Kisa cha kijana aliyetokea Jamhuri ya Taured

mikedean

JF-Expert Member
Mar 15, 2018
3,255
4,599
Habari zenu wadau

Leo katika kupitia baadhi ya mambo mtandaoni nikakutana na kisa cha "Republic of Taured".

Ipo hivi, miaka ya 1950 ilitokea kisa cha kijana wa makamo katika airport moja huko Japan na kuwaeleza maofisa wa uwanja wa ndege kuwa anatoka nchi ya Taured. Maofisa wakamwambia kwamba nchi hiyo haipo kwenye ramani ya dunia. Cha ajabu yeye akang'ang'ania kuwa anatoka huko na akaonesha vitu vya kumtambulisha vya mamlaka ya Taured.

Vitambulisho kama vile passport na fedha alivionesha. Maofisa walipomwonesha ramani ya dunia akaonesha ilipo nchi ya Andorra na kusema hiyo ndio Taured ilipo tangu maelfu ya miaka. Wataured wanaongea Kiingereza, Kifaransa na Kispain.

Lakini baada ya maofisa waairport kumchunguza muda mrefu na kumpa chumba cha kulala kesho yake asubuhi walikuta chumba kitupu na haieleweki alipotelea wapi wakati chumba kilikuwa kikilindwa na maofisa usalama usiku kucha ili kupata ufumbuzi wa tatizo lile. Cha ajabu ni kwamba hata passport na nyaraka nyingine walizomnyang'anya kwa uchunguzi zaidi zilipotea kimazingara. Mpaka sasa haijulikani mtu huyo alipotelea wapi.

Pia kuna mtu wa ajabu alikutwa huko Ufaransa akiongea lugha ya ajabu. Alionesha sehemu aliyotoka kuwa Lisbon Ureno japo lugha haikuwa ya Kireno pia yeye alionesha kuwa sio mreno bali ni kutoka nchi ya 'Lizbonia'.

Nataka kujua je, ni kweli kwamba kuna milango ya siri ambapo ukiingia unaweza kukuta nchi nyingine kama hizi za Lizbonia na Taured?

Asante na karibu tujuzane.
 
Hizo ni habari za kusadikika kama hadithi za mashimo ya mfalme sulemani na visa vya Adili na Nduguze.

Binafsi ukiamini vinakuwepo katika dunia yako na wasiomini havipo katika dunia zao
 
Hii nilishawahi kusimuliwa na Babu yangu Mzee Ismail Kanungila aliyekuwa anafanya kazi Japan miaka hiyo yaani 1949
 
Habari zenu wadau

Leo katika kupitia baadhi ya mambo mtandaoni nikakutana na kisa cha "Republic of Taured".

Ipo hivi, miaka ya 1950 ilitokea kisa cha kijana wa makamo katika airport moja huko Japan na kuwaeleza maofisa wa uwanja wa ndege kuwa anatoka nchi ya Taured. Maofisa wakamwambia kwamba nchi hiyo haipo kwenye ramani ya dunia. Cha ajabu yeye akang'ang'ania kuwa anatoka huko na akaonesha vitu vya kumtambulisha vya mamlaka ya Taured.

Vitambulisho kama vile passport na fedha alivionesha. Maofisa walipomwonesha ramani ya dunia akaonesha ilipo nchi ya Andorra na kusema hiyo ndio Taured ilipo tangu maelfu ya miaka. Wataured wanaongea Kiingereza, Kifaransa na Kispain.

Lakini baada ya maofisa waairport kumchunguza muda mrefu na kumpa chumba cha kulala kesho yake asubuhi walikuta chumba kitupu na haieleweki alipotelea wapi wakati chumba kilikuwa kikilindwa na maofisa usalama usiku kucha ili kupata ufumbuzi wa tatizo lile. Cha ajabu ni kwamba hata passport na nyaraka nyingine walizomnyang'anya kwa uchunguzi zaidi zilipotea kimazingara. Mpaka sasa haijulikani mtu huyo alipotelea wapi.

Pia kuna mtu wa ajabu alikutwa huko Ufaransa akiongea lugha ya ajabu. Alionesha sehemu aliyotoka kuwa Lisbon Ureno japo lugha haikuwa ya Kireno pia yeye alionesha kuwa sio mreno bali ni kutoka nchi ya 'Lizbonia'.

Nataka kujua je, ni kweli kwamba kuna milango ya siri ambapo ukiingia unaweza kukuta nchi nyingine kama hizi za Lizbonia na Taured?

Asante na karibu tujuzane.
Dunia hii inatisha Sana mkuu, kuna mdogo wangu sasa hivi ni marehemu aliwahi kupotea kijijini kwetu usiku ktk mazingira ya utata Sana, tulimtafuta kila sehemu hatukumwona, alikuwa na miaka 8 tu kipindi kile, tulipokata tamaa na kurudi nyumbani ili tujipange upya mida ya saa 9 alfajiri, marehemu mama alifungua chumba kilichokuwa kimefungwa muda mrefu na tukamkuta amekaa humo akiwa kimya haongei lolote, hadi alipokuja kuwa mtu mzima na kujitambua ,aligoma kabisa kusema alikuwa wapi hadi anafariki.
 
Alika
Dunia hii inatisha Sana mkuu, kuna mdogo wangu sasa hivi ni marehemu aliwahi kupotea kijijini kwetu usiku ktk mazingira ya utata Sana, tulimtafuta kila sehemu hatukumwona, alikuwa na miaka 8 tu kipindi kile, tulipokata tamaa na kurudi nyumbani ili tujipange upya mida ya saa 9 alfajiri, marehemu mama alifungua chumba kilichokuwa kimefungwa muda mrefu na tukamkuta amekaa humo akiwa kimya haongei lolote, hadi alipokuja kuwa mtu mzima na kujitambua ,aligoma kabisa kusema alikuwa wapi hadi anafariki.
alikaa humo ndani kwa muda gani? Naje Mlango ulifungwa kwa komeo Na kufuli? Maana mtoto wa miaka nane anakili za kutosha
 
Dunia hii inatisha Sana mkuu, kuna mdogo wangu sasa hivi ni marehemu aliwahi kupotea kijijini kwetu usiku ktk mazingira ya utata Sana, tulimtafuta kila sehemu hatukumwona, alikuwa na miaka 8 tu kipindi kile, tulipokata tamaa na kurudi nyumbani ili tujipange upya mida ya saa 9 alfajiri, marehemu mama alifungua chumba kilichokuwa kimefungwa muda mrefu na tukamkuta amekaa humo akiwa kimya haongei lolote, hadi alipokuja kuwa mtu mzima na kujitambua ,aligoma kabisa kusema alikuwa wapi hadi anafariki.
Hii n stori ya kutisha nilioisoma leo
 
Dunia hii inatisha Sana mkuu, kuna mdogo wangu sasa hivi ni marehemu aliwahi kupotea kijijini kwetu usiku ktk mazingira ya utata Sana, tulimtafuta kila sehemu hatukumwona, alikuwa na miaka 8 tu kipindi kile, tulipokata tamaa na kurudi nyumbani ili tujipange upya mida ya saa 9 alfajiri, marehemu mama alifungua chumba kilichokuwa kimefungwa muda mrefu na tukamkuta amekaa humo akiwa kimya haongei lolote, hadi alipokuja kuwa mtu mzima na kujitambua ,aligoma kabisa kusema alikuwa wapi hadi anafariki.
hebu jazia Nyama vyema ...huo mkasa ulikuwaje ""?? kuwaje ? mmmh
 
Back
Top Bottom