Kipi kitangulie, heshima au upendo?

Kipi kitangulie, heshima au upendo?

Tuwapende watoto, tuteseke kwa ajili ya furaha yao. Ilimradi sisi tunajua ujumbe gani tunawapa, itawajenga vema kwenye makuzi.

Heshima haikuji kwa kunyanyasa wanyonge!
 
Bongo mtoto hana haki popote pale, anzia nyumbani hadi shuleni!
 
Unadhani tatizo ni nauli basi, sio kweli!

Ukitaka kuamini hilo, siku usafiri na mtoto halafu mlipie nauli kamili kisha tulia.

Utaona venye watu wanamtazama kwa jicho la kuitamani siti yake, wapo wataodiriki kumfokea awapishe kabla wajue kama amelipa nauli kamili.

Mzazi utaonekana unamkingia kifua mwanao na kwamba unamfunza utovu wa nidhamu, pengine itakulazimu kutoa maelezo ya kuwa ‘siti imelipiwa’ kila itapotokea kuna mwamba anajisogeza.

Ni ubinafsi tu au kutokujali watoto wetu.

Kuna wakati huwa natembea na mwanangu tena ana 4yrs namlipia nauli hakuna anayehoji, labda akitaka kukaa ataomba ambebe!!!.

Zamani ndio tulikuwa tunasema kwaajili ya heshima lakini sasa kitu ni nauli bwana.

Wapo wanafunzi wanalipa ya mtu mzima wala hawasimamishwi....wala konda hahoji apishe mzima.
 
Swala si heshima wala upendo

Suala ni nauli 200

Mwanafunzi akilipa nauli ya mtu mzima hakuna anayehangaika kumsimamisha!!!

Ni kweli huwa nawaonea huruma sana watoto hawa, huchoka nao kama sisi watu wazima ila mfumo wetu wa ulipaji nauli ndio unawagharimu.

Mzazi kama unaweza mpe mwanao nauli ya mtu mzima tu.
Hapo unahamia kwenye upande mwingine, kuwa unathaminiwa kwa kile ulichonacho lakini jamii yetu hatuwezi kuishi kwa mambo kama hayo,

Mtoto mdogo kistaarabu kabisa unatakiwa upishe kiti mkubwa wako akae, umri unavyoenda nguvu pia hupungua sasa kwa kijana mwenye nguvu kabisa unaweza simama hata masaa matatu bila kuchoka unaweka ligi ni mtu mzima kweli? Upendo ndiyo kila kitu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ndugu zangu!

Nipo kwenye usafiri wa umma almaarufu daladala. Basi kuna watoto, ngoja niite wanafunzi kwa mujibu wa nauli yao lakini hawajavaa sare za shule. Miaka 8-10 hivi.

Basi, gari halijajaa vema kuna viti kadhaa konda anaendelea kuita abiria. Mara gari likaanza kuchapa mwendo huku wale watoto wamesimama japo viti vipo wazi.

Hakuna anayeshangaa, hata kwangu sio jambo geni. Ila imenipa muda wa kuwaza kidogo.

Hivi, hii tabia ya kuwainua watoto wasikae ina misingi gani?

Kama ni heshima, tunadhani ni kwa ridhaa ya mtoto au tunamlazimisha atuheshimu?

Ikumbukwe mtoto yupo kwenye umri wa kujifunza, mfano huyo mwanafunzi. Anahitaji zaidi kuoneshwa upendo ili ajisikie faraja, mfano hapo anatoka shule kama ni kuchoka naye amechoka vile vile.

Hii kwa wengi imekuwa kawaida na hakuna anayejali, hata ikitokea amekaa atafurumushwa na konda na abiria watamshangaa mtoto kakosa adabu!

Hii imekaaje?

Tunataka kupewa heshima, tunasahau yatupasa kuonesha upendo... ukisimama mtoto akae hupungukiwi na kitu.

Kipi muhimu, kipi kianze? Kwangu upendo kwanza, kwako Je!

Wasalaam,

Ncha Kali.
Upendo ukitangulia na hekima hufuata, burasa pia na hata heshima.. Upendo ni muhimili mkubwa sana unaojitegemea, vingine vinategemeana,

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tafuta hela kaka
Hapo hujamjibu sawia,

Hela ndiyo inaweza kukufanya ukaishi maisha mazuri lakini ni vitu vya muda tu kuna wakati unaweza ukawa nazo na wakati mwingine usiwe nazo,

Ila sasa upendo ni dawa upendo ni nguzo ya mambo yote, ukiwa na upendo kila kitu duniani kitakua chako, utaheshimika, utapendwa utabarikiwa, utaisha maisha ya furaha hata kama mfukoni huna kitu,

Tujifunze sana kuthaminisha utu kuliko mali za duniani, kwanza mali za duniani ni mali ya bwana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mtoto mdogo kistaarabu kabisa unatakiwa upishe kiti mkubwa wako akae, umri unavyoenda nguvu pia hupungua sasa kwa kijana mwenye nguvu kabisa unaweza simama hata masaa matatu bila kuchoka unaweka ligi ni mtu mzima kweli? Upendo ndiyo kila kitu.

Umeongea vema mkuu, ila nahisi umechanganya mtu mzima na Mzee... hapa kesi ni tofauti kwa wazee ambao hata mimi huwapisha.

Hoja mezani ni mtoto mdogo, mfano miaka 6 hadi 10 dhidi ya mtu mzima say 15 to 40 years.... huo upendo auoneshe mtoto au huyu mkubwa?
 
Kuna wakati huwa natembea na mwanangu tena ana 4yrs namlipia nauli hakuna anayehoji, labda akitaka kukaa ataomba ambebe!!!.

Zamani ndio tulikuwa tunasema kwaajili ya heshima lakini sasa kitu ni nauli bwana.

Wapo wanafunzi wanalipa ya mtu mzima wala hawasimamishwi....wala konda hahoji apishe mzima.
Ni mitazamo isiyo na upendo kabisa, kuwa na hela haiwezi ikakunyima kuwa na upendo, hata kama unalipa laki moja kwenye siti ila kama una upendo unaweza ukampisha mtu mzima ukamwambia akae, utapungukiwa nini hasa?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Dereva huwa anatangaza wanafunzi pisheni wakubwa wakae.
Ila wanawake sishangai hii kitu ni hulka yenu kabisa kwa baadhi yenu,

wewe uliokaa unaweza ukamuona mwanamke mwanzako ambae ni mjauzito kasimama tena tumbo kubwa na anasimama kwa shida kabisa kwenye daladala huwa hata hampishi, ni mpaka wanaume unakuta tunanyanyuka na kumpa nafasi/kiti, sijui mpoje nyie watu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hapo hujamjibu sawia,

Hela ndiyo inaweza kukufanya ukaishi maisha mazuri lakini ni vitu vya muda tu kuna wakati unaweza ukawa nazo na wakati mwingine usiwe nazo,

Ila sasa upendo ni dawa upendo ni nguzo ya mambo yote, ukiwa na upendo kila kitu duniani kitakua chako, utaheshimika, utapendwa utabarikiwa, utaisha maisha ya furaha hata kama mfukoni huna kitu,

Tujifunze sana kuthaminisha utu kuliko mali za duniani, kwanza mali za duniani ni mali ya bwana

Sent using Jamii Forums mobile app


Oh
 
Ila wanawake sishangai hii kitu ni hulka yenu kabisa kwa baadhi yenu,

wewe uliokaa unaweza ukamuona mwanamke mwanzako ambae ni mjauzito kasimama tena tumbo kubwa na anasimama kwa shida kabisa kwenye daladala huwa hata hampishi, ni mpaka wanaume unakuta tunanyanyuka na kumpa nafasi/kiti, sijui mpoje nyie watu

Sent using Jamii Forums mobile app

Sijui kwanini hii kitu mnaiweka kama ni jukumu la wanawake kupisha mwanamke mwenzake......huwa nawashangaa nyie wanaume basi tu.

Kwanini iwe mwanamke ndio ampishe mwanamke mwenzake? Kwanini isiwe mwanaume ampishe mkewe ama mama yake aliyemweka tumboni?

Anyway waswahili wanasema nyani haoni kundule.....!!!!

Tupendane wote hili swala lisiwe gender issue liwe la wote.

Japo mi nikijiona ni mjamzito ama nina mtoto huwa sithubutu kupanda gari lililojaa, ili nionewe huruma...na kwakweli Kama Kuna mtu anapanda mwanzo wa gari ana mtoto au mjamzito huwa simpishi....najua kafanya makusudi ili aonewe huruma.....labda apandie njiani ambako najua wazi hawezi pata siti.
 
Hapo unahamia kwenye upande mwingine, kuwa unathaminiwa kwa kile ulichonacho lakini jamii yetu hatuwezi kuishi kwa mambo kama hayo,

Mtoto mdogo kistaarabu kabisa unatakiwa upishe kiti mkubwa wako akae, umri unavyoenda nguvu pia hupungua sasa kwa kijana mwenye nguvu kabisa unaweza simama hata masaa matatu bila kuchoka unaweka ligi ni mtu mzima kweli? Upendo ndiyo kila kitu.

Sent using Jamii Forums mobile app

Si kweli hawa watoto huchoka sana...tena wengine ni wadogo hawana hata nhuvu unazosema.

Imagine ameamka saa 11 kamwenda shule kanarudi saa 12 unakasimamisha toka kivukoni mpaka mbezi.....daaa kisa tu heshima.....hapana bwana.

Huu mfumo haujakaa sawa.
 
Ni mitazamo isiyo na upendo kabisa, kuwa na hela haiwezi ikakunyima kuwa na upendo, hata kama unalipa laki moja kwenye siti ila kama una upendo unaweza ukampisha mtu mzima ukamwambia akae, utapungukiwa nini hasa?

Sent using Jamii Forums mobile app

Upendo upo kwa kumpisha mtu mzima tu?

Hoja ya mtoa mada je hawa watoto hawapaswi kupendwa kwa kuachiwa viti wakae na mkubwa asimame?

Upendo huu bongo hiii....tunaopigana vikumbo kugombea siti? Au foleni?

Tena nyie wanaume ndio kabisaa utakuta unawapush wanawake bila kujali....au utaona wenzio wako kwenye foleni ila utapitiliza mbele...!!!

Upendo bado sana TZ yetu.
 
Upendo upo kwa kumpisha mtu mzima tu?

Hoja ya mtoa mada je hawa watoto hawapaswi kupendwa kwa kuachiwa viti wakae na mkubwa asimame?

Upendo huu bongo hiii....tunaopigana vikumbo kugombea siti? Au foleni?

Tena nyie wanaume ndio kabisaa utakuta unawapush wanawake bila kujali....au utaona wenzio wako kwenye foleni ila utapitiliza mbele...!!!

Upendo bado sana TZ yetu.
Weeeee Englishfigure, hebu ngoja kwanza

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Upendo upo kwa kumpisha mtu mzima tu?

Hoja ya mtoa mada je hawa watoto hawapaswi kupendwa kwa kuachiwa viti wakae na mkubwa asimame?

Upendo huu bongo hiii....tunaopigana vikumbo kugombea siti? Au foleni?

Tena nyie wanaume ndio kabisaa utakuta unawapush wanawake bila kujali....au utaona wenzio wako kwenye foleni ila utapitiliza mbele...!!!

Upendo bado sana TZ yetu.
Kila jambo hutazamiwa kwa namna yake, hapo umesema wanawake sasa mwanamke yupi unamzungumiza hapo, je ni wa miaka 18
ila pia unasema upendo Bongo?!?? Duh hivi kuna nchi tunapendana kama wa Tz, nenda kenya nenda uganda nenda mataifa mengine hujazunguka mataifa mengine ndiyo maana unasema hivyo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom