Mimi ni mmoja wa watu ninaokwazwa sana na tabia ya rais Kikwete kuchanganya kiingereza anapoongea kiswahili kwenye hadhila mfano mzuri ni juzi kwenye mambo ya mitaa.Ninakwazwa kwa sababu nyingi chache ni hizi hapa:
1. Siamini kwamba rais Kikwete kiswahili kinampa shida kiasi cha kumlazimu kuchanganya kidhungu, Kikwete ni mtu wa pwani anajua kiswahili kuliko wengi wetu.
2. Pamoja na mapungufu yake, siamini kwamba kiswahili hakijitoshelezi ndio maana inabidi Kikwete akisaidie kukiazimia maneno kutoka kwenye kiingereza.
3. Si watanzania wote wanajua kiingereza kwa hiyo rais anapochanganya kiingerza kwenye hotuba au maongezi yeyote ya kiswahili hawatendei haki watanzania wasiojua Kiingereza.
4. Watanzania tuko kwenye mkakati wa kukifanya kiswahili kuwa lugha ya maziwa makuu, afrika ya kati na zaidi ya hapo ndio maana nchi hizo zinajitahidi sana sasa kujifunza kiswahili. Kitendo cha rais kukiabudu kiingereza anarudisha nyuma juhudi zetu hizi. Wito nautoa kwa washauri wa rais wamuombe aachane na tabia hii ya kuchanganya sana kiingereza kwenye shughuli za kiswahili kwani haileti picha nzuri kwa wengine kwani inajulikana sisi ndio waasisi wa kiswahili, ni lazima tuoneshe kukithamini kiswahili chetu.
1. Siamini kwamba rais Kikwete kiswahili kinampa shida kiasi cha kumlazimu kuchanganya kidhungu, Kikwete ni mtu wa pwani anajua kiswahili kuliko wengi wetu.
2. Pamoja na mapungufu yake, siamini kwamba kiswahili hakijitoshelezi ndio maana inabidi Kikwete akisaidie kukiazimia maneno kutoka kwenye kiingereza.
3. Si watanzania wote wanajua kiingereza kwa hiyo rais anapochanganya kiingerza kwenye hotuba au maongezi yeyote ya kiswahili hawatendei haki watanzania wasiojua Kiingereza.
4. Watanzania tuko kwenye mkakati wa kukifanya kiswahili kuwa lugha ya maziwa makuu, afrika ya kati na zaidi ya hapo ndio maana nchi hizo zinajitahidi sana sasa kujifunza kiswahili. Kitendo cha rais kukiabudu kiingereza anarudisha nyuma juhudi zetu hizi. Wito nautoa kwa washauri wa rais wamuombe aachane na tabia hii ya kuchanganya sana kiingereza kwenye shughuli za kiswahili kwani haileti picha nzuri kwa wengine kwani inajulikana sisi ndio waasisi wa kiswahili, ni lazima tuoneshe kukithamini kiswahili chetu.