Stuxnet
JF-Expert Member
- Feb 12, 2011
- 10,384
- 17,953
Mwanadamu mmoja alikua akisafiri na mkewe wakitumia usafiri wa punda yaani wakiwa wamempanda punda yule lakini wakiwa njiani katikat ya safari yao wakakutana ma wanadamu wakawapazia sauti wakisema; ''ninyi watu hamuoni ya kuwa mnamuumiza punda huyo iweje ninyi wote wawili mumpande punda mmoja?
Jamaa kuskia hivyo akaona isiwe shida akaona amwambie mkewe ashuke apande yeye peke yake na mkewe akakubali safari ikaendelea lakini walipofika mbele wakakutana na wanadamu wengine wakamdhihaki tena bwana yule wakisema; ''Wewe mbona ni mwanaume usiye na huruma yaani wewe umepanda punda huyo na kumwacha mwanamke wako atembee em kuwa na huruma hata''
Jamaa akaona isiwe shida acha nishuke apande mke wangu na safari ikaendelea. Wakiwa njiani tena wakakutana na wanadamu wengine tena na walipomtazama tu bwana yule na mkewe wakaangua vicheko vya dharau wakisema; ''Tazama mwanaume yule asivyokua na akili yaani yeye anatembea kwa miguu na kumuacha mkewe apande punda?''
Jamaa kusikia vile akaona mke wangu isiwe shida acha tushuke sie na kumuacha punda atembee mwenyewe sie tutembee kwa miguu basi wakafanya hivyo na safari ikaendelea lkini walipofika mbele wakakutana na wanadamu wengine nao walipowaona tu wakawadhihaki wakisema; ''Tazama wajinga wale watembea kwa miguu ilihali wana punda na wanaweza kumpanda''
Basi baada ya mambo yale jamaa akawaza akaamua kumbeba punda. Nimekumbuka kisa hiki nikawatazama watanzania wanavyokosoa namna Rais SSH anavyoendesha nchi.
Chonde chonde Rais Samia usibebe punda, unafanya vizuri sana, endelea hivyo hivyo. Kimsingi wewe umewapa uhuru wa kusema, waache waseme lakini fanya yale uliyopanga kuwafanyia watanzania. Huwezi kuwaridhisha wote kwa namna wanavyotaka.
Jamaa kuskia hivyo akaona isiwe shida akaona amwambie mkewe ashuke apande yeye peke yake na mkewe akakubali safari ikaendelea lakini walipofika mbele wakakutana na wanadamu wengine wakamdhihaki tena bwana yule wakisema; ''Wewe mbona ni mwanaume usiye na huruma yaani wewe umepanda punda huyo na kumwacha mwanamke wako atembee em kuwa na huruma hata''
Jamaa akaona isiwe shida acha nishuke apande mke wangu na safari ikaendelea. Wakiwa njiani tena wakakutana na wanadamu wengine tena na walipomtazama tu bwana yule na mkewe wakaangua vicheko vya dharau wakisema; ''Tazama mwanaume yule asivyokua na akili yaani yeye anatembea kwa miguu na kumuacha mkewe apande punda?''
Jamaa kusikia vile akaona mke wangu isiwe shida acha tushuke sie na kumuacha punda atembee mwenyewe sie tutembee kwa miguu basi wakafanya hivyo na safari ikaendelea lkini walipofika mbele wakakutana na wanadamu wengine nao walipowaona tu wakawadhihaki wakisema; ''Tazama wajinga wale watembea kwa miguu ilihali wana punda na wanaweza kumpanda''
Basi baada ya mambo yale jamaa akawaza akaamua kumbeba punda. Nimekumbuka kisa hiki nikawatazama watanzania wanavyokosoa namna Rais SSH anavyoendesha nchi.
Chonde chonde Rais Samia usibebe punda, unafanya vizuri sana, endelea hivyo hivyo. Kimsingi wewe umewapa uhuru wa kusema, waache waseme lakini fanya yale uliyopanga kuwafanyia watanzania. Huwezi kuwaridhisha wote kwa namna wanavyotaka.