Ncha Kali
JF-Expert Member
- Sep 19, 2019
- 15,400
- 29,339
Ndugu zangu!
Nipo kwenye usafiri wa umma almaarufu daladala. Basi kuna watoto, ngoja niite wanafunzi kwa mujibu wa nauli yao lakini hawajavaa sare za shule. Miaka 8-10 hivi.
Basi, gari halijajaa vema kuna viti kadhaa konda anaendelea kuita abiria. Mara gari likaanza kuchapa mwendo huku wale watoto wamesimama japo viti vipo wazi.
Hakuna anayeshangaa, hata kwangu sio jambo geni. Ila imenipa muda wa kuwaza kidogo.
Hivi, hii tabia ya kuwainua watoto wasikae ina misingi gani?
Kama ni heshima, tunadhani ni kwa ridhaa ya mtoto au tunamlazimisha atuheshimu?
Ikumbukwe mtoto yupo kwenye umri wa kujifunza, mfano huyo mwanafunzi. Anahitaji zaidi kuoneshwa upendo ili ajisikie faraja, mfano hapo anatoka shule kama ni kuchoka naye amechoka vile vile.
Hii kwa wengi imekuwa kawaida na hakuna anayejali, hata ikitokea amekaa atafurumushwa na konda na abiria watamshangaa mtoto kakosa adabu!
Hii imekaaje?
Tunataka kupewa heshima, tunasahau yatupasa kuonesha upendo... ukisimama mtoto akae hupungukiwi na kitu.
Kipi muhimu, kipi kianze? Kwangu upendo kwanza, kwako Je!
Wasalaam,
Ncha Kali.
Nipo kwenye usafiri wa umma almaarufu daladala. Basi kuna watoto, ngoja niite wanafunzi kwa mujibu wa nauli yao lakini hawajavaa sare za shule. Miaka 8-10 hivi.
Basi, gari halijajaa vema kuna viti kadhaa konda anaendelea kuita abiria. Mara gari likaanza kuchapa mwendo huku wale watoto wamesimama japo viti vipo wazi.
Hakuna anayeshangaa, hata kwangu sio jambo geni. Ila imenipa muda wa kuwaza kidogo.
Hivi, hii tabia ya kuwainua watoto wasikae ina misingi gani?
Kama ni heshima, tunadhani ni kwa ridhaa ya mtoto au tunamlazimisha atuheshimu?
Ikumbukwe mtoto yupo kwenye umri wa kujifunza, mfano huyo mwanafunzi. Anahitaji zaidi kuoneshwa upendo ili ajisikie faraja, mfano hapo anatoka shule kama ni kuchoka naye amechoka vile vile.
Hii kwa wengi imekuwa kawaida na hakuna anayejali, hata ikitokea amekaa atafurumushwa na konda na abiria watamshangaa mtoto kakosa adabu!
Hii imekaaje?
Tunataka kupewa heshima, tunasahau yatupasa kuonesha upendo... ukisimama mtoto akae hupungukiwi na kitu.
Kipi muhimu, kipi kianze? Kwangu upendo kwanza, kwako Je!
Wasalaam,
Ncha Kali.


