua kuwa leo Lawrence Masha yupo mle ndani (kama mgeni bungeni)
  3. Je kwa nini bunge la awamu hii imejaa malumbano yasiyo na msingi? Miongozo ya spika, taarifa, etc. malumbano yasiyo ya msingi.



Na wewe huoni kuwa unatafuta cheap popularity kwa kuanzisha thread wakati ungeendelea kuchangia kwenye thread iliyoanzishwa awali inayoelezea sakata hilo.Na hiyo ya Lawrence Masha kuwepo bungeni inahusiana nini na Wenje? Magamba kwa kutaka umaarufu tu hamjambo, ila mjue chama ndiyo kinakufa hivyo tafuteni pa kwenda
 
Nafuatilia uwasilishwaji wa Hotuba ya Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi.....baada ya Waziri Dokta Mathayo David na Mwenyekiti wa Kamati Mheshimiwa Nkumba amefuata Msemaji wa Kambi ya Upinzani Mheshimiwa Kasulumbayi na anasema hoja ya Wenje inatokana na taarifa za hivi karibuni za Vyombo vya Habari kuwa kuna Samaki wenye Sumu kutoka Japan wameingizwa nchini na wameshaanza kuliwa na Watz hasa wa Dsm huku Serikali ikiwa imekaa kimya...

"Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam wapo hatarini kula samaki wenye sumu baada ya kumpuni moja (jina linahifadhiwa) kudaiwa kuingiza shehena ya samaki hao wanaodhaniwa kuwa na mionzi ya nyuklia.
Habari za uhakika ambazo NIPASHE Jumapili imezipata ni kwamba shehena hiyo ya samaki iliingizwa nchini wiki tatu zilizopita na kampuni hiyo ya jijini kutoka nchini Japan kupitia bandari ya Dar es Salaam."
 
47.-(1) Baada ya Muda wa Maswali kwisha, Mbunge yeyote anaweza
kutoa hoja kuwa Shughuli za Bunge kama zilivyooneshwa kwenye
Orodha ya Shughuli ziahirishwe ili Bunge lijadili jambo halisi la
dharura na muhimu kwa umma.
(2) Hoja ya namna hiyo itakuwa ni maalumu na inaweza kutolewa
wakati wowote hata kama majadiliano yatakuwa yanaendelea.
(3) Hoja itatolewa na Mbunge kwa kusimama mahali pake na
kuomba idhini ya Spika kutoa hoja ya kuahirisha Shughuli za Bunge
kwa madhumuni ya kujadili jambo halisi la dharura na muhimu kwa
umma.
Maswali
kujibiwa
kikamilifu
Kuahirisha
Shughuli
za Bunge
ili
Kujadili
Jambo la
Dharura
Maswali
ya
nyongeza
yasiyoruhusiwa
29
(4) Iwapo Spika ataridhika kwamba jambo hilo ni la dharura, halisi
na lina maslahi kwa umma, basi ataruhusu hoja hiyo itolewe kwa
muda usiozidi dakika tano na mjadala juu ya hoja hiyo utaendelea
kwa muda ambao Spika ataona unafaa kwa kuzingatia mazingira
ya suala linalojadiliwa.
48.-(1) Masharti ya jumla yafuatayo yatatumika vilevile kuhusu
hoja ya kujadili suala la dharura:-
(a) hoja hiyo haitaruhusiwa iwapo inahusu jambo
ambalo kwalo taarifa ya hoja imekwisha
kutolewa au jambo ambalo limekwisha
kuwekwa kwenye Orodha ya Shughuli;
(b) hoja zaidi ya moja katika kikao kimoja zenye
kutaka kuahirisha Shughuli za Bunge kwa
kutumia Kanuni hii hazitaruhusiwa; au
(c) jambo ambalo litakuwa limejadiliwa katika hoja
ya kuahirisha Shughuli za Bunge iliyotolewa kwa
mujibu wa Kanuni hii, halitaletwa tena Bungeni
katika Mkutano ule ule kwa kutumia Kanuni hii.
(2) Jambo linaloletwa kwa hoja chini ya Kanuni hii litahesabiwa tu
kuwa ni jambo halisi, iwapo:-
(a) ni jambo mahususi;
(b) halikuwekwa katika lugha ya jumla mno au lina
mambomengi mchanganyiko;
(c) halikutolewa kwa kutegemea habari zisizo za
uhakika au habari halisi juu ya jambo hilo
hazipatikani; au
(d) halihusu mambo ya kinadharia.
(3) Jambo linaloletwa kwa hoja chini ya Kanuni hii litahesabiwa
kuwa ni jambo la dharura, iwapo:-
(a) athari zake ni dhahiri na linaweza kutokea wakati
wowote;
Masharti
ya
jumla
kuhusu
Jambo
la
Dharura
30
(b) limetokea siku hiyo au siku za karibuni na
limeletwa bila kuchelewa; au
(c) hakutatokea fursa ya kulijadili siku za karibuni
kwa njia ya kawaida ya kushughulikia mambo ya
Bunge.
(4) Jambo lolote litahesabiwa kuwa ni lenye maslahi kwa umma
iwapo utatuzi wake unategemea hatua zaidi kuliko zile za
utekelezaji wa kawaida wa sheria peke yake.



Tusome hapo vizuri.
 
Wafanyakazi wengi wawe wa umma au sekta binafsi huanza na mishahara kidogo na kupandishiwa kadri miaka inavyokwenda. Wabunge wetu ni tofauti, aliyeingia mwaka huu na ambaye yuko bungeni kwa miaka 25 wanalipwa sawa Mshahara + posho ya ubunge + mafuta ya kutembelea jimbo + perdiem wanapokuwa nje ya jimbo + posho za kila kikao; kwa vyovyote kuna ambao watachanganyikiwa na hicho kipato ambacho hawakutegemea kukipata
 
Kwa taarifa yako mimi ni pro- CHADEMA ila sikufurahishwa na malumbano kama yale. Ninapochangia hapa siegemei upande wowote wa kichama, but Utaifa kwanza. Najua kwa uchachunge wa Chadema hoja zao nyingi zinapigwa chini kwa style ya kuleta ushahidi wa maandishi. Ukilinganisha approach za akina Wenje na Dr. Slaa alipokuwa bungeni utaona wazi kuwa Dr. Slaa alikuwa anajua kuvumilia kuliko akina Wenje. Tuache ushabiki wa vyama tuseme ukweli, hapa tunaelimishana tuu wakuu.
 
Wenje, ni mtu wa Kenya kule wamezoe fujo na ugomvi kila wakati. nawasikitikia sana watu wa Mwanza
 
Ngugu wana JF,

Kuna thread ilianzishwa hapa kuhusu yaliyojiri bungeni leo kuhusu Wabunge Wenje, Moses na Tundu Lissu. Ni kweli Tundu Lissu amesema Naibu Waziri kadanganya bunge na yeye na ushahidi. Kilichotokea ni kwamba Tundu Lissu alikatishwa kumwaga radhi hadharani. Baada ya maswali na majibu, kabla ya Waziri David Mathayo kuanza kusoma bajet yake, ndo Mwenyekiti wa bunge kamtaka Tundu Lissu atoe uthibitisho saa tano na kama hana afute kauli yake. Ndipo Moses na Wenje walipoibuka na malumbano kuhusu Tundu Lissu kuongezewa muda. Mwisho wa yote, Wenje katolewa nje. Ninachoona kwa tafsiri yangu ni kama ifuatavyo;
  1. Kulikuwa na ulazima gani wa wabunge Wenje na Moses kumkingia kifua kumtetea Lissu kuongezewa muda wakati Lissu mwenyewe hajadai kuongezewa muda? Tena Lissu alikuwa yatari kutoa ushahidi wake papo hapo? Nionavyo mimi baadhi ya wabunge wa CHADEMA wanatafuta cheap popularity.
  2. Rafiki yangu Wenje hakujua kuwa leo Lawrence Masha yupo mle ndani (kama mgeni bungeni)
  3. Je kwa nini bunge la awamu hii imejaa malumbano yasiyo na msingi? Miongozo ya spika, taarifa, etc. malumbano yasiyo ya msingi.

yaani hapo kwenye nyekundu hii nikauli ya KIMAGAMBA ambayo siipendi kabisaa,sasa atafute hiyo unayoiita kwa nani na imsaidie nini!
Unaweza ukawa na hoja ila kauli hiyo tuu unaonekana wewe Kilaza, Hiyo kauli ni ya VILAZA acha hizo wewe kama vp na wewe itafute basi!
 
Wafanyakazi wengi wawe wa umma au sekta binafsi huanza na mishahara kidogo na kupandishiwa kadri miaka inavyokwenda. Wabunge wetu ni tofauti, aliyeingia mwaka huu na ambaye yuko bungeni kwa miaka 25 wanalipwa sawa Mshahara + posho ya ubunge + mafuta ya kutembelea jimbo + perdiem wanapokuwa nje ya jimbo + posho za kila kikao; kwa vyovyote kuna ambao watachanganyikiwa na hicho kipato ambacho hawakutegemea kukipata
magamba yanaendelea daah!
 
Back
Top Bottom