mikedean
JF-Expert Member
- Mar 15, 2018
- 3,255
- 4,599
Habari zenu wadau
Leo katika kupitia baadhi ya mambo mtandaoni nikakutana na kisa cha "Republic of Taured".
Ipo hivi, miaka ya 1950 ilitokea kisa cha kijana wa makamo katika airport moja huko Japan na kuwaeleza maofisa wa uwanja wa ndege kuwa anatoka nchi ya Taured. Maofisa wakamwambia kwamba nchi hiyo haipo kwenye ramani ya dunia. Cha ajabu yeye akang'ang'ania kuwa anatoka huko na akaonesha vitu vya kumtambulisha vya mamlaka ya Taured.
Vitambulisho kama vile passport na fedha alivionesha. Maofisa walipomwonesha ramani ya dunia akaonesha ilipo nchi ya Andorra na kusema hiyo ndio Taured ilipo tangu maelfu ya miaka. Wataured wanaongea Kiingereza, Kifaransa na Kispain.
Lakini baada ya maofisa waairport kumchunguza muda mrefu na kumpa chumba cha kulala kesho yake asubuhi walikuta chumba kitupu na haieleweki alipotelea wapi wakati chumba kilikuwa kikilindwa na maofisa usalama usiku kucha ili kupata ufumbuzi wa tatizo lile. Cha ajabu ni kwamba hata passport na nyaraka nyingine walizomnyang'anya kwa uchunguzi zaidi zilipotea kimazingara. Mpaka sasa haijulikani mtu huyo alipotelea wapi.
Pia kuna mtu wa ajabu alikutwa huko Ufaransa akiongea lugha ya ajabu. Alionesha sehemu aliyotoka kuwa Lisbon Ureno japo lugha haikuwa ya Kireno pia yeye alionesha kuwa sio mreno bali ni kutoka nchi ya 'Lizbonia'.
Nataka kujua je, ni kweli kwamba kuna milango ya siri ambapo ukiingia unaweza kukuta nchi nyingine kama hizi za Lizbonia na Taured?
Asante na karibu tujuzane.
Leo katika kupitia baadhi ya mambo mtandaoni nikakutana na kisa cha "Republic of Taured".
Ipo hivi, miaka ya 1950 ilitokea kisa cha kijana wa makamo katika airport moja huko Japan na kuwaeleza maofisa wa uwanja wa ndege kuwa anatoka nchi ya Taured. Maofisa wakamwambia kwamba nchi hiyo haipo kwenye ramani ya dunia. Cha ajabu yeye akang'ang'ania kuwa anatoka huko na akaonesha vitu vya kumtambulisha vya mamlaka ya Taured.
Vitambulisho kama vile passport na fedha alivionesha. Maofisa walipomwonesha ramani ya dunia akaonesha ilipo nchi ya Andorra na kusema hiyo ndio Taured ilipo tangu maelfu ya miaka. Wataured wanaongea Kiingereza, Kifaransa na Kispain.
Lakini baada ya maofisa waairport kumchunguza muda mrefu na kumpa chumba cha kulala kesho yake asubuhi walikuta chumba kitupu na haieleweki alipotelea wapi wakati chumba kilikuwa kikilindwa na maofisa usalama usiku kucha ili kupata ufumbuzi wa tatizo lile. Cha ajabu ni kwamba hata passport na nyaraka nyingine walizomnyang'anya kwa uchunguzi zaidi zilipotea kimazingara. Mpaka sasa haijulikani mtu huyo alipotelea wapi.
Pia kuna mtu wa ajabu alikutwa huko Ufaransa akiongea lugha ya ajabu. Alionesha sehemu aliyotoka kuwa Lisbon Ureno japo lugha haikuwa ya Kireno pia yeye alionesha kuwa sio mreno bali ni kutoka nchi ya 'Lizbonia'.
Nataka kujua je, ni kweli kwamba kuna milango ya siri ambapo ukiingia unaweza kukuta nchi nyingine kama hizi za Lizbonia na Taured?
Asante na karibu tujuzane.