Umeongea kitu cha msingi sana mkuu The Boss. Huwezi kuona umuhimu wa tume huru mpaka uwe mtanzania mzalendo au uwe mpinzani wa CCM. Sasa hapa kuna mawili Kingunge ameongea kama mpinzani wa ccm au ameongea kama mtanzania mzalendo?. Kingunge aliikataa rasimu ya katiba ya Warioba yenye tume huru kwakuwa alikuwa akilinda maslahi binafsi zaidi kuliko maslahi mapana ya Tanzania, Kingunge hakujua kesho yake nini kitatokea na wapi atakuwa. Kikubwa ambacho tunapaswa kujifunza kutoka kwa Kingunge ni kwamba tunapaswa kusimamia ukweli bila kujali wapi tulipo na bila kuangalia maslahi yetu binafsi yataathirika vipi. God Bless Tanzania.