Kama watu wanataka kubaki kwenye GPA basi marks zisishushwe zirudishwe juu! Mfumo wa GPA si mbaya bali taratibu za utumiaji wake kwa ngazi ya chini bado ni tatizo maana sidhani hata hizo marks zinazo jazwa kama maendeleo zina utaratibu maalum..nina hakika kuna wengine wanajaziwa tuu ili wafaulu mitihani! Huu mfumo kwa ngazi ya chini ni mbaya mbaya ....Kwa hili la kuturudisha kwenye DIVISION kutoka kwenye GPA,wadau tuna muunga mkono Mh. Waziri wa elimu, kwani mfumo huu Watanzania wote tuliuzoea,ila walikuja watu wachache wavivu walio na madaraka wakataka kuwayumbisha Watanzania.Nakumbuka hata Mh. Spika wa bunge la Tanzania wakati huo aliupinga mswada huo wa kubadilisha utaratibu wa ufaulu kutoka DISION kwenda GPA.
Asanteni.
ukitaka kufahamu ubora wa mwanasiasa wa kitanzania,zingatia maamuzi anayoyafanya karibia siku za uchaguzi.Ndalichako anaakili kubwa,sisi wenye akili kubwa ndio tulio mwelewa.
Prof. Mkumbo umesema na yangu. Lengo la prof Ndalichako si baya. Utaratibu wa maamuzi si mzuri kwa kweli. Lkn walivyokuwa wameshusha viwango vya ufaulu ilikuwa inaboa sana. Mtu ana D mbili amefaulu?
Sasa siasa basi kwenye elimu, weleji ujidhihirishe.
mfumo wa divisheni ni mzuri na wadau wa elimu wanaukubali. mfumo huu umenuia kurudisha ubora wa elimu ulioharibiwa na mfumo wa GPA baada ya wanasiasa kushusha mpango wa ufaulu ili kupata wanafunzi wa kujaza sekondari za kata. sasa hv wanafunzi wanafunzi hawachaguliwi kulingana na ufaulu bali wanachaguliwa kwenda kujaza nafasi katika sekonadari za kata.Sasa huyu Prof naye shida tu naye anataka kuwa profesa wa siasa. Tulikuwa na mfumo wa Division akaja mwingine akauondoa akaleta mfumo wa GPA huyu wa sasa ka-restore system, hivi ku-restore ni kufanya kufanya kitu kipya? Mimi nadhani sasa ni nafasi kwa huyu profesa kutoa maoni yake kwanini anadhani tuhame kwenye division na kwenda kwenye GPA maana kwa jinsi nilivyomsoma ni kwamba waziri wa elimu aliyeondoa division na kuleta GPA hakushrikisha wadau kwa hiyo huyu sasa ame-restore sysytem ili mtoe mawazo yenu
hahaha! huyu jamaa atakuwa anatetea mfumo uliomvusha kiubwete ndio maana anamshambulia sana prof ndalichako. serikali ya ccm imeiharibu elimu yetu kabisa. eti paper 2 inaitwa continous assesment...hiki akili za kimulugo ndizo zilizoifikisha hii nchi hapa ilipo.Mkuu huu uandishi ndo ulifundishwa hivi shuleni au umejiamulia tu!!
itakuwaje atakapomaliza chuo,je tutazalisha wasomi bora au bora wasomi,hi ni karne ya 21Mimi nataka GPA kila mtu afike chuo kikuu
profesa ni jibuyeye prof kitila mkumbo amefanya utafiti gani hadi kuandika hiyo article yake au anatokwa povu tu manake sioni data zozote ku sapport alichoandika