stata mzuka
JF-Expert Member
- Nov 25, 2012
- 4,834
- 1,765
Ukawa wametega masikio yao yote ccm kuona inampitisha nani ili nao wafanye mchakato wa kumpitisha babu.
Babu kuwa Rais na siku hiyo Maji yatapanda Mlima
Ukawa wametega masikio yao yote ccm kuona inampitisha nani ili nao wafanye mchakato wa kumpitisha babu.
Babu kuwa Rais na siku hiyo Maji yatapanda Mlima
Ni ili kurahisisha utatuzi wa matatizo lukuki ya jiji la Dar, kwamba waziri akilala akiamka anatoa maamuzi ya haraka kwa manufaa ya wananch. Sambamba na hilo kila mwaka zitajengwa nyumba millioni moja kuendana na sera itakayotungwa kwa ajili ya jiji hilo. Nipashe siku ya leo.
Kwani kuna mtangaza nia gani ambaye hajasema atakachofanya Akiwa raisi?Nani kampa mamlaka ya kupiga kampeni? Chama kina utaratibu wa kutafuta udhamini na si unasimama tu barabarani then unaropoka unayoona yanafaa
Ukilinganisha huyu wa kufunga cctv mitaa ya Dar na huyu wa wizara nani ana nafuu?
Kwani hela za ziara za rais wako anazopigia misele kila siku kwenye nchi za watu bila faida yoyote kwani nani anazilipia? ungetoka nje ya 18 kabla ya ku comment
Akizungumza kwa nyakati tofauti akiwa wilayani Ilala, Temeke na Kinondoni jijini Dar es Salaam, Lowassa alirejea kauli iliyotolewa na Mwalimu Julius Nyerere ya mwaka 1995, kwamba watu wanataka mabadiliko na wakiyakosa ndani ya CCM, watayatafuta nje ya chama hicho.
Mimi nitayaleta haya mabadiliko nikiwa ndani ya CCM. Nagombea urais kwa sababu nauchukia umasikini na nitaunda serikali ya kusaidia wanyonge, kuwafukuza machinga, mamantilie na waendesha bodaboda ni upuuzi. Watu wanatafuta riziki tunawafukuza inatakiwa tuwawekee mazingira mazuri, alisema na kushangiliwa kwa nguvu.
Alisema anauchukia msongamano wa magari jijini Dar es Salaam na iwapo atakuwa Rais atalimaliza tatizo la foleni katika jijini Dar es Salaam kwa miezi sita.
Kutakuwa na waziri anayeshughulika na jiji la Dar es Salaam tu kama ilivyo kwa nchi jirani ya Kenya. Yeye akiamka tu akili yake yote ni kushughulikia changamoto za jiji hili, alisema Lowassa ambaye mara kwa mara alikuwa akiwaimbisha wananchi wimbo wa mchakamchaka, huku akisisitiza kuwa ataiongoza serikali yake kwa mtindo wa mchakamchaka akisema ambaye hataweza atakaa pembeni.
Aliwataka wananchi kujitokeza kwa wingi kujiandikisha katika Daftari la Wapigakura ili wapate fursa ya kumchagua iwapo atapitishwa na chama hicho kugombea urais, huku akiwataka wamuombee kwa maelezo kuwa Mungu ndiye anayepanga kila kitu.
Mrema (Augustine) alikuwa maarufu sana mwaka 1995 mpaka gari lake likawa linasukumwa na wananchi, lakini katika kura za urais hakushinda. Jiandikisheni ili tufanikishe safari ya matumaini, alisema.
Lowassa alisema kutokana na idadi kubwa ya wananchi wanaomuunga mkono anaona kama tayari ameshashinda huku akisisitiza kuwa ameshawafunga goli wagombea wenzake kama anavyofanya mchezaji wa timu ya soka ya Real Madrid, Cristiano Ronaldo.
Kati ya wagombea wote hakuna mwenye uzoefu ndani ya CCM kama mimi. Kumbukeni rais ndiye mwenyekiti wa CCM, alisema.
Aiteka Dar
Lowassa aliwasili katika uwanja wa ndege wa zamani (Terminal 1), saa 2:00 asubuhi akitokea mkoani Arusha.
Mwenyekiti wa CCM wa Dar es Salaam, Ramadhani Madabida alisema wanachama wa mkoa huo waliojitokeza kumdhamini ni 212,150, kati yao kutoka Kinondoni ni 95,251, Temeke (72,100) na Ilala (44,799).
Afananishwa na mtume, Yesu
Akimkaribisha Lowassa Dar es Salaam, Madabida alimfananisha waziri mkuu huyo wa zamani na Mtume Muhammad ambaye alikuwa akitangaza dini lakini alikuwa akipingwa na watu wake wa karibu na kufafanua kuwa kutokana na hali hiyo Mungu alimueleza kuwa hatamuacha na atakuwa pamoja naye.
Madabida lazima ajue kuwa Yesu hakuwa na kashfa ya ufisadi...Kama huyo anayemfananisha naye.....
Hivi huyu Ramadhani Madabida kesi ya kuiuzia MSD ARVs fake imeishia wapi?
Birds of the same feather flocks together!
Wewe humpendi Kama nani, wewe subiri aibu yako, sauiti ya wengi wape..toa hoja za msingi Kama kweli umesoma na unajua, acha kunya kunyaAkacheze na vitukuu vyake huko!!
Anaanza kuwa "dogo" tena, anaongea pumba sana!
Sikapendi sana haka kababu siku hizi, kwanza kalianza kuniboa kwenye bunge maalum la katiba na bado kanaendelea kuniboa kila kanapofungua mdomo! Si kakae kimya tuu!!! aaarrggghhhhh!!!
Hivi huyu Ramadhani Madabida kesi ya kuiuzia MSD ARVs fake imeishia wapi?
Birds of the same feather flocks together!