Sana mkuu kuoa ni ufungwa
Kama umeoa na ulikosea basi mfungwa ni wewe si ndoa. Kama hujaoa huku unashauri kitu ambacho hujui uchungu wala utamu wake basi una tatizo unaitaji msaada.
Nani asiyetaka kupiga honi jioni halafu geti likifunguliwa anawaona watoto wake wote na ile nyimbo ya dady dady, huku wife akiwa keshakuandalia supu ya kuku na hii baridi?
Changamoto za ndoa zipo ila raha ni nyingi zaidi. Mradi Usiwe maskini tu, na pia usiwe mtu wa kupenda penda ngono sana za nje halafu uwe na mwanamke wa kawaida, mwerevu na mwenye hofu ya MUNGU.
Tatizo la vijana mnataka sana hawa wenye degree za udangaji, Mwanamke ana ma Long ex 6(Aliishi nao kama mke na mume) na short x 80( Wamepiga na Kusepa) unategemea nini kama si kifungo?
Ukiona una mwanamke mda wote macho juu akidhani unacheat ujue umeoa mzoefu wa hayo mambo. Mwanamke wako anatakiwa awe innocent and busy kiasi kwamba ubongo una nafasi ndogo sana ya kuwaza mambo nje ya watoto wake, ndoa yake na biashara zenu.
Jipunguzie matatizo pia, usioe mwanamke anayetongozeka kirahisi. Mwanamke anageuza kila shingo ya mwanaume, Tembo ni mzuri kumwangalizia huko huko porini si umfuge nyumbani. Nenda kaoe mama wa watoto wako, ukimtafuta waza watoto wako watakuwa na mama wa aina gani siyo wewe unampenda kwa kiwango gani au anavutia kwa kiwango gani. Upendo utakuja tu, Mtu anayekujali, anakupikia, amekupa watoto na anawalea, anasimamia biashara zako vizuri kwanini usimpende in time? Labda uwe na mapepo. Na wewe usiwe Mpenda Ngono za nje kupitiliza.