Kisima cha kutunzia maji ya mvua

Kisima cha kutunzia maji ya mvua

Sawa mkuu,nalo neno. Kuna Eli79 amesema ni kama milioni 4 hivi. Au wewe unaona gharama inaweza kuwa sawa na milioni 9 mkuu?
Kwanza unataka kisima kinachotunza maji kiasi gani au labda hiyonyumba ni ya bati ngapi maana kwa tropical sqm1 ya bati kwa msimu inajaza maji unit moja at square cubic koja , kujua mahesabu ya material ni kujua ukubwa wa tanki
 
Maji ya kisima pia ni mazuri maana ni ya kudumu hasa ukipata maji mapole. Tatizo hizo bei, naona ziko juu sana.

Utaweka ya mvua ni sawa kabisa, hivi wawezaje wote wanaokuzunguka hawana maji wewe uko ndani na familia yako na maji yako, hakika mimi siwezi.

Namkumbuka mtu mmoja alijiwekea matanki makubwa na akawa anapata maji ya mwaka mzima ila kwake husogei maana siyo mageiti hayo. Bahati mbaya sana mume na mke wametangulia, ule mjumba upo hakuna hata anayeishi, maisha bana.

Hapa kwetu tulikuwa na shida sana ya maji chini pia wapimaji miaka ya nyuma walisema maji hakuna, ila nilipochimba nilipata maji ya kisima na ikabidi nichimbe visima viwili changu na cha raia. Yaani wanachota for no cost maana nami ni kama Mungu alinipa maji kwa sababu tu japo nilitumia gharama sana.

Angalia jipime na moyo wako na mazingira ya watu wako ufanye litakalokupendeza.
Shukran sana kwa maelezo/maoni haya yako, inaonesha una experience nzuri sana kuhusu changamoto za maji na jamii zetu , Please na mimi nakumbana na scenario kama hiyo hiyo
natamani kuongea na wewe ili kujua mengi na kupata ushauri zaidi please.
 
Maji ya kisima pia ni mazuri maana ni ya kudumu hasa ukipata maji mapole. Tatizo hizo bei, naona ziko juu sana.

Utaweka ya mvua ni sawa kabisa, hivi wawezaje wote wanaokuzunguka hawana maji wewe uko ndani na familia yako na maji yako, hakika mimi siwezi.

Namkumbuka mtu mmoja alijiwekea matanki makubwa na akawa anapata maji ya mwaka mzima ila kwake husogei maana siyo mageiti hayo. Bahati mbaya sana mume na mke wametangulia, ule mjumba upo hakuna hata anayeishi, maisha bana.

Hapa kwetu tulikuwa na shida sana ya maji chini pia wapimaji miaka ya nyuma walisema maji hakuna, ila nilipochimba nilipata maji ya kisima na ikabidi nichimbe visima viwili changu na cha raia. Yaani wanachota for no cost maana nami ni kama Mungu alinipa maji kwa sababu tu japo nilitumia gharama sana.

Angalia jipime na moyo wako na mazingira ya watu wako ufanye litakalokupendeza.
Nakubaliana na wewe mimi nimechimba bwana karibu kitongoji chose cha kaya 500 wamekuwa majirani zangu na ninafaidi kweli wao wanatumia maji mm nachunga bure maeneo yao na bado nimewafundishwa was wawili wangu kunywa maziwa sasa nauza maziwa... pe gi e kama ana budget ndogp achieve bwana kwa 4m anaweza kimcha bwawa la eka moja sawa na 5000m3 kama ni sehemu ya bond yanawez yakama hata mara tatu.......A big lesson kuishi na community ni raha sana .... everyone in the village has a value and has something to give sio kama hapa mjini kila mtu na gets lake
 
Hakuna tatizo, utapunguza gharama kubwa sana. 20' deep, 15' diameter gharama inaweza kufika 4m au zaidi kutegemeana na eneo husika.

Muhimu tu utumie tofali imara, usiwe bahili wa cement, ukiweza weka wire mesh ili kuimarisha kuta, chini weka ile nailoni nyeusi ili kuzuia maji kupotea, jenga msalaba ili kuimarisha kuta na hakikisha unalifunika ili mwanga wa jua usipenye ndani. Ukifanya hivi hata hizo water guard utaweka kwa utashi tu ilà haitakuwa lazima.

Utaokoa gharama nyingi kununua maji.
Kiongozi naomba ufafanuzi kwenye nailon au picha ya nailon hiyo
 
Nakubaliana na wewe mimi nimechimba bwana karibu kitongoji chose cha kaya 500 wamekuwa majirani zangu na ninafaidi kweli wao wanatumia maji mm nachunga bure maeneo yao na bado nimewafundishwa was wawili wangu kunywa maziwa sasa nauza maziwa... pe gi e kama ana budget ndogp achieve bwana kwa 4m anaweza kimcha bwawa la eka moja sawa na 5000m3 kama ni sehemu ya bond yanawez yakama hata mara tatu.......A big lesson kuishi na community ni raha sana .... everyone in the village has a value and has something to give sio kama hapa mjini kila mtu na gets lake
Mi wanachota maji ila dukani kwangu ni wateja wazuri, nauza kiasi kuwa maduka ya jirani wananuna. Wanajua hawawezi kupata free maji bidhaa wanunue kwingine.

Tuishi kwa maarifa pia.
 
Nakushauri uchimbe kisima kirefu!!
Jenga tower ya mita kama 5, weka simtank ya Lita elfu 10 juu yake... Weka motor, vuta Maji kwenye kisima hadi kwenye tank iliyoko kwenye riser hiyo ya mita 6... Weka plumbing kwenye nyumba yako... Then anza kutumia Maji...

Utatumia gharama, lakini hiyo kitu utakaa nayo for a long time...
Labda kisima kikauke...

I know more about Water Supply System...
Ni mtalaam wa fani hii
 
Nakushauri uchimbe kisima kirefu!!
Jenga tower ya mita kama 5, weka simtank ya Lita elfu 10 juu yake... Weka motor, vuta Maji kwenye kisima hadi kwenye tank iliyoko kwenye riser hiyo ya mita 6... Weka plumbing kwenye nyumba yako... Then anza kutumia Maji...

Utatumia gharama, lakini hiyo kitu utakaa nayo for a long time...
Labda kisima kikauke...

I know more about Water Supply System...
Ni mtalaam wa fani hii
Naomba namba yako niko tayari kulipa consultation fee , tayari nimechimba kisima, na Tower tumejenga 8 mtr high base ya 3 m diameter matofali ya kulaza kila 2m bean nondo 4 na katikati sbb ni msaraba katikati kuna column ya nondo 4 toka chini.

Swali langu mnara huu unaweza beba tank la ujazo gani wa maji maximum ?
Swali la pili tofauti ya cost ya container per ltr kwa haya matank yafuatayo mfano wa 30,000 ltrs
1. Tank la kujenga chini ya ardhi moja au 2
2. Tank la kujenga juu ya ardhi 1,2 hata 3
3. Tank la plastic kwa maeneo nilipo 10,000L ni sh 2,400,000 site
2,400,000x3 =7,200,000 /30000 = Tsh 240 per lita maji
4. Tank plastic 3000L ni sh 520,000 site
650,000 x 10 = 6,500,000 /30,000 = Tsh 216 per lita

naomba msaada makadirio ya gharama namba 1 na 2 tafadhali
 
Kuongezea hapo shimo la choo liwe umbali angalau kuanzia 15m kutoka kwenye kisima usije ukawa unakunywa kinyesi na kuumwa tumbo la kuhara daily.​
Liko mbali mkuu. Isitoshe tunakochimbia kisima ni juu,liliko shimo la choo ni chini,halafu katikati hapo panatenganishwa na nyumba kubwa
 
Binafsi ndo nipo kwenye mchakato huo na shimo langu ni kwenda chini ni foot 24
Upana ft 10

Kwa upana huo natarajia kuvuna Lt 40000 elfu


Na matumiz yangu kwa siku nimepiga hesabu
Kwa idadi ya watu ma shughul za kila siku home ni Lita 100 tu ambapo hizo 40000 nikigawa kwa 100 napata siku 400


Nb kuna siku matumiz yatapanda na sio Ila siku itakuwa 100 kuna siku yatashuka mpaka 60


Kwa wewe Lt 60000 naona kama nyingi sana kumbuka msimu wa mvua matumiz ya karo yatapungua sana

Miez mitatu yote
Asante mkuu.
 
Jenga na tofali ya block.. na iwe kwa ratio ya tofali 20-25 kwa mfuko wa cement.. zinapojengwa zinakatwa nusu na mortar inakuwa ratio kali.. ukimaliza ndani tumia wire mesh kabla ya kupiga lipu ya kwanza..

Lipu ya pili changanya na water proof cement.. kabla ya Kumaliza ba niru yenye kiwango Cha kutosha Cha water proof..

Nb chini kabla kuanza kunyanyua ukuta Kama unaweza tandika janvi lenye nondo thickness at least cm 15.

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
Wewe unajua mkuu. Asante sana
 
Wewe unajua mkuu. Asante sana
Huku tuliko maji nishida kwa hiyo wengi wanatumia njia hiyo.. katika utafiti wangu nimegundua maeneo mengi ya Tanzania maji yasingekuwa shida kama huu ungekuwa ni Utaratibu mandatory..

Unapunguza gharama kubwa ya miundombinu, unapunguza surface runoff ..ambayo inaongoza kwa kuharibu miundombinu na kuleta mafuriko..

Kikubwa kila nyumba ikijengwa iwe na under ground storage ya mita (4w*4h*4l) ambayo ikijaa to the rim hiyo Ni qubic metres 64 sawa na lita 64,000 za ujazo. Katika haya mtu ataweza kutumia mpaka lita elfu 60 za maji masafi..

Tunapokea mvua kwa mwaka kiasi kidogo kabisa nadhani inakuwa dodoma na Ni milimita 600 kwa mwaka.. so kwa nyumba yenye paa lenye ukubwa wa mita za mraba 100 kwa dodoma unaweza kukusanya lita elfu sitini. Nyumba Kama hiyo hiyo kwa mikoa ya Mbeya, Arusha, Kagera na kigoma anaweza kukusanya mpaka lita 95,000



Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Nakushauri uchimbe kisima kirefu!!
Jenga tower ya mita kama 5, weka simtank ya Lita elfu 10 juu yake... Weka motor, vuta Maji kwenye kisima hadi kwenye tank iliyoko kwenye riser hiyo ya mita 6... Weka plumbing kwenye nyumba yako... Then anza kutumia Maji...

Utatumia gharama, lakini hiyo kitu utakaa nayo for a long time...
Labda kisima kikauke...

I know more about Water Supply System...
Ni mtalaam wa fani hii
Asante mkuu. Nitakuwa nakucheck
 
Kiongozi naomba ufafanuzi kwenye nailon au picha ya nailon hiyo
Hizo mkuu, zinasaidia sana kuzuia kupotea kwa maji, ziwekwe tu vizuri.
Screenshot_20200905-104341.jpg
Screenshot_20200905-104254.jpg
 
Mkuu 500L ni nyingi mno, hiyo ni kama nusu boza(bowser) ambayo ni 1,000L, unless yupo na familia kubwa sana. Ndoo kumi-kumi na tano (200L) hivi zinatosha kwa siku hata kama umeweka system ya maji ndani. Japo katika matumizi ya maji siku hazilingani.
Kwa familia ya watu watano (5) washroom pekee wakienda 3times a day ni lita 5*3*5 sawa na lita 75... Matumizi mengine Kama kuoga just twice a day kwa kila member kila dakika unayokaa chini ya shower head inakula litre 10.. kwa dakika3 za kuoga 3*5*2*10 hizo ni lita 300.. matumizi mengine [emoji16] tukienda jikoni na kufua wageni [emoji16][emoji16][emoji120]

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app

Kwahiyo.. ukiweka average ya lita 400 per day.. lita elfu 60 zinakupa miezi mitano ya matumizi.
 
Kwa familia ya watu watano (5) washroom pekee wakienda 3times a day ni lita 5*3*5 sawa na lita 75... Matumizi mengine Kama kuoga just twice a day kwa kila member kila dakika unayokaa chini ya shower head inakula litre 10.. kwa dakika3 za kuoga 3*5*2*10 hizo ni lita 300.. matumizi mengine [emoji16] tukienda jikoni na kufua wageni [emoji16][emoji16][emoji120]

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app

Mkuu shower gani hiyo inatoa 10L/min? Say 10L kwa mtu mmoja, that's 10Lx5x2, walau 100L za kuoga kila siku maana mtaoga asubuhi na jioni, chooni approx. 2Lx5x3 hiyo ni 30L(kuna masinki yana option ya kubonyeza ukikojoa na kuonyeza haha kubwa), so haja kubwa 5Lx5x2(haja kubwa max. twice per day[emoji23][emoji23]) that's 50L. So 100L+30L+50L, hiyo ni 180L. Kufua(which is not everyday) 100L. You have 280L maximum everyday.
 
Mkuu shower gani hiyo inatoa 10L/min? Say 10L kwa mtu mmoja, that's 10Lx5x2, walau 100L za kuoga kila siku maana mtaoga asubuhi na jioni, chooni approx. 2Lx5x3 hiyo ni 30L(kuna masinki yana option ya kubonyeza ukikojoa na kuonyeza haha kubwa), so haja kubwa 5Lx5x2(haja kubwa max. twice per day[emoji23][emoji23]) that's 50L. So 100L+30L+50L, hiyo ni 180L. Kufua(which is not everyday) 100L. You have 280L maximum everyday.
Standard shower head inatoa maji yasiyopungua lita 9.5 kwa dakika. By design. [emoji16] Na vyoo vya kishua vya option ni ghali wengi wetu tunatumia squatting toilets.. ambazo tank yake inakula lita tano.. pale kuna kamba tu au lever haja yoyote ..ile ukikavuta tu tano hizooo.

[emoji16][emoji16][emoji16] [emoji16] [emoji1241]

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Standard shower head inatoa maji yasiyopungua lita 9.5 kwa dakika. By design. [emoji16] Na vyoo vya kishua vya option ni ghali wengi wetu tunatumia squatting toilets.. ambazo tank yake inakula lita tano.. pale kuna kamba tu au lever haja yoyote ..ile ukikavuta tu tano hizooo.

[emoji16][emoji16][emoji16] [emoji16] [emoji1241]

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
[emoji23][emoji23] sikujua hili, 9.5L/min nadhani ni nyingi mno mkuu. Elevation ya tank hapo ni mita ngapi, kwa sababu hydraulic pressure itategemea sana tank lilipo. Tank/sink lenye options ni zuri zaidi, ukikojoa unabofya inatoka 2L, ukikaa ndio 5L zinakwagika.[emoji23]
 
Back
Top Bottom