Kitila Mkumbo awashangaa Upinzani wanaotetea vihiyo

go kitila mkumbo go... UDC huo unakunyemelea...usilegeze kamba anza sasa kwenda channel 10....
CHANNEL 10 NDIO YA WANAOJIKOMBA, WAHUBIRI WOTE WA UONGO, SHARIFU MAJINI, WASANII, NA VYOTEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEE VYENYE MASHAKA
 
Tunaomjua Kitila Mkumbo, naye ni kilaza. Alimaliza PCB mwaka 1992 akefeli, akapitia njia za panya kuingia chuo na kusoma arts. Si genius kama anavyoji potray. Kwa hiyo kusona diploma na kutafuta njia ya kuingia chuo si kitu kigeni kwa Mkumbo, hata Magufuli pia. Alisoma diploma ya ualimu kabla ya kujiunga na chuo. Ni utoto kuwadhihaki watoto hao ati ni vilaza wakati mazingira ya shule yetu ni ovyo na Magufuli anajua hivyo. Mbona Jesca wake naye alipata dvs 4 mwaka 2102? Naye tumuite baba kilaza?

Rais ni baba wa watz wote, kumdhalilisha mwano hadharani kama baba si busara.
 
Hawa hawa UKAWA ndiyo wakati wa kampeni 2015 walikuwa wanasisitiza ELIMU, ELIMU, ELIMU. Haya tujiulize elimu ya bure hadi chuo kikuu waliokuwa wanaihubiri ni hii yakupeleka watu chuo kikuu wasio na sifa?
 
wenzako wameelewa, vilaza kama wewe ndo hujaelewa. Unadhani wote huku ni wajaluo ndo tujue majina yenu yanaandikwaje? Kikubwa ni ujumbe, hata wewe najua umeelewa vema na pengine unajua zaidi ila kwakuwa huna la maana la kuongeza, basi utaamua tu uchafue mazingira kama wale wanaojisaidia kwenye vituo vya mabasi ya mwendokasi et kwakuwa tu vyoo havijakamilika!
Kumbe vyoo havijakamilika? Hii nayo kali.

Turudi kwenye mada yako sasa. Kwa nini huyo uliyeleta taarifa zake ameonekana kuwashambulia wabunge wa upinzani wakati asubuhi ile niliona wabunge wengi wa CCM pia walilalamika? Pili, sidhani kama walikuwa wanatetea wanafunzi wasio na sifa kusoma, bali namna walivyoondolewa..vile vile kwa nini walijikuta mahali pale. Kwani si waliletwa kwa 'amri' ya Rais wa wakati huo? Tatu, tunataka tuone sasa Rais akiufanyia kazi huo 'ushauri' wa Kitila maana pamoja na kuwatimua watoto hao, uhaba wa waalimu wa Sayansi bado uko pale pale.
 
Hawa hawa UKAWA ndiyo wakati wa kampeni 2015 walikuwa wanasisitiza ELIMU, ELIMU, ELIMU. Haya tujiulize elimu ya bure hadi chuo kikuu waliokuwa wanaihubiri ni hii yakupeleka watu chuo kikuu wasio na sifa?
Sifa zipi? kwani walipelekwa na nani huko chuoni? halafu nikamsikia mkubwa anasema kuwa watu hawa walioko chuo kikuu wengine kwa alama walizopata hawakustahili kwenda kusoma hata diploma! kwani ameambiwa kuwa pale wanasoma digrii? Au hajui kwamba kwenye vyuo vikuu vyote siku hizi kuna non-degree programmes na kwamba si kila aliyeko chuo kikuu anachukua shahada?

Anyway, sitaki kuongelea sana ufaulu wao, ila nafahamu kwamba wamechaguliwa kuingia pale na watu fulani. Kama kuna mtoto alifoji vyeti, huyo achukuliwe hatua kwa makosa hayo. lakini kama mmeita waliopata division four wakasome hiyo special diploma yenu na mkawachagua/mkawadahili wenyewe enyi serikali ya CCM, leo hii hamna sababu wala haki ya kuwadhalilisha.
 
Wapinzani na wale wa Chama Tawala walitetea logistics za kuwaondoa pale chuoni,especially wale wanafunzi walikua under 18years. Kwa kweli mimi naona hii issue inakuwa twisted kila sisiku na sababu zinazotolewa zinabadilika.Tuzidi kuliombea hili taifa letu,tukiendelea kuwalaumu wapinzani wakati haya yote yamefanyika chini ya Chama Tawala,hatuta fika.Cha muhimu ni kujisahihisha pale palipo kosewa na kwenda mbele.Sio wakati wa kutafuta mchawi.

Tumekuwa Taifa la hovyo kabisa Taifa lisilojali utu ila siasa tu kila sehem. Taifa la viongozi wanaongea leo hiki na kesho anabadilisha bila wasiwasi wowote. Kwa kweli tunahitaji maombi.
 
Wapinzani na wale wa Chama Tawala walitetea logistics za kuwaondoa pale chuoni,especially wale wanafunzi walikua under 18years. Kwa kweli mimi naona hii issue inakuwa twisted kila sisiku na sababu zinazotolewa zinabadilika.Tuzidi kuliombea hili taifa letu,tukiendelea kuwalaumu wapinzani wakati haya yote yamefanyika chini ya Chama Tawala,hatuta fika.Cha muhimu ni kujisahihisha pale palipo kosewa na kwenda mbele.Sio wakati wa kutafuta mchawi.

Chama Tawala kinaingiaje hapa, Chuo kimefukuza wanafunzi wake hata kama muongozo umetoka serikalini lakini sio katika chama. Taifa liko poa nyie ndio mjiombee ili busara ziwe zinawatangulia kwanza na kuacha kudumisha fikra za KUB hata kama haziko sahihi.
 
Pale issue ilikuwa ni kuwatoa hao anaosema wana 4 na zero na kuwaacha wenye sifa waendelee, mbona rahic tuu jamani!? Tawi bovu dawa sio kung'oa mti na mizizi yake
 
Cha msingi hapa tuzungumzie sifa za msingi za mtu na kujiunga na taaluma fulani kwenye vyuo vya Tanzania. Haijalishi, ni nani alitoa maamuzi hayo itabaki kuwa na makosa, tena makosa makubwa sana lakini hatupaswi kutetea uvunjaji huu wa taratibu. Yeyote atakaetetea hili anapaswa kulaumiwa. Elimu yetu imevulugwa tunapaswa ku I reform upya. Bila ya hivyo tutaendelea kudidimia.
 
Kumbe vyoo havijakamilika? Hii nayo kali.

Turudi kwenye mada yako sasa. Kwa nini huyo uliyeleta taarifa zake ameonekana kuwashambulia wabunge wa upinzani wakati asubuhi ile niliona wabunge wengi wa CCM pia walilalamika? Pili, sidhani kama walikuwa wanatetea wanafunzi wasio na sifa kusoma, bali namna walivyoondolewa..vile vile kwa nini walijikuta mahali pale. Kwani si waliletwa kwa 'amri' ya Rais wa wakati huo? Tatu, tunataka tuone sasa Rais akiufanyia kazi huo 'ushauri' wa Kitila maana pamoja na kuwatimua watoto hao, uhaba wa waalimu wa Sayansi bado uko pale pale.
hapo ni wapinzani wanakosoana wenyewe hata Kingunge alishamkosoa Mbowe. Anayekosoa upinzani huwa mnamwita nani vile?
 
Tunaomjua Kitila Mkumbo, naye ni kilaza. Alimaliza PCB mwaka 1992 akefeli, akapitia njia za panya kuingia chuo na kusoma arts. Si genius kama anavyoji potray. Kwa hiyo kusona diploma na kutafuta njia ya kuingia chuo si kitu kigeni kwa Mkumbo, hata Magufuli pia. Alisoma diploma ya ualimu kabla ya kujiunga na chuo. Ni utoto kuwadhihaki watoto hao ati ni vilaza wakati mazingira ya shule yetu ni ovyo na Magufuli anajua hivyo. Mbona Jesca wake naye alipata dvs 4 mwaka 2102? Naye tumuite baba kilaza?

Rais ni baba wa watz wote, kumdhalilisha mwano hadharani kama baba si busara.
2102? Wewe ndo kilaza OG.
 
Watu wanajitoa ufahamu kweli, huyu nae anaingia kwenye kichaka cha ujinga baada ya kusifiwa na rais alie amua maamuzi ya hovyo? Hakuna mwanasiasa wala mtu alie tetea vihiyo ila utaratibu wa kuwaondoa ndio unao lalamikiwa na watu, rais amejua amekosea kwenye hili ndio maana anatumia nguvu kubwa kugeuza uhalisia na kujidai watu wanatetea vihiyo, wakati ukweli anajua watu wanatetea nini, kila siku uwe mkweli Mungu akubariki. Watoto kufukuzwaa na polisi ndani ya saa 24 bila usafiri wala kujua wanalala wapi ndio tatizo.
 
Huyu profesa kitilya mkumbo amekuwa kama dr. Bana, hawa wote hawana tofauti na watu kama Hamad rashid au mrema au shibuda
Hata wewe mwenye akili za Kuku unawashangaa wenyewe Udaktar wa Taaluma zao?
Ukipata angalau cheti cha undergraduate ndo Uje na comments hizo
 
Niliwahi kusema maprof wetu na madr wengi ni hohe hahe wachumia tumbo na wasio na chembe ya msimamo! Refer Shivji na Mwakyembe, Refer bana na mkumbo kwa kujikomba chama tawala! Usiwasikilize hawa watu hata kidogo ni janga la kitaifa. Wanatumia kichwa wanapokuwa masomoni wakirudi kuajiriwa na wakaangalia kipato wanachopata wanaanza kufikiri kwa kutumia masaburi na tumbo.
 
Hata wewe mwenye akili za Kuku unawashangaa wenyewe Udaktar wa Taaluma zao?
Ukipata angalau cheti cha undergraduate ndo Uje na comments hizo
Acha upumbavu kuwa Dr ni kukariri tu wengi tunawajua hawana lolote la maana zaidi kichwani! Watu wenye Bachelor na masters ni wazuri kuliko hawa wakaririji
 
Hakuna aliyedhalilishwa. Shule zote siku zote zikifungwa huwa ni immediately kesho yake huwa hakuna huduma. Watoto na wazazi hawana tabu kupewa 24 hours hii ndiyo kawaida. Nani kalalamika kashindwa kuondoka? UKAWA as usual walitaka political capital out of other people's misery: mngewapa mwezi mmoja kurudi nyumbani ingesaidia nini zaidi ya kuleta wachochezi?
Ratiba ya kufunga shule/chuo na hata mabadiliko hujulikana mapema. Kwa kuchanganya swala hilo na kufukuzwa, ninatilia wasiwasi uwezo wako wa kuelewa mambo. Au ndio bk 7 zafanya kazi?
 
Chama Tawala kinaingiaje hapa, Chuo kimefukuza wanafunzi wake hata kama muongozo umetoka serikalini lakini sio katika chama. Taifa liko poa nyie ndio mjiombee ili busara ziwe zinawatangulia kwanza na kuacha kudumisha fikra za KUB hata kama haziko sahihi.
Hautaki tena iitwe serikali sikivu ya CCM. Kulikoni wajameni?
 
Back
Top Bottom