Kiranga sio atheist ni non-believer

Kiranga sio atheist ni non-believer

Kuna mwingne alinambia kuwa adam ni zinjathropas je kuna ukweli wowote?
Zinjathropus na adam ni imscible liquid havitakuja kufanana daima,zinjathropus fuvu lake aligunduliwa tanzania oldivai wakati huyo adam inaonekana alikuwa ni muebrania aliishi mashariki ya kati na alikufa huko kwa maelezo ya biblia hajaweza kuja afrika mashariki
 
Muktadha wa akili ni akili unaelewa nini?
Labda tuanze mwanzo mwa tatizo ili tupate kuelewana.

Hivi swali la "Una akili?" ni wapi ambapo hapajaeleweka? kwa mfano nikikuuliza una akili? ni kipi kitakushinda kuelewa?
 
Hadi sasa hivi hujatoa tafsiri ya maneno ambayo umeyaandika na tayari nimeshakwambia lakini umekimbia kutoa tafsiri

Umeandika unavyojua wewe maneno ulikoyatoa.
Umesema niwe specific nime quote tena na tena comment yako lakin umekaa kimya kuhusu hilo
Kiranga hajawahi kukimbia changamoto wala swali.

Kama hajui jibu atakwambia tu hajui.

Sio kamaMshana, unamwambia ajibu akili ni nini, anajibu akili ni akili, bwahahaha.

Nakujibu hivi.

Naweka maneno nilivyoyaandika Kiingereza, halafu natafsiri Kiswahili chini.

Usije kuomba tafsiri ya lugha ya kabila yenu tu hapa.

Kiingereza

By convergence, the mathematics needed to resolve the nature and beginning of the universe in the singularity at the big bang, according to the best known current theories, can be narrowed down to reconciling Einstein's Relativity, which deals with the science of the very big/heavy and quantum theory, which deals with the very small.

This is because, at the singularity, all the matter of the universe is condensed into an infinitesimally small space -the primordial beginning of our spacetime, necessitating a conundrum of the very dense/ large mass (Einstein's Relativity)in an infinitesimally small space (Quantum Physics).

Without coming up with the mathematics of reconciling Relativity and Quantum Physics, which has not been done todate, the beginning of the universe will remain unknown.

Tafsiri ya Kiswahili

Kwa kujongea kwenye kukutana, hisabati zinazohitajika kutatua asili na mwanzo wa ulimwengu katika ajabu la mwanzo wa ulimwengu lililotokea kwenye Mshindo Mkubwa, kwa mujibu wa nadharia nzuri kabisa zinazojulikana sasa, zinaweza kubanwa zaidi ndani ya maafikiano kati ya nadharia ya Einstein ya Uwiano, ambayo inafanya kazi na sayansi ya vitu vikubwa sana/ vizito sana, na Nadharia ya Kwanta, ambayo inahusika na vitu vidogo sana.

Hii ni kwa sababu, kwenye maajabu ya mwanzo wa ulimwengu, mada yote ya ulimwengu ilibanwa katika eneo dogo isivyomithilika - mwanzo wa sili wa eneomuda wetu, kusababisha kizungumkuti cha mada iliyo ngumu/ kubwa (Uwiano wa Einstein unahusika hapo) iwe kwenye eneo dogo sana (Fizikia ya Kwanta inahusika)

Bila ya kupata hisabati zitakazotatua kitendawaili cha kuunganisha Uwiano wa Einstein na Fizikia ya Kwanta, kitu ambacho bado hakijawezekana kufanyika mpaka leo, mwanzo wa ulimwengu utabaki haujulikani
 
Labda tuanze mwanzo mwa tatizo ili tupate kuelewana.

Hivi swali la "Una akili?" ni wapi ambapo hapajaeleweka? kwa mfano nikikuuliza una akili? ni kipi kitakushinda kuelewa?
Ulipaswa uelezee akili ipi unazungumzia ndyo maana likaja swali la akili ni nini?

Kwa kuwa wapo waliojibu akili ni nini, tukaweza kuwaelewa, tukasema tunazo au hatuna,

Lakini mtu unauliza una akili au hauna akili, hicho ulichouliza hauwezi kukielezea sasa unategemeaje kujibiwa na ukaelewa jibu?

Akili maana yake ni nini?
Akili ni nini?
 
Naingia mochwari nitarejea
Mkuu kumbe medicine unaijua una maana gani kuuliza swali kama hili?
Akili ni uwezo wa kuelewa jambo,kufikiri na kukumbuka
Ndio ktk medicine kipengele cha hx taking huwa tuna test mental status na si akili kama mtu yupo conscious na utaona anaulizwa kama yupo oriented to time,place na person na pia ataulizwa short and long memory,
Lakn unaposema mtu hana akili una maana gani maana akili yenyewe ipo muda wote kwa maana hiyo huwezi sema mtu hana akili bora useme mtu hana uwelewa au ufikiri au useme mtu ana matatizo ya akili psychotic disoder,epilepsy
 
Labda tuanze mwanzo mwa tatizo ili tupate kuelewana.

Hivi swali la "Una akili?" ni wapi ambapo hapajaeleweka? kwa mfano nikikuuliza una akili? ni kipi kitakushinda kuelewa?
Kuna watu washanijibu akili ni nini. Nikawajibu nina au sina akili kwa muktadha wao.

Mmoja kasema akili ni kutambua uwepo wa Mungu.

Nikamwambia kwa muktadha huo sina akili. Kwa sababu sitambui uwepo wa Mungu.

Mwingine akaniambia akili ni uwezo wa kupambanua mambo positive na negative. I am paraphrasing.

Nikamwambia kwa muktadha huo akili ninayo kwa sababu nimeweza kudadavua dhana ya kuwepo kwa Mungu kwa "proof by contradiction" iliyoanza kama nakubali Mungu yupo (positive) nikaichambua dhana ya kuwepo Mungu nikaona contradictions ambazo hazijibiki. Nikaishusha na kuikataa (negative)

Sasa hapo utaona watu wawili tofauti wame define akili kwa namna mbili tofauti, na wote nimewapa majibu yao kwa mujibu wa muktadha walioutoa katika definition ya akili.

Sikuogopa kuwajibu.

Majibu yapo wazi kwenye uzi huu huu. Kila mtu anaweza kuyasoma.

Kwa hiyo hii dhana ya kwamba Kiranga anaogopa kujibu, Kiranga hataki kujibu si ya kweli.

Tatizo nitajibu vipi swali ambalo halijafafanuliwa?

Hao wawili wamefafanua akili ni nini na nimewajibu. Kwa mujibu wa ufafanuzi wao.

Sasa kwa nini Mshana hataki kusema akili ni nini nimjibu?
 
Knuni za definition zinakataza kurudia neno linalokuwa defined katika sehemu ya definition inayolielezea neno hilo.

Nikukuuliza "akili ni nini?" unatakiwa unielezee akili ni nini kwa maneno mengine.

Ukiniambia "akili ni akili" wakati hilo neno akili ndilo ambalo silijui, nahitaji ufafanuzi nilielewe, utakuwa hujafafanua kitu.

Mbona mnaandika kama ng'ombe msiojua kitu?

Mtu akiniuliza, nimeona umetumia hili neno "schadenfreude", sielewi ni nini manaa yake hapa ulivyolitumia.

Schadenfreude ni nini?

Nikimjibu "schadenfreude ni schedenfreude" wakati yeye anataka ufafanuzi kuhusu hilo neno "schadenfreude" atawezaje kujua zaidi maana ya hilo neno, wakati hilo neno ndilo ambalo kaomba ufafanuzi walo?
Umeulizwa una akili? badala ya kujibu matokeo yake ukaanza kutaka muuliza swali akueleze ametumia neno akili kwa muktadha gani.

Hakuna uliposema hulijui neno akili.
 
Unachokataa nini sasa wakati umetaka ujibiwe kwa muktadha wake?
Kujibiwa kwa muktadha wake ni kutoa maana ya akili kwa muktadha wake bila kutumia neno akili katika kulielezea neno akili.

Kusema "akili ni akili" si kujibu kwa muktadha wake, kwa sababu si kujibu kabisa.
 
Umeulizwa una akili? badala ya kujibu matokeo yake ukaanza kutaka muuliza swali akueleze ametumia neno akili kwa muktadha gani.

Hakuna uliposema hulijui neno akili.
Akili ni nini?

Hamjajibu swali hili.

Kwa nini linakuwa swali gumu sana kwenu?

Kwa nini mnaliogopa?
 
Ulipaswa uelezee akili ipi unazungumzia ndyo maana likaja swali la akili ni nini?

Kwa kuwa wapo waliojibu akili ni nini, tukaweza kuwaelewa, tukasema tunazo au hatuna,

Lakini mtu unauliza una akili au hauna akili, hicho ulichouliza hauwezi kukielezea sasa unategemeaje kujibiwa na ukaelewa jibu?

Akili maana yake ni nini?
Akili ni nini?
Hauwezi kutaka kujua aina za kitu fulani bila kujua hicho kitu ni nini.

Ukitaka kujua aina za simu lazima kwanza ujue simu ni nini,na mwenye kujua simu ni nini akitaka kujua aina za simu hawezi kuuliza tena simu ni nini.

Sasa nyie mnataka kujua et akili ipi inazungumziwa halafu mnauliza akili ni nini?!!!!!
 
Akili ni nini?

Hamjajibu swali hili.

Kwa nini linakuwa swali gumu sana kwenu?

Kwa nini mnaliogopa?

Baadhi hawajakujibu, kuna wengine wamejibu au kuelezea maana ya akili kwa wanavyoelewa wao. Na mimi nikiwa mmoja wao.

Unamaanisha nini unaposema "mnaliogopa" na "...swali gumu sana kwenu..."? unawalenga akina nani hapo?
 
Baadhi hawajakujibu, kuna wengine wamejibu au kuelezea maana ya akili kwa wanavyoelewa wao. Na mimi nikiwa mmoja wao.

Unamaanisha nini unaposema "mnaliogopa" na "...swali gumu sana kwenu..."? unawalenga akina nani hapo?
Mshana na watetezi wake.

Waambie kwamba swali jepesi tu mbona wewe umejibu na tumeendelea na mjadala hujapata kidonda wala kutokwa damu?

Wameusimamisha mjadala kwa swali ambalo halina uzito wowote.

Ndiyo maana nasema hawana hoja.
 
Mshana na watetezi wake.

Waambie kwamba swali jepesi tu mbona wewe umejibu na tumeendelea na mjadala hujapata kidonda wala kutokwa damu?

Lakini kwangu hatukuendelea na pale tulipoachia mkuu, imekua kama ule mchezo wa chess.
 
Kuna watu washanijibu akili ni nini. Nikawajibu nina au sina akili kwa muktadha wao.

Mmoja kasema akili ni kutambua uwepo wa Mungu.

Nikamwambia kwa muktadha huo sina akili. Kwa sababu sitambui uwepo wa Mungu.

Mwingine akaniambia akili ni uwezo wa kupambanua mambo positive na negative. I am paraphrasing.

Nikamwambia kwa muktadha huo akili ninayo kwa sababu nimeweza kudadavua dhana ya kuwepo kwa Mungu kwa "proof by contradiction" iliyoanza kama nakubali Mungu yupo (positive) nikaichambua dhana ya kuwepo Mungu nikaona contradictions ambazo hazijibiki. Nikaishusha na kuikataa (negative)

Sasa hapo utaona watu wawili tofauti wame define akili kwa namna mbili tofauti, na wote nimewapa majibu yao kwa mujibu wa muktadha walioutoa katika definition ya akili.

Sikuogopa kuwajibu.

Majibu yapo wazi kwenye uzi huu huu. Kila mtu anaweza kuyasoma.

Kwa hiyo hii dhana ya kwamba Kiranga anaogopa kujibu, Kiranga hataki kujibu si ya kweli.

Tatizo nitajibu vipi swali ambalo halijafafanuliwa?

Hao wawili wamefafanua akili ni nini na nimewajibu. Kwa mujibu wa ufafanuzi wao.

Sasa kwa nini Mshana hataki kusema akili ni nini nimjibu?
Suala hapa limetumika neno akili,na lina maana yake kama neno la kiswahili.

Sasa sijajua ilikuaje wewe ukaanza kutaka ufafanuzi,ndiyo maana nataka kujua hilo neno lina utata gani? kila neno lina maana yake.
hata kila mtu akilielezea ila hawaondoi maana ya hilo neno husika.

Halafu hakuna aliyesema akili ni kutambua uwepo wa mungu...nimerudia sana kusema hili.
 
Akili ni nini?

Hamjajibu swali hili.

Kwa nini linakuwa swali gumu sana kwenu?

Kwa nini mnaliogopa?
Mimi sina muda wa kufanya utoto.

Umeulizwa swali umekwepa kujibu,huo ndio ukweli hizo habari za muktadha hazina mashiko kabisa.
 
Suala hapa limetumika neno akili,na lina maana yake kama neno la kiswahili.

Sasa sijajua ilikuaje wewe ukaanza kutaka ufafanuzi,ndiyo maana nataka kujua hilo neno lina utata gani? kila neno lina maana yake.
hata kila mtu akilielezea ila hawaondoi maana ya hilo neno husika.

Halafu hakuna aliyesema akili ni kutambua uwepo wa mungu...nimerudia sana kusema hili.
Una hakika?
 
Hadi sasa hivi hujatoa tafsiri ya maneno ambayo umeyaandika na tayari nimeshakwambia lakini umekimbia kutoa tafsiri

Umeandika unavyojua wewe maneno ulikoyatoa.
Umesema niwe specific nime quote tena na tena comment yako lakin umekaa kimya kuhusu hilo
Hiyo ndio mbinu yake pendwa
 
Na ww naomba unijibu kuwa adam ni mtu wa kwanza umepata wapi habari hii lete ushahidi kokote
Msaidie kujibu kwanza swali kongwe! Hivi na maarifa yenu yote mnayojivunia kuwa nayo (kama ni kweli) mpaka leo hii mmeshindwa kabisa kujibu kama mna akili ama hamna? HILI LAWEZA KUWA AJABU KUU NANE LA DUNIA....
Nijibu wewe kama una AKILI ama huna nitakupa ushahidi Adam kuwa binadamu wa kwanza!
Nimeulizwa AKILI ninini nimejibu ni AKILI.. Kama hili sio jibu sahihi naomba nipewe jibu sahihi... Hapa pia hakuna kitu!
 
Back
Top Bottom