Kipaumbele cha Magufuli ni Ilani ya CCM

Kipaumbele cha Magufuli ni Ilani ya CCM

mimi nijuavyo mgombea razima uwe na jambo maalum la kufanya.Basi magufuri ni roboti mpaka uswichi

wewe mnafiki nani kakwambia hana kipaombele chake,acha siasa za hovyo zisizo kuwa na tija,
 
Lengo ni jambo muhimu kwa kiongozi.Magufuri hajielewi wala hajui afanye nini.Ndio maana alisema atawalinda wazee

Tusihukumu mapema tusubiri muda wa Kampeni, tuisome Ilani yao hapo ndio tutaona msimamo wa Magufuli .

Anaweza kuahidi kipaumbelechake sasa hivi Kumbe kimo kwenye Ilani ya chama .

Mbivu na mbichi ni muda wa Kampeni ,ndio maana JK alitoa ahadi zaidi ya sabini bila kujielewa .

Kwa sasa Magufuli anatii chama na ndio kilichomfikisha hapo, atakapoona Ilani ya chama hauziki ndio ataanza kuropoka.

Ndio maana JK alisema Urais wake ni wakifamilia baada ya kutolewa jasho kwenye kampeni.
 
Wanajamvi mnisaidieni Magufuri anaulizwa kipaumbele chake,anasema ni Ilani ya CCM.Huyu mtu kweli amejiandaa au anajua anachotakiwa kufanya?

Chanzo: EATV

Sasa ndugu hujui kuwa mgombea vipaumbele vyake vinawekwa kwenye kitu kinachoitwa Ilani?ndiyo atakayotuuzia ili tumpigie kura.

Mkuu nchi hii vyama vina Ilani nzuri sana, tunasheria nzuri sana za nchi .

Tatizo ni usimamizi wa sheria ndio.

Nilikwishasema na nitarudia kusema, msitegemee jipya kutoka CCM piitia kauli mbiu ya Mh. Magufuli wakati wa mchakato wa kuchukua fomu za kuwania uwakilishi katika uchaguzi mkuu.

Katika nchi zinazojielewa, kuna priorities za Nchi ambazo mgombea anatakiwa kuzi_meet kwanza na baadaye kumeet priorities za chama atokacho. Wakati wa kampeni ni kuelezana huo utekelezaji utakuwa wa namna gani tu!

Sasa with CCM sera zile zile,ilani ile ile, siasa zilezile, kinachobadilika hapa ni figure tu! Kama wameshindwa kusimamia "ilani" hiyo kwa countless years no matter how 'beautiful'' hiyo ilani iko hawatufai. Hataweza kuwawajibisha wazee, we are past that time of HOPING 'huyu ataweza kusimamia ilani yetu'.
 
Kila ilani inakipaumbele mkuu.

Mkuu, utaratibu wa mgombea kupitia chama cha siasa ni kwa ilani ya chama ndo inainishe vipaumbele vya serikali itakayoundwa.Mgombea mwenyewe anategemewa kwenye umahiri wake wa kutekeleza ilani hiyo.Hata ilanı ya magamba huwa ni nzuri tatizo ni maongo, hayaitekelezi kwa namna yanavyoinadi.
 
Nilikwishasema na nitarudia kusema, msitegemee jipya kutoka CCM piitia kauli mbiu ya Mh. Magufuli wakati wa mchakato wa kuchukua fomu za kuwania uwakilishi katika uchaguzi mkuu.

Katika nchi zinazojielewa, kuna priorities za Nchi ambazo mgombea anatakiwa kuzi_meet kwanza na baadaye kumeet priorities za chama atokacho. Wakati wa kampeni ni kuelezana huo utekelezaji utakuwa wa namna gani tu!

Sasa with CCM sera zile zile,ilani ile ile, siasa zilezile, kinachobadilika hapa ni figure tu! Kama wameshindwa kusimamia "ilani" hiyo kwa countless years no matter how 'beautiful'' hiyo ilani iko hawatufai. Hataweza kuwawajibisha wazee, we are past that time of HOPING 'huyu ataweza kusimamia ilani yetu'.

Mapendekezo!?
 
Ujuavyo sivyo, kuna nchi ilani inatolewa na mgombea kama Marekani, lakini kwa Tanzania mgombea anayewakilisha chama anaenda kuuza kile ambacho chama kimepanga kifanyike, kumbuka chama ni jumuiya ya watu,wanakaa na kukubalina ni kipi kifanyike kwa wakati fulani, juzi wamepitisha ilani ya CCM 2015-2020, anayeibeba ilani hii ni mgombea urais.

Ni wajibu wake kuhakikisha anawaelewesha wananchi kilichopo kwenye ilani na akishinda akatekeleze yote yaliyopo kwenye ilani, ilani inabeba kila kitu unachokiwaza wewe,kipo mle Iwe utawala bora, iwe mapambano ya rushwa, iwe kilimo, iwe fursa kwa vijana na wanawake, elimu n.k vyote vipo mle...wajibu wake ni kuhakikisha hayo anayatekeleza vizuri na kwa kasi


mkuu wengine hawana ilani wakija ni mipasho tu adi unajiuliza hawa kweli wanajua wanachokifanya hao vipi?
 
Wanajamvi mnisaidieni Magufuri anaulizwa kipaumbele chake,anasema ni Ilani ya CCM.Huyu mtu kweli amejiandaa au anajua anachotakiwa kufanya?

Chanzo: EATV

Wewe ndiyo zuzu kweli unataka atekeleze vitu vya kichwani mwake? Kiongozi anayeteuliwa na chama anatakiwa kutekeleza alichotumwa na chama siyo vya kichwani mwake. Hata kazini kuna organisation strategic plan. CEO wa kampuni hatakiwi kwenda nje ya strategic plan. Ilani ya chama ndiyo strategic plan. Kiongozi atakayeenda kinyume na hiyo hafai.
 
wewe mnafiki nani kakwambia hana kipaombele chake,acha siasa za hovyo zisizo kuwa na tija,

Wadanganyika tunao upeo mdogo sana.Kasema yeye mwenyewe au Umekunjwa viroba jamaa!
 
Inaonekana Bado anamawazo tegemezi anacho ambiwa aseme hata kama haridhiki nacho ndicho hichohicho atasema.Mawazo yakupewa achanganye na yake.
 
Wewe ndiyo zuzu kweli unataka atekeleze vitu vya kichwani mwake? Kiongozi anayeteuliwa na chama anatakiwa kutekeleza alichotumwa na chama siyo vya kichwani mwake. Hata kazini kuna organisation strategic plan. CEO wa kampuni hatakiwi kwenda nje ya strategic plan. Ilani ya chama ndiyo strategic plan. Kiongozi atakayeenda kinyume na hiyo hafai.

Mkuu tulia kwanza uelewe maana ya vipaumbele.Magufuri yuko too mechanical kiongozi asiye na hekima
 
Kwa hilo tuko sahihi.
Vipaumbeke JK havikutekelezeka vingi kwa sababu havipo kwenye ilani ya ccm, mojawapo katiba mpya
 
Mkuu tulia kwanza uelewe maana ya vipaumbele.Magufuri yuko too mechanical kiongozi asiye na hekima

najua wewe ni mvivu ndo maana unapenda viongozi wanaobembelezana katika mambo ya msingi,
 
Kwa hiyo mnataka apingane na mawazo ya waliomteua.?

Tatizo la Tanzania sio Ilani ila usimamizi na utekelezaji wa hiyo Ilani.

Hapo umesema vizuri. Ilani safi ikiwepo na akawepo msimamizi imara basi maendeleo yatapatiakana. Ilani ni mwongozo wa mambo yanayopaswa kufanywa na kusimamiwa na kiongozi aliyepewa dhamana. Siyo kiongozi kukurupuka na yake kila anapoamka. Ilani inatokana na tafiti iliyokusanya maoni ya wananchi kulingana na mahitaji yao, hivyo ilani inajibu utatuzi wa kero za zinazowakabili wananchi
 
Back
Top Bottom