kavulata
JF-Expert Member
- Aug 2, 2012
- 12,319
- 12,622
Kuna mtu anajifariji kwa kusema Simba ni kubwa kuliko Chama, ni sawa lakini Chama ni Bora kuliko Wachezaji wote wa Simba, Tanzania na Afrika. Chama alishaondoka Simba kwenda Uarabuni Simba ikakosa ubingwa kwa misimu 2 hadi wakaenda kumtafuta kwa hali na mali kwa udi na uvumba arudi kikosini. Tabia na maisha anayoishi Chama ni yaleyale na vilevile alivyokuwa anaishi tangu ajiunge na Simba. Lakini mara hii kilichobadilika kwake ni kipigo Cha goli 5 alichopigwa Simba na Chama akiwemo kwenye play list.
Chama Hana utovu wa nidhamu hata kidogo, kama timu ingekuwa inashinda mechi zote tusingesikia habari za Chama maana amekuwa akiishi na kufanya hivihivi lakini viongozi walivumilia na kuzoea kwakuwa alikuwa akiishindia timu.
Kwanini walimrudisha Chama kama Chama sio mkubwa? Maana yake walitafutaweeeee Wachezaji wengine walikosa hadi wakarudi kuwapigia magoti Chama na Miquison warudi kuinusuru Simba. Shida sio Chama bali uzee wa Wachezaji muhimu Simba. Kipigo Cha goli 5 kitawasambaratisha kama hamtakubali haraka kama imetokea.
Mlimlea hivyo Wacha awe hivyo, hakuna utovu wa nidhamu ila Kuna kipigo Cha goli 5.
Chama Hana utovu wa nidhamu hata kidogo, kama timu ingekuwa inashinda mechi zote tusingesikia habari za Chama maana amekuwa akiishi na kufanya hivihivi lakini viongozi walivumilia na kuzoea kwakuwa alikuwa akiishindia timu.
Kwanini walimrudisha Chama kama Chama sio mkubwa? Maana yake walitafutaweeeee Wachezaji wengine walikosa hadi wakarudi kuwapigia magoti Chama na Miquison warudi kuinusuru Simba. Shida sio Chama bali uzee wa Wachezaji muhimu Simba. Kipigo Cha goli 5 kitawasambaratisha kama hamtakubali haraka kama imetokea.
Mlimlea hivyo Wacha awe hivyo, hakuna utovu wa nidhamu ila Kuna kipigo Cha goli 5.