Kingunge, kweli ubaya hauna kwao...

Kingunge, kweli ubaya hauna kwao...

Kuna jambo moja mnashindwa kulielewa, nalo ni kwamba hakuna kitu kama hiyo mnayoiita Tume huru Dunia hii, ila kilichopo ni Mshindi na aliyekataliwa na Watanzania, kama Watanzania wakiamua kuiingiza chadema madarakani watafanya hivyo kama bado hawajaamua kama ilivyo sasa na itabakia kuwa hivyo na huo ndio Ukweli pekee Dunia hii, kama vile kifo!
Mkuu kwani chadema pekee ndo inafaa kuingia ikulu? na sio chama chochote cha upinzani?
 
Nimesoma jinsi Kingunge alivyozungumzia umuhimu wa
'tume huru ya uchaguzi'...

nimejikuta nakumbuka huu msemo maarufu 'ubaya hauna kwao'

Kwamba jambo likiwa baya ni baya tu....kokote kule likienda litachukiwa
na ukinyamaza wakati mtu mwingine anafanyiwa ubaya basi
usishangae ubaya huo ukaja kufanyiwa wewe au ndugu yako na wewe
ukaumia na kulia kama hao wengine..


Wizi wa kura ni jambo baya saana....ni kudhulumu haki za watu

Kingunge sasa anaongea kwa uchungu sana.....

natamani kumuuliza....why now?

Lini tuliwahi kuwa na tume huru ya uchaguzi? ...

Wazee walisema 'ubaya hauna kwao'......laiti kama

Kingunge,Lowassa Sumaye na wengine wote wange simama kuhesabiwa
kwenye mstari wa haki maisha yao yote...na kupigania 'tume huru' kabla hata
hawajatoka CCM leo tungekuwa mbaali saana....

Na wale wana CCM ambao leo watakejeli kauli ya Kingunge....wajifunze hili
'ubaya hauna kwao'


Wengi wenu hamjui jinsi Lowassa alivyotumia ushawishi wake bungeni kuikataa katiba ya Warioba, kwa kuamini kuwa alikuwa Rais ajaye baada ya JK akaitaka katiba ya zamani ''afaidi mema ya nchi''. Sasa leo yeye na wapambe wake wanakaa upande wa pili wa meza ndipo wanagundua milango imejifunga, too bad!
 
Kwny Mchakato wa Katiba Mpya Kingunge wakati huo akiamini Lowassa angekuwa Ndie Rais wa Tano alimshambulia Jakaya kuwa Taifa halihitaji Katiba Mpya Bali marekebisho madogo madogo tu ya Katiba.

Huyu Mzee hata Kama analoongea ni Muhimu yeye binafsi anaonekana ni Mnafiki sana sana kwa kuwa alikuwemo kwny Bunge la Katiba na hakuzungumzia wala kupigania hiyo Katiba Mpya

Wakati wa bunge la katiba Kingunge akiwa mwana CCM, asingethubutu kusema anayosema leo kwa sababu alikuwa anatetea itikadi ya Chama chake.
 
Nimesoma jinsi Kingunge alivyozungumzia umuhimu wa
'tume huru ya uchaguzi'...

nimejikuta nakumbuka huu msemo maarufu 'ubaya hauna kwao'

Kwamba jambo likiwa baya ni baya tu....kokote kule likienda litachukiwa
na ukinyamaza wakati mtu mwingine anafanyiwa ubaya basi
usishangae ubaya huo ukaja kufanyiwa wewe au ndugu yako na wewe
ukaumia na kulia kama hao wengine..


Wizi wa kura ni jambo baya saana....ni kudhulumu haki za watu

Kingunge sasa anaongea kwa uchungu sana.....

natamani kumuuliza....why now?

Lini tuliwahi kuwa na tume huru ya uchaguzi? ...

Wazee walisema 'ubaya hauna kwao'......laiti kama

Kingunge,Lowassa Sumaye na wengine wote wange simama kuhesabiwa
kwenye mstari wa haki maisha yao yote...na kupigania 'tume huru' kabla hata
hawajatoka CCM leo tungekuwa mbaali saana....

Na wale wana CCM ambao leo watakejeli kauli ya Kingunge....wajifunze hili
'ubaya hauna kwao'
The Boss, umeyasema yote, hata hivyo inafurahisha hayo wanyopigania sasa wameyaona.
 
Ndg zanguni wana jamii hebu acheni mawazo yasiyokuwa na tija katika wakati huu na ujao tusikubali kukaririshwa hivi unapozungumza tume huru lazima ujuwe unachokizungumza na ni vyema ukatowa mifano ili uleweke.

Labda nije na Mfano wa Tume ya Uchaguzi ya Kenya IEBC ikiwa huu ni mfano wa karibu zaidi ambayo tume ni hii iliitwa ni Tume huru iweje leo kenya wanilani tume hiyo na kuiona kuwa haifai ?

Sasa Ushauri wangu kwa waelewa hebu tujiulize kuna Tunzo tele Duniani zinatolewa Umewahi kuskia kuwa kuna Tume bora ya Uchaguzi Duniani,?

Au kwa pamoja tutafute kwenye engeen search Tume 10 bora Duniani tuone tutazipata ? Sasa cha msingi tuamini kuwa tume uwe huru isiwe huru Zaidi itaendana na utendaji wa Tume zetu...

Ifike wakati sasa tuzipongeze tume zetu kwa kazi zinazozifanya kwani zina jukukumu kubwa sana tuache mazowea ya kulalamikia marefa wakati timu zenu hamjaziandaa vyema si kiti kizuri ata kidogo
 
Unadhani hata katiba ikibadilishwa watu wataifuata na italeta maendeleo? Bora tungeomba kwanza tutawaliwe tena na wakoloni kwanza hasa mjerumani.

Kwa ufupi tu sisi ni watu wa ajabu sana siyo kingunge tu.

Ndio maana sifa na thamani ya PhD imeshuka sana mwaka huu!
Huko Kenya walibadili katiba lakini kumbe aheri hata katiba iliyobadilishwa ,katiba bila utashi ni kazi bure kabsa.Hata angekuja malaika hizi katiba za nchi za kiafrika zitazidi kuchezewa tu si mumeona Kenya hivi sasa wanataka kubadili mfumo wa uchaguzi wa kielekitroniki kwa kurudi enzi za mawe kisa watawala wameshituka safari hii hawawezi kuiba kura tena kwa kuutumia mfumo uleule uliowaingiza madarakani baada ya kuthibitiwa WAPINZANI SIO MALAIKA NI WATAFUTA MADARAKA TU .
 
Rafiki yangu kizazi kipi tena?? kizazi cha wacheza pull table, kubeti au kutoboa pua..au labda kizazi cha malaika kwa sasa kizazi cha wanao tumia smart za kupukuta..nitofauti na kizazi cha wakina Patrice Lumumba ,Nelson Mandela, Kenneth Kaunda Mwl Nyerere na wengi walio kua wanatumia barua za mkono sio SMS za sm simu za mezani..wanalikua wanasoma vitabu na wana vitolea mawazo endelevu
Kumbuka tu kipindi cha miaka ya 90s ukisikia kuna udhalim chuoni lazima serikali itokwe na jasho..kwa sasa ni waoga na sio wepesi wa kuthibutu..kwan walikua wanaharaki wa kuleta mapinduzi hasa kwa wanyonge sasa hivi ni wakusifia hata kwenye upuuzi wa macho
Labda nchi zingine lkn sio hapa.."Adui muombe njaa" by Afande Sele

TE="dustless, post: 19015361, member: 394462"]Hawa watu pande zote hawafai tu, labda tusubiri damu changa kabisa ambayo haijawahi shiriki dhambi hii.

Na kama unaona msamaha ndo kila kitu basi hata waliopo leo acha watukandamize mwishoni tutawasamehe.

Imani yangu, nangonjea kizazi kipya kutatua changamoto tulizonazo, sio mizee hii inayotuigizia kwa pande zote mbili.[/QUOTE]
Best
 
Kingunge anazeeka vibaya.Ni kama ana wa enjoy chadema.
Wote wanafiki chadema na Kingunge tu.
CCM wanashabikia na kuunga mkono maswala yanayowabakisha madarakani hata kama hayana faida kwa maendeleo na mustakabali wa watanzania na hili ndilo tatizo letu kuu kama nchi.

Kama ni unafiki CCM ni wanafiki kuliko.
 
Mzee Kingunge mnamlaum bure alikuwepo kwenye bunge la katiba na mambo ya tume huru wala hakuyasemea na kinachochekesha kabisa aliingia katika bunge la katiba kama mjumbe anayetoka kundi la waganga wa kienyeji so hata anayoyaongea hv sasa ni kama ya waganga wa kienyeji so msimshangae
 
Ndg zangu hata bila kina Kingunge hii ni nchi yetu na mustakbali wake uko mikononi mwetu . Katiba nzuri yenye uwazi ni muhimu bila kujali uko CCM au wapinzani wake. Mahitaji yako ya kisiasa na kiuchumi ya leo si ya kesho !!

Tuitafute leo na lisiwe swala la viongozi wa upinzani peke yao bali wananchi wote. Ikiwa ya kina Mbowe na Seif tu wale wanaofaidi leo watafanya hila lisifanikiwe, lakini ikiwa ni hitaji la taifa hatutakwamishana .
 
CCM wanashabikia na kuunga mkono maswala yanayowabakisha madarakani hata kama hayana faida kwa maendeleo na mustakabali wa watanzania na hili ndilo tatizo letu kuu kama nchi.

Kama ni unafiki CCM ni wanafiki kuliko.
Mtu mwaka mmoja tu uliopita aliipinga kwa nguvu zake zote katiba mpya,leo anakuja anawaambia anataka katiba mpya.Aidha amewaona wajinga au anasumbuliwa na matatizo ya akili
 
Ndg zangu hata bila kina Kingunge hii ni nchi yetu na mustakbali wake uko mikononi mwetu . Katiba nzuri yenye uwazi ni muhimu bila kujali uko CCM au wapinzani wake. Mahitaji yako ya kisiasa na kiuchumi ya leo si ya kesho !!

Tuitafute leo na lisiwe swala la viongozi wa upinzani peke yao bali wananchi wote. Ikiwa ya kina Mbowe na Seif tu wale wanaofaidi leo watafanya hila lisifanikiwe, lakini ikiwa ni hitaji la taifa hatutakwamishana .

Katiba mpya inamhusu kila mtu
hata hao CCM inawahusu na ina manufaa kwao
 
Wengi wenu hamjui jinsi Lowassa alivyotumia ushawishi wake bungeni kuikataa katiba ya Warioba, kwa kuamini kuwa alikuwa Rais ajaye baada ya JK akaitaka katiba ya zamani ''afaidi mema ya nchi''. Sasa leo yeye na wapambe wake wanakaa upande wa pili wa meza ndipo wanagundua milango imejifunga, too bad!


Angepigania katiba mpya na tume huru ya uchaguzi labda now angekuwa Ikulu
 
Hivi Ingetokea UKAWA Wakashinda Uchaguzi Wa Mwaka Jana Wangeleta Katiba Ya Warioba ?

Kwangu mimi naona JMP anaweza kuileta kuliko mtu mwingine yeyote...ila hata kama ni mimi si wakati huu kwani kwa sasa anahitaji kuwa na uwezo huu ili atuweke vizuri then tukishajifunza kujituma na kutopenda mabwanyenye dhidi ya walio wengi huko 2025 ndiyo atuletee katiba ya Mh. Warioba....ni maoni yangu!
 
Angepigania katiba mpya na tume huru ya uchaguzi labda now angekuwa Ikulu

Sidhani kama anaamini katika democracy kama ingekuwa hivyo basi yeye kwa influence aliyokuwa nayo leo hii nchi yetu isingefika huku tuliko....Katika wote yeye sidhani kama hata anatakiwa kuzungumza ningekuwa mimi ningeona aibu!
 
Umeongea kitu cha msingi sana mkuu The Boss. Huwezi kuona umuhimu wa tume huru mpaka uwe mtanzania mzalendo au uwe mpinzani wa CCM. Sasa hapa kuna mawili Kingunge ameongea kama mpinzani wa ccm au ameongea kama mtanzania mzalendo?. Kingunge aliikataa rasimu ya katiba ya Warioba yenye tume huru kwakuwa alikuwa akilinda maslahi binafsi zaidi kuliko maslahi mapana ya Tanzania, Kingunge hakujua kesho yake nini kitatokea na wapi atakuwa. Kikubwa ambacho tunapaswa kujifunza kutoka kwa Kingunge ni kwamba tunapaswa kusimamia ukweli bila kujali wapi tulipo na bila kuangalia maslahi yetu binafsi yataathirika vipi. God Bless Tanzania.
 
Back
Top Bottom