Kipaumbele cha Magufuli ni Ilani ya CCM

Kipaumbele cha Magufuli ni Ilani ya CCM

Inaonekana Bado anamawazo tegemezi anacho ambiwa aseme hata kama haridhiki nacho ndicho hichohicho atasema.Mawazo yakupewa achanganye na yake.


anajua anachokifanya sio wale wanaopayuka na kuongea hovyo hovyo,
 
Ujuavyo sivyo, kuna nchi ilani inatolewa na mgombea kama Marekani, lakini kwa Tanzania mgombea anayewakilisha chama anaenda kuuza kile ambacho chama kimepanga kifanyike, kumbuka chama ni jumuiya ya watu,wanakaa na kukubalina ni kipi kifanyike kwa wakati fulani, juzi wamepitisha ilani ya CCM 2015-2020, anayeibeba ilani hii ni mgombea urais.

Ni wajibu wake kuhakikisha anawaelewesha wananchi kilichopo kwenye ilani na akishinda akatekeleze yote yaliyopo kwenye ilani, ilani inabeba kila kitu unachokiwaza wewe,kipo mle Iwe utawala bora, iwe mapambano ya rushwa, iwe kilimo, iwe fursa kwa vijana na wanawake, elimu n.k vyote vipo mle...wajibu wake ni kuhakikisha hayo anayatekeleza vizuri na kwa kasi
Yaani ina maana yeye kama mtu anayetaka kuwa rais wa nchi hii hana maono yoyote?...I mean hata kilichopo ndani ya ilani hakijui?...otherwise angesema basi kwamba ntasimamia /nitahakikisha hiki na hiki na hiki ambacho ndicho basis ya ilani yetu au tuseme vipaumbele vya ilani yetu
Nahofu anaweza kuwa mtu wa kuambiwa tu .....mzee tunatakiwa tufanye hivi....na yeye anafanya!!!
 
Wanajamvi mnisaidieni Magufuri anaulizwa kipaumbele chake,anasema ni Ilani ya CCM.Huyu mtu kweli amejiandaa au anajua anachotakiwa kufanya?

Chanzo: EATV

wewe pengine unatokea kwenye lile kudi linalotembea na mafile ya mipasho badara ya kuwa na ilani,
 
Magufuli ni president to be. Watanzania tunahitaji Rais mtekelezaji sio mropokaji kama Dr Slaa. Vipaumbele vya mgombea vipo kwenye ilani ya chama na kama ana ya kwake ataongezea.

Vipi jana hukumsikia akiainisha atakayoyafanya ikiwemo kupambana na wala rushwa na mafisadi.Pia wakati anamteua mgombea mwenza mbona alisema ataendelea kumpa fursa mwanamke ktk ngazi mbalimbali za maamuzi? Au wewe unayo ya kwako unayotaka kuyasikia.
 
mimi nijuavyo mgombea razima uwe na jambo maalum la kufanya.Basi magufuri ni roboti mpaka uswichi
Hiyo ni awamu ya nne tu ndio ilikuwa na ahadi za rais vinginevyo mgombea anasimamia utekelezaji wa ilani ya uchaguzi wa chama chake mkuu mambo mengine ni mbwembwe na wengi hawatekelezi. Ni sawa na mbunge anakuja kuomba kura anasema nitajenga daraja sijui nitafanya nini alafu anapata kura anasepa
 
Wewe ndiyo zuzu kweli unataka atekeleze vitu vya kichwani mwake? Kiongozi anayeteuliwa na chama anatakiwa kutekeleza alichotumwa na chama siyo vya kichwani mwake. Hata kazini kuna organisation strategic plan. CEO wa kampuni hatakiwi kwenda nje ya strategic plan. Ilani ya chama ndiyo strategic plan. Kiongozi atakayeenda kinyume na hiyo hafai.

Na kwa utaratibu huo ni kwamba assumption inajengwa kuwa ilani ndo inayouzwa kwa wananchı na ndo inayopigiwa kura.Tukisha kuwa na mgombea binafsi, huyo ndiye atakuwa na vipaumbele pamoja na ilani yake.Km sehemu ya utekelezaji wa ilani Pombe amesema atahakıkisha uwajibakaji kwa watendaji na watumishi.Pia atachukua hatua kali wabadhilifu na wezı wa mali za umma.
 
Yaani ina maana yeye kama mtu anayetaka kuwa rais wa nchi hii hana maono yoyote?...I mean hata kilichopo ndani ya ilani hakijui?...otherwise angesema basi kwamba ntasimamia /nitahakikisha hiki na hiki na hiki ambacho ndicho basis ya ilani yetu au tuseme vipaumbele vya ilani yetu
Nahofu anaweza kuwa mtu wa kuambiwa tu .....mzee tunatakiwa tufanye hivi....na yeye anafanya!!!

unamjua magufuli? au unatumia miemuko ya siasa kujadili hii hoja, unaweza kweli ukawambia watu kuwa magufuli ni mtu wa kuambiwa ?uchambuzi wako ni wa hovyo,
 
Yaani ina maana yeye kama mtu anayetaka kuwa rais wa nchi hii hana maono yoyote?...I mean hata kilichopo ndani ya ilani hakijui?...otherwise angesema basi kwamba ntasimamia /nitahakikisha hiki na hiki na hiki ambacho ndicho basis ya ilani yetu au tuseme vipaumbele vya ilani yetu
Nahofu anaweza kuwa mtu wa kuambiwa tu .....mzee tunatakiwa tufanye hivi....na yeye anafanya!!!
Ilani ya uchaguzi ndio kwanza ipo kwenye final touch na jibu alilotoa ni sahihi kabisa kuliko kuanza kutema cheche alafu baadae tuanze siasa bwana, hapo aangalie ilani inasemeje alafu ajipange namna gani ya kufanya mambo
 
Marehemu Kabuye alikuwa mtu wa kwanza kumuangusha Magufuli ubunge chato. Huyu marehemu alikuwa Mtaalam Wa kutumia baisikeli kwenye kampeni!
 
Wanajamvi mnisaidieni Magufuri anaulizwa kipaumbele chake,anasema ni Ilani ya CCM.Huyu mtu kweli amejiandaa au anajua anachotakiwa kufanya?

Chanzo: EATV

hivi ni kuuliz e swali
hivi wale wabunge wanaopitanga na vipaombele vyao kuwa nitajenga madaraja,barabara na nyumba za watumishi wakiongozwa na mawazo binafsi walishayafanya hayo?

kama sio basi jua magufuli anajua anachokifanya ,hana sifa za kijinga

 
Magufuli ni mjanja. Hataki kuingia kwenye mtego wa kufanya kampeni kabla ya uchaguzi ili awekewe pingamizi. Hapa anacheza na akili za watu.

Subirini kampeni zianze
 
  • Thanks
Reactions: cpt
Marehemu Kabuye alikuwa mtu wa kwanza kumuangusha Magufuli ubunge chato. Huyu marehemu alikuwa Mtaalam Wa kutumia baisikeli kwenye kampeni!

unaleta habari za marehemu hapa,sio mahali pake,
 
Magufuli ni mjanja. Hataki kuingia kwenye mtego wa kufanya kampeni kabla ya uchaguzi ili awekewe pingamizi. Hapa anacheza na akili za watu.

Subirini kampeni zianze

mkuu wengi hawajui wanazani kukurupuka na kupayuka mbinu zako ndo ushindi,kumbe ni kumpa adui wako silaha,

 
Magufuli ni administrator not a leader.

Ndiyo maaana Anasimamia sheria kwa kwenda Mbele bila kuangalia mazingira Kama yatawaaffect wananchi au hata Chama chake. Tatizo Kubwa ni kwamba sheria Nyingi ni mbovu na kandamizi. Hivyo wananchi Wajiandae kuumia.

Sitashangaa akadumu miaka 5 na sio 10 sababu timbwili lake linaweza kusababisha watu wakaichukia Zaidi CCM. Na wakubwa Wenye nchi wanaweza wakaguswa maslahi Yao.

Disadvantage nyingine ni kwamba yeye sio politician so anaweza akagusa maslahi ya wakubwa hapo Ndiyo itakuwa kasheshe.


Sina Shaka na uwezo wake kwenye kazi. Ni mzuri kwenye usimamizi ila tusitegemee any thinking outside the box hapo.

Kwa nchi yetu ina Raha na Karaha Yake.

Ila kwa sasa hivi Tanzania tunahitaji Mtu aina Yake kunyoosha watendaji waliolala usingizi.

Natamani Waziri Mkuu awe Mwakyembe hii nchi itapaa.
 
Nadhani watanzania ndio tulivyo, na baada ya miaka 3 tutaanza kusema hafai hafai hafai. Hatuna ujuzi wa kutambua nani afanye nini katika nafasi gani. Majuto ni mjukuu ila namuona angefaa sana kwenye uwaziri mkuu na Rais akawa mtu wa calibre ya mwandosya hivi, nawaza tuuu nisameheeni sana
 
Nashangaa sana watu wanavyoongea ujingaujinga kama vile hawajasoma! Wapi wameandika kuwa ni lazima kiongozi awe na ilani yake mwenyewe? Tanzania ya sasa tunamtaka kiongozi anayeweza kutekeleza ilani ya chama chake. Baasi! Hatutaki kingine kwa sababu waliopita hawajatekeleza ilani za chama chao kwa ukamilifu na kasi. Hayo mengine ni ya ziada.
 
hivi ni kuuliz e swali
hivi wale wabunge wanaopitanga na vipaombele vyao kuwa nitajenga madaraja,barabara na nyumba za watumishi wakiongozwa na mawazo binafsi walishayafanya hayo?

kama sio basi jua magufuli anajua anachokifanya ,hana sifa za kijinga

mmmm weweee usifananishe mbunge na rais.....Kkwete alisema nitajenga chuo kikuu dodoma....alisema nitawapa watanzania katiba mpya....yote hayo aliyafanya(japo la katiba limekwamia hapo lilipofikia)....Na yote hayo hayakuwa popote kwenye ilani ya CCM....anyway nataka ujue tu kuwa Rais hawezi kufananishwa na mbunge.....
Mkapa aliahidi kutujengea uwanja wa kisasa wa mpira wa miguu...you know it...the fabulous national stadium!
 
unamjua magufuli? au unatumia miemuko ya siasa kujadili hii hoja, unaweza kweli ukawambia watu kuwa magufuli ni mtu wa kuambiwa ?uchambuzi wako ni wa hovyo,
Uko wapi huo wa kwako wa maana?....a robotic leader!?...you are programmed on how to act......you have no vision for your country....huwezi kusema unataka, as a president to be, kuona tanzania ikifika sehemu fulani,kuwaona watanzania wakiwa na hali fulani tofauti na sasa?....
 
Ilani ya uchaguzi ndio kwanza ipo kwenye final touch na jibu alilotoa ni sahihi kabisa kuliko kuanza kutema cheche alafu baadae tuanze siasa bwana, hapo aangalie ilani inasemeje alafu ajipange namna gani ya kufanya mambo
ok muda sio mrefu saana ulobaki....sijui atakariri na kila jambo kwenye hiyo ilani na ni la ngapi na liko page gani!
 
Back
Top Bottom