Kipilimba, Umekubali kuvuliwa nguo?

Mission Accomplished
IMG-20190912-WA0015.jpeg
 
Leo tena mimi na wewe mzee wangu, usije kudhani nakuchukia baada ya wiki iliyopita kukuandikia makala nyingine. La hasha, ila nakuonea huruma sana. Ni Kama hujui umuhimu na uzito wa kazi ulionao.

Musiba si mjinga wala kichaa kama watu wanavyodhania, bali kuna mtu mwenye nguvu kubwa kuliko wote Tanzania ndo yupo nyuma ya Musiba.

Maneno anayoongea Musiba, hayaongei kwa bahati mbaya au kwa kuhisi, bali ni mkakati maalumu mzito ili kufanikisha jambo maalumu zito.

Bahati mbaya zaidi ofisi yako inadhalilishwa na Musiba, huyu ni mtu Hatari sana ambaye idara yako ilitakiwa kumnyamazisha kimya hata kwa njia zisizojulikana Kwa ajili ya usalama wa nchi.

Musiba amekuwa msiba Kwa watu, hivi hujui athari ya kauli zake na tuhuma zake Kwa watu zinaweza kuchafua usalama wa nchi?

Huyu mtu amefikia hatua ya kuwagusa hadi marais wastaafu. Unadhani ni hali ya kawaida hiyo?

Wewe Kama Mkurugenzi mkuu wa TISS, unajua majukumu yako, hakuna wa kukufundisha kazi, ila hali ilivyo inaonyesha kabisa unafundishwa kazi.

Hivi unajua kuwa vita vya ghuba vilisababishwa na mtu kama Musiba, mkimbizi wa Iraq aliyekuwa akiishi Germany?

Musiba kaumiza wengi, na anaendelea kuwaumiza, na hakuna wa kumgusa huyu mtu, yupo juu ya sheria, a strong man is behind him.

Kwanini TISS imekosa uadilifu mikononi mwako?

Nakushauri u resign ili ulinde heshima yako, vinginevyo utaendelea kuvuliwa nguo.

Nilitarajia ungeiendesha Idara kwa muundo wa CIA, MI6 au Mossad, haya mashirika yapo Kwa maslahi ya mataifa yao na watu wao, na hayatumiki na wanasiasa uchwara.

Watu wanahangaika kuipasua Tanzania, upo umekaa unawatizama tu.

Kwa hiyo unasubiri kushuhudia Tanzania ikipasuliwa na wakati uwezo wa kuzuia unao? Ni kituko cha karne mtu mmoja tu anayejiita mwanaharakati anafanya lolote atakalo na hakuna wa kumgusa.

Yetu macho, siku mkianza kuvuna mnachopanda msikimbie.
Tusipoteze muda kujadili mambo ambayo ni implied badala ya factual events. Wastaafu wanaojiita wazee wa kuheshimika wanasema Musiba, Kipilimba kuhamishwa unasema Musiba. Baadaye utasema hata Diwani kuhamishwa ni Musiba, Nape kuomba radhi ni Musiba. Let’s not waste good reasoning. Ulivyoanza kuandika ni kama ulitaka kumjadili Kipilimba, lakini uliishia kuandika Musiba. Musiba tumeshamjadili sana hapa JF. Ubora wake, umuhimu wake, vyanzo vyake vya taarifa, n.k.
 
JF ina mambo mengi...Duh! Kumbe nilikuwa sahihi kabisa, kueleza hapo awali kuwa Kuifungia JF ama kuihujumu JF nikutokujitakia mema. Ila Dr ni 'kichwa'...niliwahi kusikiliza mahojiano yake kabla ya kupewa nafasi ile...ana'tiririka vizuri'...!
 
Back
Top Bottom