Kipaumbele cha Magufuli ni Ilani ya CCM

Kipaumbele cha Magufuli ni Ilani ya CCM

Magufuli is a good "manager" but he is not a good "leader" kwaiyo hafai kuwa rais bali anafaa zaidi kuwa waziri mkuu, katibu mkuu n.k
Kazi ya meneja ni kusimamia utekelezaji wa mipango. Lakin kazi ya kiongozi ni kusoma alama za nyakati, kubuni na kuonesha dira kisha kuhakikisha mameneja wanatimiza wajibu wao.
 
mimi nijuavyo mgombea razima uwe na jambo maalum la kufanya.Basi magufuri ni roboti mpaka uswichi

Mimi nakubaliana na wewe miamia Mimi nadhani haya ni matumizi mabaya ya vipaji magufuli ana kipaji cha kutumwatumwa na kupewa maagizo na huyasimamia kwa ukamilifu PM ndo ilikuwa saizi yake
 
Wengi hawajui hili, ukiisoma ilani na ukaitekeleza vizuri hakuna tatizo litabaki nchi hii.Sikuzote uwa tuna ilani nzuri mno, utekelezaji wa viwango na kasi ndio unaojitajika na Magufuli sina shaka atafanya hili.
kwa mfumo uliopo, tusitegemee maajabu kutoka kwa magufuli! Tuiipitishe kwanza katiba ya tume ya warioba na kuikataa ya ccm ndo watanzania tutakuwa na uwezo wa kuwabana viongozi wetu wafanye yale tunayotaka watufanyie...labda wewe kama ni mtaalam wa ilani za vyama, tuambie zinatekelezwaje na watawala na jinsi wanavyoshughulikia masuala kama ya rushwa na ufisadi?
 
Sasa ndugu hujui kuwa mgombea vipaumbele vyake vinawekwa kwenye kitu kinachoitwa Ilani?ndiyo atakayotuuzia ili tumpigie kura.

Pamoja na ilani ya chama, na yeye kama yeye anapaswa kuwa na priorities zake, kwan kikwete alipoanzisha mchakato wa katiba ilikuwa kwenye ilani?? Lazima awe na vision na mission,..
Mkapa aliwahi kuiweka ilani ya chama pembeni akafanya yake
 
Ujuavyo sivyo, kuna nchi ilani inatolewa na mgombea kama Marekani, lakini kwa Tanzania mgombea anayewakilisha chama anaenda kuuza kile ambacho chama kimepanga kifanyike, kumbuka chama ni jumuiya ya watu,wanakaa na kukubalina ni kipi kifanyike kwa wakati fulani, juzi wamepitisha ilani ya CCM 2015-2020, anayeibeba ilani hii ni mgombea urais.

Ni wajibu wake kuhakikisha anawaelewesha wananchi kilichopo kwenye ilani na akishinda akatekeleze yote yaliyopo kwenye ilani, ilani inabeba kila kitu unachokiwaza wewe,kipo mle Iwe utawala bora, iwe mapambano ya rushwa, iwe kilimo, iwe fursa kwa vijana na wanawake, elimu n.k vyote vipo mle...wajibu wake ni kuhakikisha hayo anayatekeleza vizuri na kwa kasi

Katiba mpya haikuwa kwenye ilani ya CCM.... Hapo unasemaje...
 
Pamoja na ilani ya chama, na yeye kama yeye anapaswa kuwa na priorities zake, kwan kikwete alipoanzisha mchakato wa katiba ilikuwa kwenye ilani?? Lazima awe na vision na mission,..
Mkapa aliwahi kuiweka ilani ya chama pembeni akafanya yake

Mkapa aliweka prmbeni ilani ya chama... Akaanza kutekeleza ilani ya CUF....
Hata kwa JMK, aliweka pembeni ilani hake akaanza kutekeleza ahadi zake binafsi za ajabu ajabu kama kuwa ana ambulance za pikipiki/bajaji
 
Wewe subili awe raisi ndo utajua Magufuli nani? Wizara alizoziongoza watendaji wanamkubali kwa uongozi wake na ubunifu wake. Akikwambia ilani lazima ujue kwamba ilani inabebe kila kitu unacho kifikilia. Kwahiyo kila mwaka kwenye budget kutakuwa na vipaumbele vyake . Mwenyewe anaamini ilani ya chama imebeba mambo yote ambayo wanainchi wanayaitaji na akiyasimamia vizuri kila mwananchi ataridhika.
 
ok muda sio mrefu saana ulobaki....sijui atakariri na kila jambo kwenye hiyo ilani na ni la ngapi na liko page gani!

Kimsingi ilani ya uchaguzi chama na mgombea mwenyewe plus wanachama wa chama husika wanatakiwa waielewe na kuanza kuipigania, nimekusoma sehemu nimekuelewa kuhusu mgombea kuwa na vipaumbele, kimsingi unaweza ukaangalia kwenye ilani ya uchaguzi mambo yaliyopo na kama anaona kuna jambo moja linamfurahisha akaamua kulishikia bango lifanyike (si unajua tena sio kama kilichopo kwenye ilani kinafanyika), kwa Mgufuli nikimlinganisha na JK naona kuna tofauti kwani JK alikuwa anaulia mingo uraisi kwa miaka 10 tangu ile 1995 alipoukosakosa hivyo kama kujipanga alijipanga achilia mbali miaka ile mingine michache kabla ya 1995 kutangaza nia. Nadhani tumpe muda hii wiki labda atakuja maana hata kwenye udhamini hakuwa akienda kwa mashamsham hivyo labda ndio strategy yake aliyoamua. Hapa nadhani anaangalia wapi mtangulizi wake amepita na wapi anatakiwa aboreshe alafu mwisho wa siku aruke na za kwake (namsemea utasema rafiki yangu)
 
Pamoja na ilani ya chama, na yeye kama yeye anapaswa kuwa na priorities zake, kwan kikwete alipoanzisha mchakato wa katiba ilikuwa kwenye ilani?? Lazima awe na vision na mission,..
Mkapa aliwahi kuiweka ilani ya chama pembeni akafanya yake
Katiba mpya haikuwa kwenye ilani ya CCM.... Hapo unasemaje...
Kama anayo yake angeyapeleka kwenye timu ya iliyokuwa inaandika hiyo ilani, ideally ilani inacontain mawazo ya wanachama.Inawezekana Magufuli pia aliyapeleka mawazo yake kule.

Kama mgombea unayewakilisha kundi huwezi ukaanza kuuza mawazo yako binafsi wakati umetuma kwa niaba ya;miongoni mwa sababu Dr Slaa alikataa kwenda kwenye mdahalo wa vyama juu ya uchaguzi mwezi uliopita alisema hana cha kuongea maana hawana ilani bado, ndio ustaarabu wa siasa za kundi.

Ilani sio static document, baada ya kuingia madarakani na kuanza kuietekeleza, evaluation inafanyika from time to time kuona mmefikia wapi, changamoto zilizopo, na nini namna bora zaidi ya kutimiza hilo, na mengineyo.

Umetoa mfano wa Mkapa, Mkapa baada ya kuanza kuifanyia kazi ilani ya 1995, akaona wazi kuwa ilikuwa too ambitious na isingewezekana kuitimiza yaliyomo ndani ya miaka 5, akarudi kwenye chama kwa wenye ilani na kusema wazi kuwa ilani ile haitekelezeki, modifications zikafanyika na kazi ikaendelea.
 
Ccm inayo ilani pia mgombea razima uwe na vipaumbele pls elewa.Magufuri atwambie yeye anakitu gani zaidi ya wengine.

kama wewe hapo nyuma hutompa kura yako, mke wako na dada zako pale mbele watamjazia kura za kutosha tu mkuu u can count on that
 
kwa mfumo uliopo, tusitegemee maajabu kutoka kwa magufuli! Tuiipitishe kwanza katiba ya tume ya warioba na kuikataa ya ccm ndo watanzania tutakuwa na uwezo wa kuwabana viongozi wetu wafanye yale tunayotaka watufanyie...labda wewe kama ni mtaalam wa ilani za vyama, tuambie zinatekelezwaje na watawala na jinsi wanavyoshughulikia masuala kama ya rushwa na ufisadi?

Nin kinawashinda sasa kuwabana hao viongozi kitakachoongezeka kwa katiba ya Warioba?hakuna kitu kama hicho.

Hawa hawa unaosema wabunge wenu wabovu wanakuja sasa majimboni na mtawachagua.

Katiba ni document tu, katiba haileti muujiza, yenyewe kama yenyewe haileti mabadiliko bali mabadiliko yapo kwa watu, kama ile ya kupata saini za kutokuwa na imani na mbunge hasara yake tutapoteza pesa nyingi kurudiarudia chaguzi na tukienda kwenye uchaguzi yuleyule mbunge bado akashinda kwenye uchaguzi.Kuwa realistic.
 
Yaani ina maana yeye kama mtu anayetaka kuwa rais wa nchi hii hana maono yoyote?...I mean hata kilichopo ndani ya ilani hakijui?...otherwise angesema basi kwamba ntasimamia /nitahakikisha hiki na hiki na hiki ambacho ndicho basis ya ilani yetu au tuseme vipaumbele vya ilani yetu
Nahofu anaweza kuwa mtu wa kuambiwa tu .....mzee tunatakiwa tufanye hivi....na yeye anafanya!!!

Muda huo haujafika, saizi anatoa salaam tu.
 
Nilikwishasema na nitarudia kusema, msitegemee jipya kutoka CCM piitia kauli mbiu ya Mh. Magufuli wakati wa mchakato wa kuchukua fomu za kuwania uwakilishi katika uchaguzi mkuu.

Katika nchi zinazojielewa, kuna priorities za Nchi ambazo mgombea anatakiwa kuzi_meet kwanza na baadaye kumeet priorities za chama atokacho. Wakati wa kampeni ni kuelezana huo utekelezaji utakuwa wa namna gani tu!

Sasa with CCM sera zile zile,ilani ile ile, siasa zilezile, kinachobadilika hapa ni figure tu! Kama wameshindwa kusimamia "ilani" hiyo kwa countless years no matter how 'beautiful'' hiyo ilani iko hawatufai. Hataweza kuwawajibisha wazee, we are past that time of HOPING 'huyu ataweza kusimamia ilani yetu'.

Ilani ya chama iinafuata dira ya nchi, inaandaa mipango ya kuelekea kwenye lengo hilo la kitaifa, hizo priority unazozima tayari zipo humo.

Hii kali, eti wametekeleza ilani hiyo hiyo kwa countless years?inaonyesha ata hujui ilani ni nin!ebu kabla ya kuandika maelezo marefu elewa mada inayozungumzwa.
 
mtoto wa nyoka ni nyoka.Katiba mpya ndioooo,gesi ndioooo leo raisi
 
Naomba wale walio kwisha ona vipaumbele vya huyu ndg magufuri wanisaidie mana me naona kama katoka 1 kwenda 4
 
Habari zenu

wakuu nimesikitishwa sana na kitendo cha watanzania wengi kusahau gafla matatizo,shida,ufisadi na hali mbaya ya kiuchumi yaliyosababishwa na mfumo mbovu wa CCM na sasa wameanza kuwa na imani na CCM baada ya kumteua Dr John pombe Magufuli.

Watanzania Magufuli hawezi kufanya jipya lolote ndani ya mfumo mbovu wa ccm,Magufuli ni sawa na CHAI. Huwezi kuzuia chai kwa kubadili aina ya chai bali naweza kuzuia chai kupoa kwa kubdili aina ya chupa ya chai. Magufuli ni chai mpya ndani ya chupa ileile ya chai ya zamani LAZIMA ITAPOWA TU

TAFAKARI
 
Naomba wale walio kwisha ona vipaumbele vya huyu ndg magufuri wanisaidie mana me naona kama katoka 1 kwenda 4
Usiwe mtu wa kuropoka Alishakwambia toka day one kuwa yeye ni mtu wa chama, hivyo ilani ya chama ndimo kuna vipaumble vya chama na si vya magufuri. Vipi ukawa babu ana vipaumbele vyake au vya cdm?
 
... vipao mbele vyake ni ilani ya chama .

Huyu jamaa hana "visheni yake binafsi"

ana fanya pale chama kitakapo muambia
 
Back
Top Bottom